MAPENZI NA MASOMO
Olivia
alikuwa mpenzi wangu na hadi sasa bado tunapendana kimapenzi.
Wakati
nipo naye chumbani tumemaliza shughuli yetu ya kuondomola.
Olivia
alianza kunisimulia hadithi moja kali aliyosimuliwa na mpenzi wake wa zamani.
Nikamkubalia
“Haya Olivia nipe hiyo hadithi mpenzi”…………”
Rashimail
want to be your friend.'confirm' 'ignore' ulikuwa ni ujumbe ambao macho yangu
yalikutana nao nilipofungua mtandao wa kijamii wa ‘facebook’,sikumbuki kama
nilijifikiria mara mbili kwani niliona ni jambo la kawaida sana kukutana na
'notifications’ kama hizo,na mara zote neno confirm(kubali) lilipata fursa ya
kutumika.hivyohivyo hata kwa Rashimail nilifanya hivyo."You and reshmail
are now friends" ndio ujumbe ulionisindikiza baada ya kukubali ombi lile
kutoka kwa Rashmail.
--------------------------------------------------------------------------------------
Ni kijana mtanashati niliyebahatika kukutana nae pale chuo kikuu cha mtakatifu
Augustine Mwanza,alijipenda kuanzia ndani ya chumba chake hadi mwili
wake,ilikuwa ni nadra sana kumfumania akiwa amevaa nguo aliyoivaa jana,bila
kumnyima haki yake nasema alikuwa anapendeza kila siku,macho yangu ya
kipelelezi na kamera zangu za kipaparazi kamwe hazikufanikiwa kumjua aliyekuwa
ubavu wa pili wa bwana huyu yaani 'MPENZI'. Ukipenda waweza kuniita
kimbelembele lakini ukiniita hivyo basi majina hayo yatakuwa mengi pale chuoni
kwani wengi walikuwa na shauku kubwa ya kujua siri hiyo na kamwe
hawakufanikiwa.
Binadamu hatuna dogo watu washaanza kusema eti huenda jamaa ana matatizo
makubwa tu mwilini mwake ndio maana yuko peke yake licha ya kushobokewa na
wasichana warembo, mh! mimi sikuwa mmoja wao lakin nilijiuliza pia
kulikoni??
Makala mbovu zilizokuwa zinaandikwa na gazeti la chuo
lililojulikana kama ‘Saut voice’ ndo zilinizonivuta zaidi kutaka na mimi siku
moja kuandika katika gazeti hilo lililokosa mvuto siku za hivi karibuni makala
nzuri itakayorudisha heshima ya gazeti hilo.Taratibu nilijenga mazoea na
hatimaye nikafanikiwa kumzoea "THE MOST WANTED" ucheshi wangu ndio
uliomvutia zaidi kupenda kuwa karibu nami pamoja na mchezo wa mpira wa miguu
kwani wote tulikuwa mashabiki wakubwa,haukupita mwezi mzima nikawa nina uwezo
wa kuanza kazi yangu,ni mimi na Adam
kwenye meza moja chumban kwangu ananipa hadithi yake ya maisha yaliyomfanya awe
kama alivyo.
"Aah!! jamani Rashmail..." alianza Adam,yangu masikio na macho
nikaanza kusikiliza kwa makini.
---------------------------------------------------------------------------------------------------
Hadi anafika mwaka wa
pili kimasomo chuoni mtakatifu Augustine Mwanza kitivo cha sheria Adam
aliitumia simu yake ya mkononi kwa ajili ya kupiga,kutuma ujumbe (sms) na
kupokea ni hayo tu na kwa upande wa pili alipenda sana kucheza michezo ya simu
(game) ya kwenye simu.
Alikuwa ni Hughorito
Hamada ama maarufu kama 'HUHA'.hakuwa tu rafiki yake adam bali pia alikuwa ni
mshirika wake wa chumba (room mate) na pia walisoma darasa moja la sheria pale
chuoni,ni huyu aliyemuingiza Adam katika ulimwengu ambao hatausahau kamwe,tabia
yake ya kupenda kuazima simu ya Adam aina ya Nokia Express music kwa dhumuni la
kuchat katika mtandao maarufu wa kijamii wa ‘facebook’ ndio ilimshawish Adam
naye kuanza kujiuliza kulikoni hasahasa alipokuwa anamwona Huha akicheka
mwenyewe kila anapokuwa anachat,"Mh! we jamaa yangu chizi kweli yaani unacheka
na watu usiowaona" Michael alimkebehi Huha alipokuwa anacheka na simu yake
punde tu baada ya kuanza kuchat
"Kwani we ukiwa unaota unaongea huwa kuna
watu mbele yako?" Huha alijibu mashambulizi na Adam akabaki kimya na taulo
yake kiunoni akaenda bafuni kuoga.
"Mwanangu nimekuunga na wewe namba yako
ya siri ni..,.." hata kabla Huha hajamaliza adam akamkatisha "Nini?
huo upumbavu wako sitafanya kamwe bro" ..."Hv kwan inakuwaje huo
upuuzi" Michael akajikuta anauliza baada ya kuwa amevaa nguo zake
"Hii kitu inaitwa FACEBOOK,yan adam ukijiunga wewe hutoki na utakuwa nayo
bize kweli" Adam alisikiliza kwa makin japo alijidai kufanya dharau
machon,Huha hakujali aliendelea kutoa somo had Adam akapata mwanga,"Mh.
Sidhan kama itanivutia bt i wil try". Alijisemea adam wakat anachukua simu
yake.
-----------------------------------------------------------------------
Tabia ya Adam ilikuwa imebadilika ghafla ni
Michael na facebook,facebook na yeye,iwe barabaran,club,lecture room,hostel
yani kasoro mskitini tu ndio Adam aliweza kuhfadh simu yake.Sio Huha wala
rafiki yake yeyote aliyejua nini zaid ya facebuk kimemuathiri adam wa
watu.Hakumuazima tena Huha simu,hakutaka mazoea na wasichana ni yeye na simu
yake tu!! "Adam mbona washkaji wanalalamika eti wanakuomba urafiki
facebook unachomoa? siku moja Huha aliamua kumuuliza Michael baada ya kuona
tabia yake imekuwa ya ajabu mno kupindukia."Sitaki that's all". Ndio
jibu fup alilopewa.kisha adam akajiondokea.Huha akabaki ameduwaa asijue la
kufanya,mara ghafla adam akarudi tena "Huha naomba ukamwambie Halima
simtaki,usiniulize kwa nini mwambie SIMTAKI!" Michael alimwambia Huha kana
kwamba alimfumania huyo Adija.
Mpenz msomaj Halima alikuwa binti matata pale
chuon kwa kipind kile,Michael ndo alipata fursa ya kuangukia penz lake,penz lao
chuo kizima walifahamu,gari ya Halima ilikuwa kama ya Adam..chumba cha Cha
Halima kilipambwa picha na kad za Adam lait na Michael angekuwa anakaa peke
yake basi hata yeye chumba chake kingekuwa had na nguo za ndan za Halima pamoja
na pedi bas tu alikuwa anakaa na Huha.
Huha alibak mdomo waz akijiuliza ni Adam au
kivuli chake kinaongea.Alikuwa Adam sio kivuli.....
Ubize aliokuwa nao mheshimiwa mbunge
ulimkosesha raha mkewe bi.Gaudensia Ogunde,hakuipata haki yake ndoa kwa
takribani mwezi mmoja sasa,mume alikuwa anachelewa kurudi na akirudi anakuwa
amechoka sana kutokana na majukumu mazito ya kiserikali,na ikitokea siku akathubutu
kujaribu kutoa huduma basi alikuwa hamridhish mkewe,taratibu mama akajaribu
kuzoea lakini kuna wakat uvumilivu ulikuwa unamshnda,nyumba nzima alikuwa
akiish yeye,mtoto wake wa kike na msaidiz wa kazi (House girl)."Mwanangu
ni siku ya tatu baba yako halali nyumbani,najisikia mpweke sana kulala
mwenyewe" bi.Gaudensia alimweleza mwanae kwa unyonge "Pole sana mamii
hata mi sipend hyo tabia ya baba,leo nakuja kulala na wewe mama" alijibu
yule binti mwenye miaka 17 akiwa ndio kwanza amemaliza kidato cha nne.Mama
hakujibu kitu badala yake alimkumbatia mwanae kwa sekunde kadhaa kisha
akamwachia huku machozi yakimlengalenga.
Majira ya saa tatu usiku mama na mwana walikuwa kitandan wote wakiwa na night
dress,kitanda kilikuwa kikubwa lakin umbali wao ulikuwa karibu mno,mapigo ya
moyo ya mama yalikuwa juu sana,jasho lilikuwa likimtoka mtoto kwa kasi air
condition iliyokuwa inapuliza haikuwa na maana tena mama na mwana walijikuta
katika hisia nzito sana za mahaba,sio mimi wala wewe tunaojua walipoanzia.
----------------------------------------------------
Reshmail Mtoto wa
mwisho na pekee wa kike kati ya watoto wanne wa mbunge wa jimbo la Kinondoni
Mheshimiwa Msuruli Haruna,hakupata kujua shida katika maisha yake na urembo
aliojaliwa pia hakuufaham kwa sababu hakuwepo wa kumwambia kuwa yeye ni
mrembo,kuta na fensi ya sen'gen'ge iliyozunguka mji wao haikumruhusu kutoka nje
hovyo hovyo,tofauti na siku ya kwenda msikitini Resh alilazimika kusubiri hadi
alipofikisha miaka kumi na nne alipojiunga na kidato cha kwanza katika shule ya
st.marry's international ndio alipata wasaa wa kujumuika na wananch wengne wa
Tanzania na nchi za jirani,elimu yote ya darasa la kwanza hadi la saba
aliipatia katika jumba la kifahari la baba yake.
Mazoea ya kuish maisha ya peke yake peke yake yalimtesa sana Resh kiasi kwamba
hadi anamaliza kidato cha nne aliweza kuwa karibu kiurafiki na wanafunzi
wachache na weng wao wakiwa wasichana tena watoto wa matajiri na vigogo
mbalimbali wa serikali.Kampani kubwa ya Reshmail alikuwa ni mama yake
mzazi,yalikuwa ni mazoea makubwa sana lakini yasiyoshangaza,mara nying walikuwa
wanatembea pamoja huku wameshkana mikono huku wakifurah sana.
Kidato cha tano na sita katika shule ya Arusha international school ndio kwa
mara wa kwanza ilimpeleka nje ya jiji la dar-es-salaam.
Resh alilia sana kutenganishwa na mama yake lakini hakuwa na jinsi ilimlazimu
kuondoka,mama alishindwa kujizuia alilia kwa uchungu ambao mumewe hakuutambua
maana yake. "Nitakuwa nakuja kukusalimia" bi Gaudensia alimnon'goneza
mwanae wakati akipanda gari la baba yake kuelekea airport."Usiache
mama".alijibu resh huku akimbusu mama yake shavuni.
Mwanzoni ilianza kama utani pale Adam
alipokubali ombi la Reshmail kuwa marafiki,walikuwa wakiulizana mambo ya
kawaida sana huku katika orodha ya marafiki wa Reshmail ni Adam peke yake
alikuwa mwanaume,"Mbona una marafiki wachache au ndo umejiunga
facebook?" adam alimuuliza reshmail katika moja ya 'chatings' zao "No
ni uamuzi 2 iam nt interested with boys i wonder why you?" "May be
iam someone special,who knows" alijibu Adam, "You might be"
alijibu reshmail."Yani hadi mchumba wako hujamweka kwenye orodha?"
"Sina huyo mchumba unayemdhania" "What? msichana mrembo kama
wewe,au hizi picha sio zako?" "Ni zangu kwani ukiwa mrembo lazima uwe
na mpenzi?"alisisitiza Resh kisha akaendelea "Naona we upo kwenye
uhusiano,hongera" aliandika Resh,ni wanaume wachache sana akiulizwa na
msichana mrembo kama ana mpenzi halafu akubali na hata kwa Adam ilikuwa
hivyo,"Mh! nimejiandikia tu,mi sina mtu nani wa kunipenda mimi?".
Alidanganya Adam,"What! hawakioni hcho kifua chako au na wewe hiyo sio
picha yako?"
"Ni ya kwangu,Reshmail una utani
wewe"
"Sina utani nimekipenda sana"
"Haya asante,kwako wewe sina la
kusema unavutia kila upande"
"Asante lakini we zaidi,Adam naingia
kuoga nisindikize basi"
"Wee,si umeniambia mnakaa wanne sa
wenzako watanielewaje?" alijibu Adam huku akiamini kwamba hayo yote
yanayotokea ni utani mtupu.
"Kwa hyo ningekuwa peke yangu
ungenisindikiza?" "Yeah? ningekusindikiza lakini ningefumba
macho" alitania Adam.
"Vp ninatisha sana au,yan hadi ufumbe
macho sawa tu" alilalamika Resh,"Natania mrembo lakin si unajua tena
nitajiumiza"
"Ok! tuachane na hayo,simu yako inauwezo
wa kufungua e-mail?"
"Inafungua tena sasa hivi nilikuwa
ninasoma emails" alijibu adam.
"Ndio hii Adamboy@Yahoo.com?"
"Yap ndio hyo" "Fungua baada ya dakika tano uone zawadi
yako"
Jasho jembamba huku mikono ikitetemeka,macho
yakiwa yamemtoka Adam hakuamin anachokiona kwenye simu yake.
-----------------------------------------------
Mazoea ya Reshmail na mama yake kujigeuza mtu
na mpenzi wake yaliwaathiri sana wawili hawa,mara kwa mara Bi.Gaudensia
alifanya safari za ghafla kwenda Arusha kufaidi penzi la jinsia moja kutoka kwa
mwanae mpendwa,raha alizozipata hakuwa na muda wa kumfikiria mumewe tena,tabia
hii ilimuathri sana Reshmail pale shulen,licha ya urembo wake hakuwa na
uhusiano wa kimapenzi na mwanaume yeyote pale shulen bila kujalisha uwezo wao
kifedha wala sura na utanashati wao,aliwaona hawana maana kwake zaid ya mama
maskin Resh hakujua tamtam ya penzi la wanaume.
Alikuwa ni Eveline,binti aliyekuwa anaish
chumba kimoja na Resh,akiwa ni mzaliwa wa hapohapo Arusha anayezijua kona zote
za Arusha,pombe,club na ngono ndio walikuwa marafiki zake wakubwa,alikuwa
mchesh na mzuri wa sura lakin kubwa na jema zaid alikuwa mwelevu sana darasani
katika mchipuo wa "H.G.E" pamoja na reshmail,ni jambo hilo
lililowaweka wawil hawa karibu.Mshipa wa aibu haukuwepo kichwani mwa Eveline,na
kama ulikuwemo basi haukuwa unafanya kazi vizuri,picha alizozipenda ni za uchi
na movie za ngono ndio alizokuwa anaangalia tena kwa anapandisha sauti hadi
vyumba vingne wanasikia.Ni huyu Eveline aliyemwingiza Resh katika maswali ya
kwa nini,na inakuwaje "Mbona nikifanya na mama silii kama hao? alijiuliza
Reshmail akiwa ndan ya kitanda chake huku pemben Eveline akiwa bize na laptop
yake akiangalia filamu ya ngono "Ponographics"
......."Nitamuuliza Eve siku moja lakin nitaanzaje?" alijiuliza
Mara zote walizokuwa wakipeana burudani
kitandani au sakafuni Mama yake alikuwa ndiye mwalimu wa kila kitu,yeye ndio
alijua wapi amguse,wapi amtekenye ili mradi kuleta raha na wote
kuridhika.Lakini safari yake ya mara ya tano kwenda Arusha kwa mpenzi wake huyo
haramu ndipo alipokutana na mshangao.Reshmail yuleyule aliyekuwa zuzu kitandani
akihudumiwa kila kitu na mama yake ili aridhike alikuwa moto wa kuotea
mbali.Alimgalagaza mama yake ipasavyo kwa ku2mia vidole vya mikono yake pamoja
na ulimi wake kutambaa kila kona ya sehemu husika .Mama reshmail (Bi.Gaudensia)
alijikuta akiongea lugha ambazo hazipo katika ulimwengu huu.Hoteli ya Tanzanite
chumba namba 18 kiligeuka kama pepo kwa wawili hawa,mama alikuwa analia sana
machozi ya furaha na mbaya na ya kuchekesha eti akasema "Darling UTANIOA
eeh!" jaman raha zikizidi sijui kilimfurahisha nini mama huyu kwa
mwanae.Kulipokucha Bi.Gaude alimrudisha mwanae shuleni kama alivyokuwa
amemwombea ruhusa."Mama huyu ni rafiki yangu anaitwa Eveline,Eve huyu ni
mama yangu mpenzi" Reshmail aliwatambulisha baada ya kumkuta Eveline pale
ofisini."Shkamoo mama" "Marahaba" alijibu mama bila
kumwangalia usoni Eveline ambaye hakujali hilo sana "Punguza wivu
sweet" Resh alimnon'goneza mama yake,ambae alitabasamu "Nakupenda mwanangu"
"Nakupenda mama" waliagana mama akaondoka kurudi kwa gogo lake
(Mumewe) huko dar.
---------------------------------------------------
"Ukitaka kuujua utamu wa ngoma ingia
ucheze" ndio jibu alilopewa Resh baada ya siku moja kumuuliza eti
anafaidika nini kuangalia filamu za ngono,mwanzoni alikuwa akiangalia kwa aibu
san lakini baada ya kufanikiwa kuzihamishia kwenye "Laptop" yake
mambo yakawa ya kawaida japo kwa kujificha,mara nying alijifunika shuka na
kuweka earphone masikion kisha burudani.Ni mchezo huohuo mchafu Resh aliuiga na
kwenda kujaribisha kwa 'mpenzi mama'."Hivi Eveline kuna raha kufanya au
kuangalia peke yake inatosha?" "Haha haloooooo! unalo shosti,wenzio
wakata viuno we wafurahia miguno looh!" Vidole vikiwa juu kama muimba
taarabu Eve alimchambua Resh,"Mh! shoga si unifunze kuliko
kunichambua?" alijitetea resh kwa saut ya chini,"Ulisema huna bwana
weye sasa kulikoni ya nini haya tuachie sie wamama wa shughuli" "Eve
we ni rafiki yangu ngoja nikwambie ukweli.....mimi nampenda mtu ambaye sijui
kama ananipenda au tutaendana"
"Vipi hujawah kumwona au?"
"Nimemwona kwenye picha"
"He! una makubwa we mrembo au ndo yule
kwenye kompyuta yako?"
"Haswaa ndio yeye"
"Hata kama hujamuona yule pale dume la
ukweli,kile kifua usimlete kwangu nitakuibia," alitania Eve.kisha
akaendelea "Najua hujui jinsi gani utampata niachie hyo kazi mimi ndan ya
wiki moja nakukabidh mali yako." "Asante evely asante sana"
alishukuru
* * * *
Ilikuwa ni picha ya binti mrembo sana akiwa
amejifunga taulo kwa chini huku chuchu zikiwa nje,"Ndio natoka kuoga,vp
nimetakata?" iliambatana na ujumbe ule.Adamu alibaki mdomo wazi,mh!! hivi
inawezekana akawa Reshmail dah! alishangaa Adam.Akiwa bado mdomo wazi email
nyingne iliingia ilikuwa picha tena,safari hii ilionyesha sehemu yote ya nyuma
"NIPAKE MAFUTA" ndio ujumbe uliobeba picha hyo.Bila kujua muda gani
na kwa misingi ipi Adam alikuta pensi laini ikiwa imembana,kuja kugundua chanzo
ni sehemu flani kwenye mwili
wake ilikuwa imeongezeka ukubwa (Ha ha ha ha
wanaume dhaifu sana.
Majukumu ya hapa na pale yalikuwa yamembana
sana Bi.Gaudensia ambaye ni mama yake na Reshmail,pia uwepo wa mumewe katika
himaya yake ilimnyima kabisa raha mama huyu na alikuwa anakosa nafasi ya kwenda
Arusha mara kwa mara kufurah na mwanaye jambo ambalo lilimtesa kwa takribani
mwezi mmoja na nusu.Vipindi vya bunge vilipoanza tena ndio hapo nafasi
ilipatikana tena,kwa muda wote ambao alikuwa jijin dar-es-salaam Bi.Gaude
alikuwa akiwasiliana na mwanae karibia kila siku kwa njia ya simu,alijua ni
jinsi gan hata mwanae huyo alivyo'm-mis' hvyo aliamua kumfanyia 'surprise' ya
kwenda huko Arusha shuleni bila kumwambia ili kuinogesha furaha yao ambayo
ilikuwa inakamilika kitandan."Baba Resh mie kesho naenda kumsabah
mwanetu,lakin hata simwambii nataka ashtukie tu,mama huyo"
"Atashangaa kweli,msalimie sana mwambie
nitakuja kumsalimia bunge likimalizika" "Haya,zimefika"
-------------------------------------------------------------------------------
Penzi la ku-chat katika mtandao wa facebook
lilikuwa limemchanganya sana Reshmail wa watu,Adam hakuwa nyuma kumpa maneno
matamu ya hapa na pale ambayo kamwe alikuwa hajawah kuyasikia masikion
mwake,Eve mwenyewe alimshangaa huyu shoga yake lakin hakuwa nyuma kumpiga tafu
katika mpango mzima wa kumtia Adam majaribuni ndio maana alimshawish Resh kupga
picha mbaya ambazo mwanaume yeyote akiziangalia lazima ajiulize mara mbilimbili
kuhusu urembo asilia wa binti yule.
"Mi nipo peke yangu siku hizi rum-mate
wangu ameenda kwao babake anaumwa" "Don't tell me kuwa unalala
mwenyewe"
"Nitafanyaje sasa na wewe upo
mbali?"
"ooh! my ghosh! assume nipo hapo"
"Aah,nitajiumiza bure tu mpenzi
wangu"
"Anarudi lini kwani?"
"Mh! amesema atatumia kama wiki mbili
hivi,njoo basi unipe 'kampan' kiaina"
Yalikuwa mazungumzo kwa njia ya simu kati ya
Adam na Reshmail yaliyokatishwa na na mlio wa 'low battery' katika simu ya
Reshmail "Baby boy tutaongea kesho,pole sana na ninakupenda sana"
alimaliza Resh na simu ikawa imezima.
"Eveline nataka kwenda Mwanza"
asubuh ya siku iliyofuata Resh alimwambia Eve.
"He! makubwa haya,imekuwaje kwan
shoga" aliduwaa.
"Mi sijui lakin nataka kwenda tu"
alisema Reshmail "Haya lini wataka kwenda?"
"Hata kesho mi naenda tu" "Mh!
sikuwez haya jiandae kutoroka coz ruhusa hapa kupata sahau" "Vyovyote
poa ninachotaka ni kuondoka na kwenda Mwanza that's all" alijibu kijasiri
Resh hali iliyomduwaza eveline.
----------------------------------------------------------------
"Reshmail hayupo? mbona jana alikuwa hapa
ofisin?" mwalimu wa zamu alikuwa anamuuliza mwanafunzi aliyeagizwa kumuita
Reshmail baada ya mama yake kuwa amefika,"Hata mi sijui mwalimu"
"Hapana sio jambo la kawaida reshmail
kutokuwa mazingira ya shule tena jumatatu! hebu mwambie time-keeper agonge
kengere mara moja" aliamrisha mwalimu.
----------------------------------------------------
Hakuwa hata na chembe ya utani Reshmail wa
watu,majira ya saa moja asubuhi tayari alikuwa kwenye gari la KIMOTCO
ninalotoka Arusha kwenda Musoma kwa kupitia Mugumu Serengeti,kitu kinachoitwa
hofu moyoni hakikuwepo hata kwa mbali,ndani ya kipochi chake kidogo alikuwa na
pesa taslimu za kitanzania shiling laki mbili zikisindikizwa na kadi ya viza ya
CRDB iliyokuwa na uwezo wa kutoa shiling laki tano kwa siku mara nne yaani milioni
mbili zilikuwa zimehfadhiwa katika acount yake ya akiba.Mamaa wa shughuli
(Eveline) alikuwa pembeni ya Reshmail,hofu kwake haikuwepo wala hakuiwaza
tayari alikuwa mzoefu wa mambo hayo."Eveline yani akili ndo inakuja sasa
hivi eti kwa nini tusingepanda ndege dah! gari linaenda taratibu hilo
jaman" alilalama Reshmail kwa wananch wa kawaida waliomsikia walidhani ni
mashauzi na majigambo ya watoto wa kike
"Mh? shoga ulivyokuwa na hamu ungekumbuka
hayo,tutafika weye acha papara"
Gari lilizidi kuchanja mbuga za ngorongoro kwa
kasi ya kawaida hadi majira ya saa saba tairi chakavu za gari hili zilikuwa
tayari kwenye mbuga za Serengeti,Resh alikuwa macho anatazama safari
inavyokwenda huku akihesabu masaa yanavyokatika kwa kasi huku mwisho wa safari
ukiwa haufiki.Eve yeye alikuwa ameuchapa usingzi huku akiwa amejifunika uso
wake kwa kofia yake nyeusi ambayo vumbi ilikuwa imeibadili rangi yake na kuwa
ya ugoro.(Brown).
"Eve Eve Eve,amka uone wewe" Resh
alikuwa anamwamsha kwa fujo."Angalia hii sms imeingia sasa hv" "Resh
mazako kaja unatafutwa uko wap?" jasho jembamba likaanza kumtoka Resh
lakin Eve hakushtuka sana.Walikuwa wametumiwa ujumbe mfupi na mmoja wa
viranja."Eve tumeisha tumeisha"
----------------------------------------------------------------------
Ulikuwa mshikemshke wa ghafla pale shuleni
mwalimu aliamuru kila mmoja aje mstarini hata kama ni mgonjwa,viranja walitii
amri na kuita wanafunzi wote kwa haraka hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyebaki
ndani ya bweni.
Wakiwa hawajui nini kinachoendelea mwalimu wa
zamu aliyeitwa Mwl.Chipeta alikuwa mbele ya wanafunzi waliokuwa kimya
kumsikiliza yeye.”Kabla sijatoa tangazo hili,ni nani anatambua mwanafunzi
ambaye hayupo eneo hili? (Kimya)
"Nani anaumwa na amepewa ruhusa?"
(Kimya)
"Kwa hyo wote mpo?" (Ndiooo)
"Haya mchepuo wa H.G.E wote pita
mbele" aliamuru mwalimu Chipeta na kwa haraka wakaanza kujongea
mbele."Mamaaaaa," ghafla kelele ilisikika kuna mwanafunzi aliyekuwa
mgonjwa alikuwa ameanguka chini kwa sababu ya kizunguzungu.Ustaarabu ukatoweka
pale ghafla kila mwanafunzi akawa anasema lake,mara hivi mara vile. Hata
mwalimu Chipeta alitimua mbio kuelekea kwenye tukio.
Ni wakat huohuo Joyce ambaye alikuwa kiranja
alipata mwanya wa kutuma ujumbe kwa Reshmail kumpa taarifa.
-------------------------------------------------------------------
Roho ilikuwa inamdunda Reshmail kwa kasi
sana,aliamin kila kitu kitakuwa wazi na atafukuzwa shule,"Eve
watanielewaje wazazi mie mh! nimerokoroga" alijisemea Reshmail.
"Upo na steringi lazima tushinde haka
kavita kadogo" Eve alimpa moyo wa ujasiri Resh,"Naomba hiyo simu si
ina salio kidogo"
"Imo elfu tatu"Alijibu huku akimpa
simu Eve.
"Sihitaji zote hizo natumia shiling 60 tu
hapa"Alijibu kwa jeuri Eve huku akionekana kujiamini zaidi.
"Sasa hyo 60 itafanya nini shogangu au
umesema elfu sitini?"Alitania Resh na wote wakajikuta wanacheka.
"Dakika tano nyingi majibu mazuri
yatakuja,chukua simu yako ikiingia meseji uisome mi nalala bibie tuliza roho
yako hii sio movie ya kihindi eti stering anauwawa,hili picha la kichina
stering anachomwa kisu bado anapona" alimaliza Eve na kushusha kofia yake
ikafunika macho.
Ni kama alivyosema dakika tano zilikuwa nyingi
sana ujumbe kujibiwa
"Na ufanye kweli mi narekebisha mambo
nyie tanueni kwa raha zenu na pia kuhusu yule wa H.G.L vipi?" ulisomeka
ujumbe."Mungu wangu amakweli Eve steringi jamani yaani kirahisi hvyo"
alijisemea Resh kwa sauti ya chini akidhani Eve amelala tayari "Futa sms
ya huyo mjnga nitamalizana nae" kwa saut ya kivivu Eve alimwambia Resh.
-----------------------------------------------------------
Ndege ya Precion Air ilikuwa inaondoka kutoka
Musoma kwenda Dar-es-salaam kupitia Mwanza majira ya saa kumi na moja wakati
basi la KIMOTCO lilifika saa kumi na nusu jioni,Resh aliona akipanda gari
anaweza kuchelewa kwa Adam Mwanza japo hata umbali wa Musoma kwenda Mwanza
hakuufahamu."Resh ndege ya wapi tunapata sasa hv jaman" Eve
alimuuliza Resh wakiwa ndani ya 'Teksi’ kutokea stendi kuu ya Musoma maeneo ya
Bweri."Tunajaribu steringi wangu"
"Haya!! utamu na uchungu wa mapenzi
mwachie aliyeyabeba" alitoa fumbo Eveline.
"Dereva dereva zuia kidogo
tafadhali" ghafla Resh alimwomba dreva naye bila hiana akazikanyaga breki
bila kuuliza kulikoni. Mbio mbio Resh akashuka akaanza kutimua mbio kurudi
nyuma huku akiwa peku viatu ameacha garini Eve,Dereva na wananchi wengine
wakabaki kumshangaa.
Mwalimu Chipeta aliongoza zoezi zima la
kumshughulikia mwanafunzi aliyeanguka pale mstarini,shule ya Arusha international
ilisifika sana kwa kujali afya za wanafunzi hivyo tukio lile lilisababisha
Mwalimu Chipeta kumsahau kabisa Bi.Gaudencia mama yake Reshmail na kwenda
kushughulika ipasavyo kwenye lile tukio,aliyekuwa ameanguka alikuwa Naomi
Holela mwanafunzi aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua na pale kilikuwa
kimembana hasa kutokana na baridi iliyokuwepo nje. Gari ya shule ilifika haraka
Mwalimu Chipeta na viranja wawili pamoja na 'matron' walimsindikiza Naomi
hospitali. Akiwa ndani gari Mwalimu Chipeta alisikia simu yake ikitoa mlio wa
kupokea ujumbe mwanzoni alipuuzia kutokana na ubize uliokuwa ukimkabili lakini
punde alitoa simu yake na kufungua ujumbe ulioingia
"Niaje ticha mi Wa ukweli nipo na Resh
mbali kimtindo kama vipi rekebisha mambo huko mi nikija nakuletea geto yule
Amina wa H.K.L,niandalie tu mapene yangu" uso wake ulisahau matatizo yote
yaliyokuwa mbele yake,ni muda mrefu sasa tangu Mwalimu Chipeta muhitimu wa
shahada ya elimu ya fasihi andishi katika chuo kikuu cha Dodoma alikuwa
amemfukuzia binti mrembo wa kawaida tu Amina bila mafanikio tegemeo lake
alikuwa ni Eve au Wa ukweli kama walivyomzoea,bila kupoteza muda Chipeta
alifungua sehemu ya ku'forwad' meseji na akaituma kwa Mwalimu.Madege ambaye
wote lao lilikuwa moja,alikuwa ni mwalimu Madege aliyeijibu ule ujumbe na
kuulizia kuhusu yeye na mpango wa kumpata binti wa H.G.L.
"Samahani wewe ndio mama yake na Reshmail
"Mwalimu Madege aliuliza baada ya Bi. Gaude kuingia katika ofisi ya makamu
mwalimu wa zamu .
"Ndio ni mimi baba"
"Kwanza samahan sana kwa usumbufu
uliojitokeza"
"Usijali na mimi niwape pole
kwa matatizo yaliyojitokeza hapa"
"Tunashukuru ndio mambo ya shule
haya,eeh! mama nimepokea ujumbe sasa hivi kwamba mwanao yupo katika mbuga za
Serengeti ambapo wanafunzi watano waliofanya vizuri walipelekwa kufanya utalii
wa siku tano" alidanganya mwalimu Madege.
"Jaman huyu mtoto mbona hakuniambia?...
baba yake atafurahi sana akisikia maendeleo ya mwanae"mama Resh alijieleza
kwa furaha iliyozidi wasiwasi aliokuwa nao.
"Tuliwashtukiza hawakuwa na taarifa hata
wao wameshangaa mno" aliendelea kupanga maneno huku akichorachora mezani
kwa kutumia karamu isiyokuwa na wino.
Moyo wa mama Reshmail uliridhika japo mwili
ulikuwa na kinyongo kwa kukosa haki yake. Ilimbidi siku hiyo hiyo afunge safari
kurudi jijini Dar na zawadi alizokuwa amemletea mwanae zikiwa mikononi mwake.
----------------------------------------------------------
A.T.M ya N.B.C aliyoiona maeneo ya Nyasho
ilimkumbusha kuwa kadi yake ni 'VISA' inafanya kazi mashine ya A.T.M ya benki
yoyote bila kujali macho ya watu alitimua mbio pekupeku hadi kwenye mashine
ambapo kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni na mtandao ulikuwepo "You can
withdraw up to 1000000 with your A.T.M card daily N.B.C WE CARE"
kijitangazo kwenye kioo cha mashne kiliibua tabasamu la Reshmail,na bila ajizi
akabonyeza chaguo la kutoa laki tano kwa mikupuo miwili na kutimiza kiasi cha
milioni moja, kisha kwa mwendo wa mbio kama alivyoingia akatoka akisindikizwa
na miluzi ya wauza mitumba wa Nyasho ambayo kwake haikuwa na madhara hata
chembe
"Samahani safari yenu imeahirishwa
tafadhali hadi kesho asubuhi!" sauti nyororo ya mwanadada wa mapokezi
aliyehusika na masuala ya Booking aliwaeleza mwanaume mmoja aliyekuwa na mpenzi
wake wakitegemea kusafiri muda mfupi ujao kwenda Mwanza.
Sura zao zilizokuwa na furaha zililegea na kuwa kama watakavyokuwa pindi
wakipata wajukuu,"Haiwezekani huu ni upumbavu tena ujinga ujinga
ujinga,yani safari yangu inahairishwa ghafla kama vile safari za
baiskeli,hapana sipo tayari nas...."
"shhhhh!!" kwa ishara ya kidole
kimoja kuziba mdomo alinyamazishwa yule baba aliyetaka kuugeuza ukumbi ule
uwanja wa mapambano na matusi. Kwa ishara nyingine yule dada akamwita akasogea
pale alipo akamnon'goneza "Unawaona wale wasichana wawili,mmoja kimada wa
mtoto wa raisi mwingne mtoto wa kamanda wa jeshi ni simu kutoka ikulu,kwa
usalama wako acha kelele" alimwambia huku akimwelekezea walipo Resh na
Eve. Bila kuhoji huku uoga ukimtawala hadhi yake ikashuka haraka haraka
akamvuta mkewe wakaondoka wakawapisha kwa mbali Resh na Eve kama vile wanatema
cheche za moto.
------------------------------------------------------------------------------
Ni kweli nafasi zilikuwa zimejaa lakini pesa iliongea nafasi ya mtu mwingine
wakapewa wao tena harakaharaka,huku mtendaji wa jambo hilo akiweka shilingi
laki mbili na nusu kibindoni. Huku Resh na Eve wakipata nafasi katika ndege ya
Precision Air kiulaini,kwa mara ya kwanza Eve anapanda ndege "Mh! ushoga
nao raha wakati mwingine” alijisemea wakati muhudumu wa ndani ya ndege akitoa
maelekezo madogomadogo.
Ilikuwa kama safari ya kutoka Kimara Dar kwenda Mbagala,tayari walikuwa jiji la
Mwanza
"Eve rushwa tamu wewe,naamini haitaisha
ona sasa tupo Mwanza tayari" Resh alimwambia Eve wakati wanasafisha macho
yao wajue nini cha kufanya baada ya kushuka kutoka kwenye ndege.
"Hoteli yenu ni nzuri?" Eve alimuuliza muhusika aliyekuwa ndani ya
kigari kidogo kilichoandikwa Millenium Hotels kilichokuwa hapo kwa lengo la
kutafuta wateja wanaotua na ndege uwanjani hapo,"Ni nzuri sana hautajuta
kuwa pale.”
"Mh! haya,Resh twende giza
linaingia" Eve alimwita Resh wakajitoma ndani ya gari na safari
ikaanza.
"Darling umetoka kwenye michezo tayari pole mpenzi" ulikuwa ujumbe
mfupi kutoka kwa Adam kuja kwa Resh,tabasamu pana likameza mdomo wake looh!
lilikuwa tabasamu lililoelezea furaha ya moyo.
Adam alituma ujumbe huo akijua Resh yupo shuleni tena ilikuwa siku ya michezo
ambayo Resh alipenda kushiriki hasahasa mpira wa kikapu.
"Mamaaaaa!!"Resh alipiga kelele ghafla gari ikayumba huku na
huko,dereva akajaribu kwa uwezo wake wote kuirudisha barabarani
"Paaaa!!" mlio mkubwa ukasikika.
--------------------------------------------------------------------------------------
Adam alipokea ujumbe kutoka kwa Reshmail akiwa
maeneo ya kijiweni barabara ya lami kuelekea chuo kikuu cha mtakatifu
Augustino,kupitia shule ya wasichana ya Ngaza.Adam alikuwa pamoja na rafiki
yake (Huha) katika pikipiki ya rafiki yao aliyekuwa amewaazimisha
wazungukiezungukie maeneo.
"Huha hebu endesha twende hapo Nyegezi
kona kuna mtu nataka kuonana naye mara moja" Adam alimwomba Huha.
"Tayari Halima ametuma meseji mwambie hatuna mafuta atufate na gari yake
bwana" Alitania Huha huku akianza kuiondoa pikipiki taratibu
"Ungejua hata usingesema wewe twende ukajionee maajabu ya
mwaka" alijibu Adamu huku pikipiki ikizidi kushika kasi.
Ndani ya dakika tano tayari walikuwa Nyegezi kona ambapo Huha alipaki pembezoni
kidogo na barabara iendayo stendi kuu ya Nyegezi jijini Mwanza,Adam alielekea
dukani kununua vocha,na Huha akasogea pembeni kidogo aweze kuvuta sigara yake.
------------------------------------------------------------------
Dereva akiwa mwingi wa mawazo yake binafsi yasiyomuhusu Reshmail wala Eve na
hata kama yangekuwa yanawahusu ule haukuwa muda muafaka wa kuwaambia.Macho ya
Reshmail yalikuwa yamekutana na bango kubwa lililoandikwa "KARIBU CHUO
KIKUU CHA MTAKATIFU AUGUSTINO" kwa hamu kubwa aliyokuwa nayo ya kumwona
Adam ambaye alikuwa pia mwanafunzi ndani ya chuo hicho ndio sababu kuu ya
kujikuta akipiga kelele kwa nguvu hali iliyomshtua dereva kutoka katika mawazo
mazito na kujikuta akiyumbisha gari huku na huko hadi ilipokutana na pikipiki
iliyokuwa imepakiwa pembezoni mwa barabara na kuirusha umbali ambao si wa kutisha
sana,iligeuka vurumai madereva wa teksi na bodaboda za pikipiki walikuwa wakali
sana hawakutaka kusikia la mtu,wengine hasira za kukosa abiria tangu waingie
kijiweni asubuhi walizihamishia katika tukio hilo. Usingekuwa upole wa yule
dereva basi mawe waliyobeba wananchi yangeigeuza ile gari kuwa mkweche. Eveline
alitelemka garini kwenda kumsaidia dereva kujitetea lakini Reshmail uoga
ulimtawala akawa amejibana kwenye viti vya nyuma vya ile gari huku akitetemeka.
"Mh! Adam hawezi kukosa mwenyeji maeneo haya ngoja nijaribu kumpigia,ah!
hii safari imetawaliwa na mikosi dah!" aliwaza Resh huku akichukua simu
yake kutoka katika kipochi chake.
Lakini kelele zilizokuwa pale aliamini hawezi
kusikilizana vizuri na upande wa pili,taratibu huku akitetemeka alifungua
mlango akashuka na kuanza kutembea kuelekea pahali ambapo kidogo pametulia.
Zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wenye hasira eneo lile wakageuza vichwa vyao
kuangalia kazi ya Mungu ilivyotendeka vyema katika mwili wa Reshmail,badala ya
kumpigia kelele dereva,miluzi mikali ikiongozwa na dereva mkongwe wa teksi eneo
lile ndugu Sanya Bonda ikahamia kwa Reshmail,Resh akajifanya kama hasikii vile
"Ilikuwa haki ya dereva kupotea njia jamani" Bonda alisema kwa sauti
ya juu na kugeuza hasira za watu kuwa vicheko. Resh taratibu akaufikia mti
mdogo mbali na eneo la tukio akabonyeza namba za Adam. Simu iliita muda mrefu
bila kupokelewa. Alipopiga mara ya pili simu ilipokelewa."Helow Resh
subiri nisogee pembeni nakupigia kuna tatizo limenipata" alijibiwa na Adam
katika simu.
"Hata mi....." kabla hajamalizia kauli yake Reshmail simu ilikatwa
akiwa bado anaduwaa kama dakika mbili pembeni yake alizengea kijana mmoja
ambaye Resh hakutaka hata kumwangalia machoni,alijua ni walewale waliokuwa
wakipiga miluzi na kumwita majina waliyotaka. Resh taratibu akajisogeza
pemben."Vipi dada mbona wanikimbia au mi nanuka halafu we mrembo haya basi
umebarikiwa sana najua unataka kusifiwa" aliongea yule kijana lakini Resh
hakujibu.Simu yake ya mkononi iliyokuwa katika mfumo wa kimya(Silence mode)
ilikuwa inatoa mwanga kuashiria aidha kuna ujumbe umeingia au kuna simu
inaingia,lakini kwa jinsi alivyoandamwa na yule kaka kwa maneno hata hakuweza
kugundua.
Baada ya dakika kadhaa akaondoka yule kaka ndipo kuangalia simu akagundua
ilikuwa imeita mpaka imekata na hakuwa mwingine bali ni Adam alikuwa
amepiga,harakaharaka akapiga tena. Ulikuwa mshangao wa hali ya juu sana
Reshmail hakuamini alipomwona yule kijana aliyekuwa ametokea pale dakika chache
zilizopita kuelekea kwenye zile vurugu ndio anapokea simu."Resh mbona
nimekupigia hupokei mamaa" alimshuhudia yule kaka akiongea kwenye simu
huku akirejea lile eneo kukwepa kelele,kama ilivyo kwa mtu aliyenaswa na umeme
Reshmail alikuwa ametulia tuli na simu sikioni huku yule kaka akizidi kulikaribia
eneo lile “Reshmail mbona huongei!!” aliendelea kuuliza bila kupata
majibu."Adam" alijitutumua Resh na kutamka akiwa jirani naye
kabisa,bila kujua yule kijana akaangusha simu yake hakuamini msichana aliyetoka
kuongea nae dakika kadhaa ndio Reshmail wa Arusha.
----------------------------------------------------------------------------------
Vurumai lilisawazishwa haraka sana Adam na Huha ndio waliokuwa wamiliki wa ile
pikipiki iliyogongwa na gari waliyokuwemo akina Reshmail."Jamani huyu hapa
ni dada yangu,ndio alikuwa amenipigia simu tuonane hapa naomba haya mtuachie
sisi" Adam aliuambia umati ule ambao hasira zao zilikuwa zimeanza kupoa na
haraka walimwelewa wakaacha kumzonga dereva.Reshmail bila kupoteza muda
akamwongoza Adam wakaingia garini akampa pesa taslimu shilingi laki tatu kwa
ajiri ya matengenezo ya ile pikipiki naye Adam akamkabidhi Huha kisha
akajumuika na Eve pamoja na Reshmail katika gari,huku Reshmail akiwaacha watu
hoi kwa uzuri wake wa asilia ambao hata Adam alikuwa amechachawa nao na
kukubaliana na ukweli kwamba picha zilizotumwa zilikuwa za Resh kweli.
---------------------------------------------------------------------------------
Bi Gaudensia alifika Dar-es-salaam majira ya saa tatu usiku,bado alikuwa
hajaridhika kumaliza siku yake bila kuongea na mwanae,hivyo punde tu baada ya
kuingia chumbani mwake aliamua kujaribu kupiga namba za simu za Reshmail ambazo
zilikuwa hazipatikani siku nzima. Furaha aliyoipata ilikuwa haisimuliki,pale simu
ilipoita upande wa pili"Mh! kalala nini huyu?" alijiuliza simu
ilivyoita kwa muda mrefu bila kupokelewa,lakini mara ikapokelewa
"Helow! samahani Reshmail
amelala" sauti ya kiume ilijibu baada ya kupokea kisha simu ikakatwa na
kuzimwa. Mama Resh hakuamini kuwa amesikia sauti ya kiume katika simu ya mwanae
alidhani amekosea namba lakini alipohakikisha zilikuwa zenyewe,wivu mkali
ukamshika,akajaribu kupiga mara nyingi lakini bado hali ilikuwa ileile simu
ilikuwa imezimwa usingizi ulipaa,alitokwa na jasho,hisia mbaya zikamvuruga na
kufanya kichwa chake kiume sana,mama huyu alikuwa amejisahau kabisa kuwa
Reshmail ni mwanae wa kumzaa, alizurura kama mtu anayetafuta kitu ambacho
amesahau alipokiweka pale chumbani,alitamani kupiga kelele lakini aliamini
hazitasaidia kitu.
---------------------------------------------------------------------
Reshmail akiwa usingizini Adam pembeni yake,yeye(Resh) alikuwa hoi kwa uchovu
wa safari na misukosuko yote waliyopitia,na alipomaliza kuoga tu na kupata
chakula alisinzia,hata simu yake ilipoita hakuisikia hata kidogo na hata
angeisikia asingeweza kunyanyuka kupokea "Resh ni kipetito anapiga"
Adam alimuuliza Resh aliyekuwa hoi kitandani."Ah! ni rafiki yangu mwambie
nimelala" alijibu kwa taabu akiwa hata hajui anachokiongea. Naye Adam bila
kugundua kwamba Resh hajui anachokisema na ile namba ni ya mama yake Resh
alipokea na kuzungumza
Kitendo cha Adam kumkuta Reshmail akiwa bado
ni bikra kilimzuzua sana,mapenzi yake kwa Halima yalipungua sana na kuisha
kabisa hatimaye. Siku tatu mfululizo walizotumia pale Millenium Hotel zilitosha
kuvunjilia mbali penzi la Adam na Halima na kujenga penzi imara kati ya Adam na
Reshmail.
"Mwezi wa pili uje ujitambulishe nyumbani Adam yaani siwezi kusubiri kwa
kweli nakupenda Adam wewe ni mwanaume wangu wa kwanza na ninakuahidi
nitajitunza kwa ajili yako" Reshmail alikuwa anamsisitiza Adam siku
alipokuwa amewasindikiza uwanja wa ndege tayari kwa wawili hawa kurejea Arusha
shuleni.
"Mama anapiga! Eve" Resh alimwambia Eve pale simu yake
ilivyoita."He! usiniambie huyo ndio mama,sasa mbona ulikubali niongee nae
usiku ule? aliduwaa Adam.
"Eti! uliongea nae? Yesu wangu!"
alishtuka Resh lakini Eve akamshauri azime simu kwanza mengineyo watajua mbele
kwa mbele naye Resh akatii amri hiyo haraka akaizima simu bila kupokea Resh kwa
kiasi kukuwa alikuwa amemzoea na kumwamini Eve.
Adam,Resh,na Eve waliagana kama watu waliofahamia na kukaa pamoja siku nyingi
sana,Resh alimkumbatia Resh alimkumbatia Adam kwa muda mrefu hadi Eve alipowatenganisha
na kuambiana Kwaheri.
---------------------------------------------------------------------
Ilikuwa imebaki miezi minne wafanye mtihani wa kumaliza kidato cha tano,Resh
akiwa amekolea katika penzi la Adam na kusahau kuhusu
Mama yake ambaye alikuwa amezuiwa na mwanaye
huyo kwenda pale shuleni kumsalimia kwa madai kwamba yeye(Reshmail) anataka
ajikite zaidi katika masomo. Reshmail kwa maksudi akabadilisha namba yake ya
simu ili mama yake asiweze kumpata mara kwa mara badala yake muda mwingi akawa
anawasiliana na Adam.
Mwezi wa pili ilikuwa ni likizo ya mwezi mzima kwa wanafunzi wa kidato cha tano
na cha sita na pia wakati huohuo wanafunzi wa chuo kikuu cha mtakatifu
Augustino huwa katika mapumziko mafupi baada ya kumaliza muhula(Semister) ya
kwanza. Kwa Reshmail ulikuwa wakati muafaka wa kumtambulisha Adam kwa wazazi
wake jambo ambalo aliamini lingesaidia kupunguza makali ya mama yake. Tangu
akiwa mtoto kamwe hakuwahi kuwakwaza wazazi wake kwa sababu ya wanaume hata
siku moja hivyo alitegemea hawatampinga.
Ilikuwa siku ya furaha kubwa sana kwa Bi. Gaudencia na familia yote kwa ujumla
kumwona tena Reshmail nyumbani baada ya miezi mingi tena akiwa mwingi wa
furaha. Lakini tofauti na mama yake alivyofikiria kwamba mwanae huyo anafurahia
kurudi katika ulimwengu wao wa mapenzi haramu yeye(Reshmail) alikuwa anafuraha
ya kumtambulisha Adam ndani ya siku chache.
Kwa kujua wazi kabisa mama yake atachukizwa na maamuzi yake hayo,Reshmail
aliamua kulifikisha hilo mbele ya Mzee. Manyama ambaye ni baba yake.
"Kwa sababu ni uchumba tu na hakupeleki
popote hamna tatizo hata kidogo,mlete tu mwanangu mlete una maamuzi mazuri sana
sio kama wasichana wengine wanafanya upuuzi kimyakimya mambo yanapokuwa mabaya
ndio wanasema" alijibu mzee.Manyama huku akimshika mwanae huyo shavuni,Resh
akatabasamu na kumkumbatia baba yake "I love you dad(Nakupenda baba)"
Resh akamwambia kwa furaha tele mzazi wake huyo,huku moyoni akijiaminisha
kwamba hapatakuwa na kikwazo tena kwa mama yake kwani baba ndiye kichwa cha
familia.
Baada ya siku tano Adam aliwasili ndani ya kasri la mbunge huyu.Alikuwa
anaogopa na hakuamini kama angepokelewa na kama angepokelewa alijua yatakuwa
mapokezi mabaya sana kwani katika simulizi mbalimbali anazozisikia kwa watu
zilimwonyesha kwamba ni vigumu sana kwa wazazi kumwelewa mtoto wa kike
linapokuja suala la kumtambulisha mwanaume kama mchumba wake.
"Da Rosemary nina hofu mie" Adam
alimwambia dada yake kipenzi waliyekuwa wameongozana naye "Acha uoga bro
mbona hata sisi babu yetu alikuwa chifu? kwani chifu na mbunge nani zaidi"
alitania Rosemary kumwondoa hofu kaka yake.Mapokezi waliyoyapata kutokea kituo
kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo yaliwashangaza mno waliwakuta watu
wa kuwapokea na kwenda nao kwenye gari mbili walizokuja nazo,waliwafikisha hadi
getini ambapo kina dada wawili kwa heshima kabisa waliwaongoza hadi sehemu
maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao,japo usoni waliuficha mshangao wao lakini
moyoni uliwajaa tele.Adam akiwa ndani ya suti nyeusi wanazotumia wanasheria
katika shughuli zao na Rosemary aliyevaa suti pia walielekezwa wapi walipo
wazazi wa Reshmail wakaenda kutoa salamu zao,ilikuwa ni hafla kubwa sana
ndugu,jamaa na marafiki wapatao miamoja walikuwa wamealikwa na mheshimiwa huyu.
Ilikuwa kama harusi kwa asiyejua lakini ulikuwa utambulisho tu.
Bwana na bibi Manyama walipendeza kwelikweli na walikuwa na kila haki ya kuitwa
wakwe na Adam. Furaha ya Bi. Gaudencia ilificha chuki aliyokuwa nayo moyoni
dhidi ya Adam kwa kumchukua mwanae ambaye ndio alikuwa anampa raha zote za
dunia.
Hadi hafla inafikia tamati majira ya saa mbili
usiku kila mtu alikuwa amepata furaha kubwa sana,wabunge na madiwani ambao ni
marafiki wa karibu wa Manyama walitoa zawadi nyingi kwa wawili hawa huku babu
yake Reshmail akitoa mawaidha yenye maana kubwa sana katika maisha
waliyotarajia kuyaishi Reshmail na Adam siku za usoni.
Mzee Manyama kwa ombi la mwanae aliwasiliana na wazazi wa Adam kuwa muda wa
mapumziko ya siku tano alizobakiza Adam amalizie katika familia yake,hapakuwa
na kinyongo wala kipingamizi chochote walikubali kwa moyo mmoja na Adam
akaendelea kuishi pale huku dada yake akirejea Mwanza kwa usafiri wa ndege
ambao gharama zote zilikuwa juu ya mheshimiwa Manyama. Kila alipowasiliana na
wazazi wake Adam hakusita kuelezea upendo wa kipekee anaoupata kutoka familia
ya Reshmail hata wao walifarijika sana.
---------------------------------------------------------------------
Ilikuwa jumapili moja tulivu sana baada ya kutoka kanisani familia yote akiwemo
pia Adam,baba yake Reshmail aliongozana na mwanae kwenda mjini kwa lengo kuu la
kuonana na walimu mbalimbali wa masomo ya ziada(Tution) watakaompendeza
Reshmail basi waweze kumfundishia nyumbani.
Huku nyuma alibaki Adam pamoja na mkwewe (Mama Reshmail) baada ya kupata
kifungua kinywa Adam alimwaga mkwewe kuwa anaenda kuzungukazunguka bustanini
"Tena nilitaka nikwambie leo unataka uondoke hata bustanini hujawahi
kufika,afadhali nenda mwanangu" alijibu mama Reshmail.
Ulikuwa mpango
kabambe uliosukwa na Bi. Gaudencia,kwa dhumuni kuu
la kumwondolea mamlaka Adam ya kuwa na Reshmail. Kwa kuwatumia vijana kutoka
katika ngome ya vigogo,ngome maalum iliyokuwa inatumiwa na watu wenye pesa zao
kwa ajili ya kuwatenda vibaya watu wanaoonekana kuingilia mambo yao aidha
kimapenzi au kibiashara.Alipoaga anaenda bustanini Gaudencia alitumia fursa
hiyo kupiga simu kwa wanaume hao wa shoka ambao tayari alikiwa ameelewana nao
bei.
"Ndani ya dakika tano tutakuwa hapo” ndio
jibu lililotolewa upande wa pili
Bila kuongezea lolote Bi.Gaudencia alikata simu yake na kutoka nje.
"Babu kwa mama Veneranda si unapajua?" alitoa swali hlo Bi. Gaudencia
kwenda kwa mlinzi wao wa getini.
"Ndio si yule mama anayesuka pale mbele"
”Hapo hapo haya haraka nenda kaniangalizie kama kuna foleni kubwa"
aliamrisha Bi. Gaude na mlinzi akatii amri hiyo haraka haraka akaondoka katika
lindo lake akaenda kutimiza amri ya bosi wake.
Baada ya dakika takribani kumi alirejea mlinzi yule "Yupo mmoja tu
anamaliziwa" alileta taarifa hiyo kwa furaha.
"Haya mi ninatoka nimemwacha Adam ndani amelala akiamka mwambie nimetoka
kidogo" alisema mama Reshmail huku akiondoka.
“sawa bosi nitamwambia”
Masaa mawili badae alirejea akiwa amesukwa tayari nywele zake,ni muda huohuo
Reshmail na baba yake walikuwa wametoka mizungukoni,walimkuta Gaudencia
anatokea ndani. "Babu Adam alivyoamka ameenda wapi? au
bustanini?"Aliuliza Gaudencia na kuongezea "Maana nimegonga chumbani
kwake kimya,hebu Reshmail ingia ukamwangalie ndani mwake humo huenda amelala
bado" kwa mwendo wa maringo lakini harakaharaka Reshmail alijongea ndani.
"Babu unasema Adam hajatoka?" Resh aliuliza baada ya kurejea akiwa na
hofu kidogo usoni.
"Hajatoka na mimi hapa sijatoka tangu mama alipoenda kusuka na kumwacha
Adam amelala" alijieleza mlinzi yule jibu lililopokelewa kwa furaha na
Bi.Gaudencia.
Jambo gumu zaidi kwa ambao hawakujua janja ya mama huyu ni kwamba simu ya Adam
ilikuwa haipatikani hali hiyo ilileta wasiwasi sana,walisubiri huenda atarudi
hadi jioni hali ilikuwa tete ndipo mzee Manyama alipoamua kupiga simu kituo cha
polisi maeneo ya jirani kwa sababu alikuwa mbunge msako ulianza usiku huohuo.
Siku
tatu zilipita bila taarifa yoyote kutoka katika kituo cha polisi,Reshmail
alikuwa amepooza sana kupita maelezo mara kwa mara alimpigia baba yake simu na
kuuliza kulikoni lakini jibu bado lilikuwa lilelile kuwa hajapatikana.
"Mama niache tafadhali,tena niache nasema upuuzi wako siutaki tena
niache!" alifoka Reshmail pale mama yake alivyomkuta amekaa sebuleni na
kujaribu kumpapasa huku akimpa pole ya kupotelewa na Adam wake ghafla.
"Mwanangu usiwe na hasira kiasi hicho polisi watafanikisha upelelezi na
watamrejesha Adam akiwa mzima wa afya" alibembeleza Bi. Gaudencia lakini
Reshmail hakujibu kitu akajiondokea akiwa ameuvuta mdomo wake sana.
Siku ya tano polisi waliopewa jukumu la kufanya upelelezi
huo walirejea na taarifa yao huku wakiambatana na ushahidi. Zilikuwa nguo
aliyokuwa amevaa Adam kwenda kanisani ikiwa na matundu sita ya risasi na ikiwa
imetapakaa damu pote,suruali ilikuwa na matundu matatu ya risasi.
"Hapana hawezi kuwa Adam hata
kidogo nasema hawezi kuwa yeye" alifoka Manyama huku akiwa wimawima mbele
ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai jiji la Dar-es-salaam Chacha Boniphace
au maarufu kama Chacha B.
"Mheshimiwa lakini huu ni upelelezi wa
awali tunaendelea zaidi na zaidi tutazidi kutoa taarifa kadri tunavyopata
majibu mapya" alijieleza kwa utulivu bila wasiwasi kabisa jambo ambalo
kidogo lilirejesha amani ya Manyama japo hofu tayari ilishaukumba moyo wake
kwamba huenda Adam ameuwawa tena kikatili.
Ilikuwa ni shughuli pevu kwa Reshmail kuamini kile ambacho alikuwa anaelezwa na
baba yake kwamba Adam anadhaniwa kuuwawa kwa risasi nane kisha mwili wake
hauonekani. Bi. Gaudencia tayari alikuwa anaangua kilio kikubwa hata kabla
maelezo hayajaisha ikawa kazi kwa mumewe kumbembeleza.
"Mke wangu Adam hajafa ila inadhaniwa pia upelelezi bado unaendelea
jamani,ukilia hivyo unakuaribisha msiba mama watoto sawa" alibembeleza
mzee Manyama huku amemkumbatia mkewe.
"Baba haiwezekani baba haiwezekani nguo za Adam zipatikane katika hali
hiyo halafu mnasema hajafa,jamani Adam wangu wamemuua" alipiga mayowe
Reshmail ikamlazimu mzee Manyama kufanya kazi mara mbili jambo ambalo lilimtoa
jasho mzee huyu.
"Reshmail mwanangu,tulia hiyo siyo taarifa rasmi jamani ni majibu ya awali
mbona mnanifanyia hivyo au mnataka nipate presha nife?" alijieleza Manyama
huku akijifuta jasho kwa kutumia shati lake. Reshmail mbio mbio akaondoka pale
sebuleni akaanza kuzipanda ngazi kuelekea chumbani kwake huku akilia,mzee
Manyama nae huyo nyuma yake.
"Reshmail mwanangu,njoo malkia wangu,njoo
mwanangu" aliyazungumza hayo huku akimkimbiza kwa nyuma. Wakati huo Bi.
Gaudencia tayari alikuwa amenyamaza kimya kabisa,akijaribu kupikicha
macho yake.Reshmail hakusimama hadi chumbani
kwake akajifungia,baba yake alibembeleza mpaka akachoka hakupata jibu zaidi ya
kilio cha kwikwi kutoka ndani.
"Baba Resh twende chumbani mume wangu,twende utakaa hapa hadi saa ngapi
cha msingi tumwombe Mungu asije akajidhuru mwanetu" Gaudencia alimnyanyua
mumewe wakajikongoja kuelekea chumbani kwao,Manyama akiwa amelegea kabisa.
Asubuhi ya siku iliyofuata naibu waziri wa ulinzi na usalama,alifika na msafara
wake wa magari matano kwa mbunge Manyama kuja kutoa pole ya kutokewa tukio hilo
lenye utata kwa mwenzao. Shughuli ngumu iliyokuwa mbele yao ni jinsi gani
watawaeleza wazazi wake Adam ambao hadi dakika hiyo waliamini Adam yupo salama
na mwenye furaha kwa mchumba wake Reshmail,Manyama alimuomba waziri
ashughulikie hilo suala na bila kupoteza muda alinyanyua simu yake ya mkononi
na kutoa taarifa hiyo kwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mwanza pamoja na
mawasiliano anayoweza kumpata baba yake Adam. Ilikuwa vigumu sana kwa baba Adam
kuelewa anachoelezwa lakini kwa kadri ya uwezo wake na taaluma yake mkuu huyo
alifanikiwa kumwelewesha ambapo baba yake Adam aliondoka akiwa na matumaini
kwamba ipo siku Adam atapatikana.
Nyumba nzima ya kina Adam ilipooza sana dada yake Adam (Rosemary) alikuwa
analia muda wote kwa uchungu hakuamini kwamba siku ile pale uwanja wa ndege
alivyosindikizwa na familia nzima ya mhe.Manyama ndio ilikuwa mara ya mwisho
kumwona kaka yake kipenzi(Adam).
Uongozi wa polisi uliifikisha taarifa hiyo pale chuoni ambao pia walipokea kwa
simanzi kubwa.
"MAUAJI YA KUTISHA", ndivyo mandishi
meusi kabisa kwenye magazeti mbalimbali yalisomeka,hali hiyo ilithibitisha
kabisa kuwa Adam hayuko hai tena. Picha yake iliyoambatanishwa na habari hizo
akiwa na mtoto wa mbunge iliteka na kuumiza mioyo ya watu wengi hasahasa
vijana."Tumempoteza mwanasheria" ndilo neno la pamoja walilosema
wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino Mwanza katika misa ya pamoja
kumwombea mema Adam kama yupo hai au kumtakia pumziko jema la milele kama
tayari Mungu ameichukua roho yake,kila uso ulikuwa na simanzi kubwa ilikuwa
kama tamthilia.
Reshmail alikuwa kama zezeta,hamwelewi mtu yeyote,roho yake ilimwambia kwamba
mama yake mzazi anahusika kwa namna moja au nyingine katika tukio hili
lililojaa utata. Lakini ataanzia wapi kumweleza baba yake,atajisikiaje mzee
Manyama akigundua kwamba mke na mtoto wake walikuwa katika ndoa haramu ya siri
ndani ya nyumba yake."Hapana sitaki kuongeza tatizo juu ya tatizo
nitasubiri liwalo na liwe,kama Mungu alimpanga Adam awe wangu naapa sitaolewa
na mwingine kamwe,lakini kama hakuwa halali yangu basi ataletwa mwanaume
duniani kwa ajili yangu tena"Alijipa ujasiri wa hali ya juu Reshmail huku
akijipigapiga kifuani."Nitarejea shule na nitasoma tena kwa bidii
sana,sitamwaza mwanaume yeyote tena alikuwa Adam na atabaki kuwa Adam hadi
Mungu aamue tena" aliendelea kujipa matumaini."Bibi yangu aliniambia maneno
ya mdomo huumba halisi,na nina uhakika ninachokiongea kwa mdomo wangu Mungu
ataniumbia" aliendelea kuongea huku machozi yakifumba macho yake na
kitambaa alichokuwa anatumia kujifuta kilikuwa kimelowana tayari kwa wingi wa
machozi alikuwa kama yatima vile,Resh alikuwa akifungasha baadhi ya mizigo yake
tayari kwa kurejea shuleni tena,tangu tukio la Adam kupotea hakuna aliyetegemea
hata siku moja Resh atawaza kurudi tena shuleni kwani waziwazi akili yake
ilionekana kuathirika kwa kiasi kikubwa kwa kumpoteza Adam katika mazingira
yasiyoeleweka.
"Baba kesho narejea shule si unajua tayari shule imefunguliwa?"
Reshmail alimkurupua mzazi wake huyo kutoka alipokaa kwa mshangao
"Umesema nini malkia wangu!" alihoji
Manyama huku akiwa wima
"Narejea shule kesho" kwa msisitizo
na tabasamu alijibu Reshmail. Mzee Manyama hakuamini kwani alikuwa akiwaza ni
namna gani atamshawishi mwanae aweze tena kurejea shuleni baada ya matatizo
yote yaliyojitokeza kwa mchumba wake Adam ambaye hadi wakati huo bado mwili
wake ulikuwa haujapatikana wala taarifa yoyote zaidi ya nguo zikiwa na matundu
ya risasi na damu."asante sana mwanangu nakupenda sana" mzee Manyama
aliongea kwa furaha huku akimkumbatia mwanae.
Tangu kupotea
kwa Adam aliyehisiwa kuwa tayari amekufa kulipokelewa kwa hisia tofauti na
wananchi huku asilimia kubwa ikiegemea upande wa imani potofu za kishirikina
wakihusisha tukio hilo na utajiri alionao Mh. Manyama na uchaguzi uliokuwa
mbele yake.
------------------------------------------------------------
"Wamemtoa
mwanangu kafara ili waongeze utajiri,nilimwambia Adam aoe msukuma mwenzake ona
sasa,watoto wa siku hizi wabishi wanajifanya wanajua sana na elimu yao
inawadanganya" mama yake Adam alikuwa analaani vikali mbele ya mume wake wakiwa
ndani ya nyumba yao maeneo ya Igoma kwa 'one-way'
"Usiseme hivyo mama Adam kumbuka sisi ni wakristu,tumwachie Mungu yeye
ndio atajua nini cha kufanya" Babaye Adam alimtuliza mkewe huku
akimgongagonga mgongoni kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kuume.
Mawasiliano baina ya familia hizi mbili ya Adam jijini Mwanza na ya Reshmail
jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamekatika licha ya baba yake Adam (mzee Michael)
kutangaza kuwa kutoka moyoni mwake amesamehe yote yaliyotokea na anaamini ni
mipango ya Mungu lakini kinyongo kilionekana dhahiri kwa matendo,upendo wa
zamani haukuwepo tena jambo hilo lilimfadhaisha sana mzee Manyama kiasi cha
kukondeana na kukosa umakini katika utendaji wake wa kazi jambo lililoishusha
sana heshima yake kama mbunge aliyekuwa anaheshimika sana kuanzia bungeni hadi
jimboni kwake,wapinzani walitumia fursa hiyo kumchafua hasahasa na kweli uchafu
huo ukakubalika kwa wananchi kwa ujumla Manyama hakuwa na lake tena
pale,wananchi walimpuuzia sana tofauti na zamani na hata hiyo miaka miwili
iliyobaki wananchi waliiona kama ni mingi sana kuwa na kiongozi wa aina yake.
Kuliko fedheha yote hiyo Mh. Manyama kwa hiari
yake mwenyewe alipitisha kura ya maoni ya wananchi kuhusu imani waliyonayo
kwake kama mbunge wao. Asilimia 70 ya waliopiga kura walidai hawana imani naye
huku asilimia kumi na nne tu ndio wakidai bado wana imani naye na kura
zilizobaki zikiharibika,rasmi Manyama akawa ametolewa bungeni na katika
uchaguzi mdogo uliofanyika akachaguliwa mbunge kutoka chama cha upinzani na
maisha yakaendelea huku Mh.Manyama akiendelea na biashara zake mikoani.
-------------------------------------------------------------------------
Adam akiwa pale bustanini alivamiwa ghafla na wanaume wawili wa shoka wakiwa na
bunduki,ishara ya kidole mdomoni ilimfanya atulie tuli kisha wakamwonyesha
ishara kwamba awafuate alifanya kama walivyotaka hadi kwenye gari iliyokuwa
imepaki pembeni kidogo ya nyumba yao Adam alishangazwa sana na ukimya
uliokuwepo hakuwepo mlinzi wala mama mkwe wake.Safari yao ilikwenda mpaka
Iringa gari iliyokuwa na vioo vyeusi 'tinted' ilimzuia Adam kujua ni wapi
alipo,gari ilizimishwa ndani ya jumba kubwa sana ambapo alipelekwa kwenye
chumba kikubwa tu,hofu kubwa ilimtawala hakujua kwa nini yuko pale,hakupigwa
wala kupewa bughudha yoyote,hali hiyo ilzidi kumshangaza "au ndio wachuna
ngozi" alijiuliza Adam kwa hofu tele.
Hayo ndio masharti ambayo mama Reshmail alitoa
kwa vijana aliowapa tenda hiyo ya kumtorosha Adam pale nyumbani. Shida yake
haikuwa kumtesa Adam bali kumweka mbali na mwana (Reshmail) ambaye alikuwa
amempagawisha ipasavyo katika mapenzi ya jinsia moja.Suala la pesa halikuwa
tatizo hata kidogo alichohitaji ni kutimiziwa alichotaka. Mkataba wa miaka
mitano ndio alioingia na watu hawa kukaa na Adam bila kumruhusu kutoka nje ya
jingo.Bi Gaudencia aliamini kwamba kwa kutokomea Adam mbele ya uso wa Reshmail
ilikuwa fursa nzuri ya kurudisha tena uhusiano wake na Reshmail ambao ulikuwa
unaelekea kufa lakini kinyume chake alikuwa ameibua chuki kubwa baina yake na mwanae
“heri wote tukose kama ni hivyo” alijiapiza mama Reshmail baada ya
kuona dalili za kumshawishi Reshmail hazipo tena
Alikuwa
ni Reshmail mwingine kabisa mkasa uliomkumba ulimbadilisha sana na kuitanua
akili yake sana,Eveline naye alisikitishwa na yaliyomkumba shoga yake
akajitahhdi sana kuwa karibu naye kumpa moyo huku akijiepusha sana kufanya
vitendo ambavyo vitamkumbusha Resh jinsi alivyoweza kukutana na Adam. Ni katika
kujiepusha na kumkera rafiki yake huyo kipenzi Eveline akajikuta amefuta picha
za uchi na filamu za ngono katika kompyuta yake akawa si mtu wa kutoroka
shule,hakuwa tena mtu wa wanaume na hatimaye akawa Eveline wa kuigwa na
wanafunzi wenzake jambo hilo liliwaduwaza sana wanafunzi pale shuleni lakini
ndio hivyo Eve alikuwa amekubali mabadiliko katika maisha yake. Juhudi zao
katika masomo ziliendelea kuwaweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri
mtihani wao wa mwisho. Hawakuyazungumzia tena yaliyopita tena walijadili mapya
na yanayowanufaisha "Eveline wewe ni kama dada yangu nakupenda sana"
"Nakupenda pia Reshmail umebadili maisha yangu moja kwa moja nina maisha
mazuri sasa" alijibu Eva kwa upole huku akimwangalia Reshmail aliyekuwa
anaishusha chandarua yake aweze kulala. Ni kweli walitokea kupendana wawili
hawa.
"Hivi Resh una mpango bado wa kusomea uhasibu mi lazima niwe mhasibu"
"Mh! unavyojiaminisha utadhani tumefaulu tayari" alijibu Resh.
"He! mi najua sisi kufaulu kwetu sio swali ni jibu,swali ni je tunaenda
chuo gani na kusomea nini." alijiaminisha Eveline.
"ok! nilidhani nitasomea uhasibu lakini
kwa heshima ya Adam nitasomea sheria" alijibu Reshmail kwa furaha.
"Mh! na upole wako huo na mambo ya kutoa hukumu wapi na wapi? mwenzio
naangalia ankara" alisema Eva.
"Wala hata siendi kuhukumiana naenda kwa heshima tu" alisisitiza
Reshmail.
"Mh! haya mheshimiwa hakimu napenda kujitetea kama ifuatavyo" Eve
alitania akifuatiwa na kicheko kikubwa kutoka kwa Reshmail.
------------------------------------------------------------------------------
Maisha yaliendelea vyema sana tu japo yalikuwa maisha ya mashaka Adam
aliruhusiwa kuongea na kuuliza kila kitu kasoro swali moja tu "Kwa nini
niko hapa?",ndio hakuruhusiwa kuliuliza hata kwa mbali,watu wote pale
hawakuwa na ubaya nae hata kidogo,hawakumtesa,hakugombezwa wala hakufanya
kazi,alipewa huduma zote za msingi,aliweza kutoka nje na kwenda bustanini
lakini nje ya geti hakuruhusiwa. Tayari aliyazoea maisha haya lakini kumbukumbu
ya jinsi alivyochukuliwa ndani ya jumba la wakweze bila kupata msaada wowote
ule "Nani atakuwa nyuma ya haya yote mlinzi alikuwa wapi? Mama Resh
je?" alijiuliza sana bila kupata wa kumpa jibu.
"Hivi unaitwa dada nani vile?" Adam alimuuliza dada mmoja ambaye kila
baada ya siku tatu alikuja kufanya usafi katika chumba chake.
"Naitwa Beatrice Cosmas niite Bite"
alijibu huku anafuta vioo kwa dirisha la chumba cha Adam.
"Una jina zuri wewe mh!"Alisanifu Adam.
"Asante wewe ni Adam eeh!" aliongezea yule binti huku akiwa ameacha
shughuli yake aliyokuwa anafanya.
"Ndio mimi ni Adam! samahani nikuulize maswali machache"
"Uliza tu lakini sitakujibu sasa hivi"
"Kwa nini?"
"We uliza yote ndo nitakwambia kwa nini"
"Hivi hapa ni wapi? kwa nani? na kwa nini nipo hapa?"
"Ndio hayo matatu tu?...sawa nitakujibu kwa sharti dogo sana yaani"
"Sharti gani hilo mi nipo tayari"alitoa uhakika Adam bila hata
kulijua sharti lenyewe.
"Sikia Adam sina haja ya kuzunguka zunguka nina mwaka wa pili hapa kitu
kinaitwa mwanaume katika mwili wangu ni kama ndoto sasa ni wewe wa kutii kiu
yangu na mimi nitajibu maswali yako" alijieleza Bite,jambo ambalio
lilikuwa zito na la kumshangaza Adam.
"Mh! au ndo mtego tena kutoka kwa
Reshmail? dah! ikiwa hivyo nitaaibika kweli mimi"Alijiwazia Adam kwa
mashaka makubwa kabla ya kujibu.
"Basi utakuja kunijibu baadaye!" alisema Adam.
"Haya usiku na wewe jiandae" alijibu na kuaga Bite.
Hayawi hayawi mara yakawa usiku wa saa tatu,Bite tayari ndani ya chumba cha
Adam ndani ya khanga moja peke yake.
"Haya nipe nikupe hakuna longolongo hapa" alizungumza Bite.
"Subiri taratibu basi,sikiliza"
alianza kujitetea Adam wakati Bite anajisogeza kitandani,Adam alikuwa
amechelewa tayari joto la Bite lilipenya katika mwili wake na kumchanganya hadi
kujikuta akifanya kinyume na alivyotarajia kwamba atafanikiwa kutegua mtego wa
Bite badala yake alikuwa ameshafanya mapenzi na Bite. Kwa Bite ulikuwa ushindi
mkubwa sana kwani tangu aletwe hapo kuwa msaidizi wa kazi za ndani ya vyumba
hakuwahi kutoka nje ya jengo hilo,sio kwamba alikuwa amefungwa hapana kila kitu
kilikuwepo ndani kila siku pia alikuwa ameridhika kuwa hapo.
"Hapa ni Iringa,nimejibu swali lako la kwanza tuendelee tena nikujibu
swali la pili na tatu" alisema Bite kwa shauku kubwa sana.
"Hapana Bite imetosha kwa leo sijisikii vizuri,siku nyingine basi
sawa!" alidanganya Adam na Bite hakuwa mbishi akambusu Adam shavuni
akajiondokea zake.
Ilimchukua takribani siku tano Bite kugundua kwamba tayari ameshika ujauzito
jambo ambalo halikuruhusiwa katika jumba hilo na alipewa onyo kali wakati
anaingia hapo. Kwa usalama wake na Adam alifikiria suala la kutoroka lakini
haya yote aliyafanya baada ya kuongea na Adam na kumweleza hali halisi. Ni
katika wasaa huo alimweleza Adam chanzo ambacho kinaweza kuwa kimemsababishia
yeye kuwepo pale "Umemchukulia kigogo mpenzi wake,umemendea mtoto wa
kizito au umemkataa kimapenzi mtu maarafu" hizo ndizo zilikuwa baadhi ya
sababu alizoorodheshewa na Bite,lakini kwake yeye aliona hakuna hata moja
inayomuhusu kwani wazazi wote wawili wa Reshmail walimpenda sana hakuwa tayari
kuweka hisia kwamba pengine moyoni wanamchukia.
"Usijali lakini hutakaa milele humu,huwa unafika
Muda aliyekuweka humu akiridhika unatoka.
"Nitamlea mtoto,napenda watoto hata kama usipokuwa mpenzi au mume wangu
nitampenda sana na nitamwita....."
"Christian akiwa mvulana au Christina akiwa msichana" alidakia Adam
ambaye kwa mbali alianza kumtamani Bite kimapenzi.
------------------------------------------------------------------------------------------------------
Biashara za baba yake
zilikuwa zinaendelea vizuri na skendo lake lilikuwa linafifia taratibu. Hadi
anamaliza kidato cha sita Reshmail mapenzi kwa wazazi wake yalikuwa palepale na
japo hakutaka kumwongelea Adam jena alikuwa na picha yake waliyopiga pamoja
siku moja kabla ya tukio lile la kushangaza na kuumiza. Reshmail kwa ruhusa ya
wazazi wa Eveline alienda nae mpaka kwao ambapo walikaa wote kwa siku tano
kisha akarejea tena Arusha. Urembo wa Reshmail ulipagawisha kila mwanaume na
hata baba yake ilifikia kipindi akakiri kwamba kweli pale alizaa mtoto mmoja wa
kipekee na kweli alikuwa wa kipekee. Mama Resh bado alikuwa na matamanio lakini
kwa ssa alimwogopa sana Reshmail tofauti na miaka mingi iliyopita.
"Baba na mama wiki ijayo nataka kwenda Mwanza kwa wazazi wa Adam"
Resh alitoa hoja yake wakiwa mezani wanakula.
"Wapi? Mwanza! hawatakuelewa mwanangu
utakuwa kwa maksudi kabisa unafufua shari iliyopoa tayari.
Tayari"Kwa busara tele na upole mzee
Manyama alimweleza mwanae ambaye pia aliyapokea kwa nidhamu ya hali ya juu na
kichwa chake kuyakubali kuwa yana maana kubwa ndani yake."Nimekuelewa baba
sitaenda tena" alijibu kwa unyenyekevu sana Reshmail.
Muda mwingi wakati anasubiria matokeo aliutumia kuimba na kusikiliza muziki na
mara chache sana kwenda kutembelea rafiki zake walioishi jirani naye.
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Matokeo ya kidato cha sita yalipotoka hayakuwa ya kushangaza sana kwa upande
wake kwani alikuwa amevuna alichokipanda. Reshmail alikuwa amepata daraja la
kwanza na ndivyo alivyotarajia,furaha yake iliongezeka baada ya kumwona katika
orodha Eveline Maige rafiki yake kipenzi naye akiwa amepata daraja la kwanza
huku wakitofautiana pointi kadhaa. Akiwa anajiandaa kumpigia simu tayari simu
yake iliwakawaka na kuandika "pacha" jina ambalo alikuwa amemwandika
Eve katika simu yake,badala ya kuongea wote kwa pamoja wakaanza
kucheka,walicheka sana hadi simu ilipokatika. Zilikuwa ni furaha kutoka
moyoni,kwa nini wasifurahi wakati ndoto zao zilikuwa zinatimia?
Tanzania Commission of Universities (T.C.U) ilipotoa uchaguzi wa kwenda vyuoni
Reshmail kama alivyopenda alichaguliwa chuo kikuu cha mtakatifu Augustine
Mwanza kwa masomo ya sheria huku Eveline Maige akipelekwa Mzumbe chuo kikuu
kwenda kuchukua masomo ya uhasibu shahada ya juu.
"Ndugu hakimu naomba kujitetea!" Eve
alimtania Resh utani wao wa shuleni siku walipokuwa wanaagana.Walikuwa
wametenganishwa hatimaye lakini mawasiliano yao yalidumu
Kama alivyojiwekea kiapo chake cha kutopenda
hovyohovyo ni hivyohivyo alivyoingia pale chuoni,hakuringia uzuri wake lakini
hakutaka pia usumbufu unaopitiliza kutoka kwa wanaume yaani kwa kifupi alikuwa
na msimamo mkali sana,ni rafiki yake (Eve) pamoja na wazazi wake ambao
wangeweza kubashiri sababu hasa inayomfanya binti huyu awe hivi na si mtu
mwingine pale chuoni.
Maringo yake yalifichwa na werevu wake darasani,kwani ilikuwa ni warembo
wachache sana wa aina yake waliofanya vizuri kimasomo,jambo hilo lililowavutia
waalimu wengi sana na wanafunzi ambao wanapenda maendeleo kimasomo. Reshmail
hakuwa mtu wa mambo mengi hakunywa pombe wala kwenda kumbi za starehe usiku
starehe yake ilikuwa ni kusoma na michezo.
Mnamo mwezi wa pili michezo ya FAWASCO
ilipoanza michezo hiyo inayohusisha vitivo vyote pale chuoni,kwa maksudi
alichaguliwa kuwa mhamasishaji kwa wasichana wajibu alioufanya vizuri ipasavyo
na kikubwa zaidi akawa pia mdhamini mkubwa sana. Moyo wake wa kujitolea
uliwavutia sana wanadarasa wenzake ambao baadhi walimpenda huku wengine wakidai
ana maringo, msimamo wa Reshmail ulibaki palepale.
Mwaka wa pili pale chuoni ndio ulikuwa mbaya kwake. Darasa walilolitumia mwaka
wa pili wanafunzi wa kitivo cha sheria,lililojulikana kama Mombasa Raha kwa
mbele lilikuwa na picha kubwa sana ya Adam ambayo ilikuwa pembeni ya ubao wa
kufundishia hiyo ikimaanisha kwamba kila atakapoingia darasani lazima
aione,"ADAM THE GREAT" yaliandikwa maandishi haya chini ya picha
kubwa ya Adam. Amani,ikatoweka kabisa moyoni mwake kumbukumbu mbaya za
kumpoteza mpenzi wake Adam zikaanza kumrejea kwa kasi sana.Reshmail akaanza
kujihisi yeye ndiye chanzo cha yote hayo,tofauti na waalimu wake hakuna
mwanafunzi aliyemfahamu Adam zaidi ya kujua tu historia ya yaliyomkuta na wengi
kuichukulia kama simulizi tu ya kusadikika. Reshmail alianza kuwa mtoro
darasani na hata alipoingia badala ya kumwangalia na kumsikiliza mwalimu,mawazo
yake yote yalivutwa na picha ya Adam yenye tabasamu pana mara zote aliamini
inamuangalia yeye na kumlaumu kwa kumkatisha masomo yake kwa penzi la
mtandaoni. "Adam stop blaming me!!(Adam usinilaumu)" alipiga kelele
kwa nguvu Reshmail bila kujitambua,mwalimu alimshangaa na hakuelewa kilikuwa
kimemsibu nini "Is she dreaming? (Anaota?)" aliuliza mwalimu Sijjo
aliyekuwa anawafundisha somo la mawasiliano (Communication skills),darasa zima
likacheka kwa fujo sana,lakini Reshmail alikuwa analia huku akitetemeka
sana,kwa ghadhabu akasimama na kutoka nje. Japo ulikuwa ni mwezi mmoja tu tangu
waanze masomo ya mwaka wa pili lakini
tabu na mateso aliyokuwa ameyapata yalitosha
kumshawishi kuwa huenda amesoma hapo kwa miaka kumi.Wazazi wake hawakuwa na la
kufanya,Eveline alibaki kumwonea huruma shoga yake huyu alijaribu mara kwa mara
kumpigia simu lakini haikuwa tiba ya tatizo la Reshmail. Ni kweli Reshmail
asingeweza kujilazimisha kuwa na furaha kwani ni yeye aliyemshawishi Adam awe
nae kimapenzi na ni yeye huyuhuyu alimshawishi Adam aende kwao kwa ajili ya
kujitambulisha na safari hiyo ikawa ya mwisho ya Adam. "Nikiwaambia
waalimu wangu watanielewaje,na hata wakinielewa itakuwaje wanafunzi wenzangu
wakijua siri hii? watajenga picha gani tena kuhusu mimi,mh! niepushe na hali hi
bwana,kama uliweza kuniondolea mawazo haya hadi nikamaliza kidato cha sita
vyema hebu baba na sasa ondoa tena na hili jaribu zito mbele yangu
na jina lako lisifiwe." aliweka ombi fupi Reshmail katika mawazo yake hayo.
Lilikuwa ni jambo gumu sana kwa Reshmail alikonda sana na punde si punde maneno
ya wakosaji yakaanza tena "Mh! kumbe ndio maana anakataa wanaume kumbe
anaishi kwa matumaini maskini,dada mrembo kama huyu" yalisikika maneno
hayo katika vijiwe vya wanafunzi pale chuoni. Ilikuwa ni kero kubwa kila
alipokatiza vidole vilimwelekea yeye umaarufu wake wa awali kwamba ni mrembo
ukaongezeka maradufu karibia chuo kizima lakini wakati huu ilikuwa ni sifa
mbaya kwamba ana virusi vya UKIMWI hata yeye aliyasikia maneno hayo yalikuwa
yakivuma kwa kasi,hakuwa na uwezo wa kuzuia tetesi hizo "Wangejua kwamba
mi ni bikra na wanayoyasema yote ni uongo,hata wasingenyanyua midomo yao
michafu kuropoka upuuzi huo,lakini bila Adam watajuaje?" alijiuliza
Reshmail akiwa chumbani mwake katika hosteli ya Ngulelo aliyokuwa amepanga
chumba alichoishi peke yake. Marafiki zake taratibu wakaanza kumtenga wakiamini
ameathirika,hilo halikumuumiza kichwa kwani alilitegemea sana hasa hasa dhana
ya unyanyapaa kwa waathirika iliyokuwa inatawala chuoni hapo.
-----------------------------------------------------------------------------
Bite alifanikiwa kutoroka katika ngome ile kubwa aliyokuwa amehifadhiwa Adam.
Kwa jinsi alivyokuwa amezoeleka pale haikumchukua muda mrefu kumshawishi mlinzi
amfungulie geti atoke kidogo na ndio ikawa jumla hakwenda mbali sana na mkoa
wa Iringa bali aliweka kambi yake maeneo ya Uyole Mbeya mkoa uliopo
jirani na Iringa ambapo kipesa kidogo alichoondoka nacho pale ndani alifungua
kibanda chake sokoni na kupanga nyumba eneo jirani la Igawilo akianzia maisha
ya kulala chini hadi aliponunua godoro.Biashara ya kuuza nyanya
na mbogamboga ilimkimu sana maisha yake kwani
wazo wala tegemeo lake halikuwa kununua gari,au kujenga nyumba hapana lengo
lake lilikuwa uhai pekee,na shilngi elfu moja alizozipata zilikuwa zinamtosha
kabisa. Alikuwa mchangamfu na mstaarabu sana,wateja walivutika kwake kwa kasi
kufaidi ukarimu wake katika biashara.Tumbo lake lilianza kukua taratibu,kina
mama sokoni wakaanza kuhisi tayari Bite kapata mjanja Mbeya amemjaza
mimba,lakini miezi yake ya kujifungua ndiyo ilifungua akili za waliokuwa na
maswali na kugundua kwamba ile mimba alikuja nayo pale na sio kwamba aliipatia
pale. Salama bin salmin Bite alijifungua mtoto wa kiume miezi tisa ilipowadia.
"Mh! baba yake atafurahi tena alimpa jina
pale tu nilipomwambia nimeshika mimba" Bite kwa furaha tele aliwaambia
kina mama wa pale sokoni,akiwemo jirani yake mama wawili,ni hao ndio walikuwa
ndugu zake."Hongera Bite,sijui ndio unakuwa mama nani vile" Bite
alihojiwa na mama wawili
"Mwanangu anaitwa Christian"
alijibu Bite huku akibusu kichanga chake hicho ambacho kilikuwa kinarusharusha
miguu na mikono yake huku na huko.
Christian
alizaliwa akiwa na afya tele na hakusumbuliwa na magonjwa wakati wa ukuaji wake
mwaka wa kwanza,ilikuwa furaha kubwa kwa mama yake.
----------------------------------------------------------------------------
Miaka ilizidi kukatika wazo la Bi. Gaudencia
kumtoa Adam katika jumba lile lilikuwepo kichwani mwake kwani udhaifu alioupata
Reshmail pamoja na kashfa mbaya anazozipata pale chuoni zilimsononesha sana
lakini ataanzia wapi kuificha aibu yake pale ambapo Adam,akasababisha uovu wa
mama huyu uwekwe hadharani. Ni jambo hilo lililomuumiza kichwa mama huyu.
Reshmail na baba yake watanielewaje kwa mabaya niliyowafanyia,nimeishusha
heshima ya mume wangu aliyekuwa na heshima kubwa bungeni" alizidi kuwaza
Huku Iringa maeneo ya Ruaha Adam alikuwa anauanza mwaka
wa tatu,akiishi kama nyumbani kwake,lakini hakuridhika hata kidogo maisha hayo
ya ufungwa. Miaka mitatu ilikuwa mingi sana "Mama na baba yangu wanahisi
niko wapi? vipi kuhusu mpenzi wangu Reshmail,hapana imetosha nahitaji kutoka
hapa,lakini lazima nijiulize nitatoka vipi hapa katika ngome hii"
alijisisitiza Adam japo ulinzi madhubuti ulioongezwa kutokana na kutoroka kwa
Bite katika mazingira ya kutatanisha pale ngomeni
***
Mwaka wa pili uliisha hivyohivyo kimateso
makali yaliyojawa na kumbukumbu mbaya na isingekuwa kuhamishwa kwa darasa la
sheria mwaka wa pili kwenda katika maghorofa ya Mwanjonde chuoni hapo basi
Reshmail angefeli vibaya masomo yake kutokana na msongo wa mawazo.
Akiwa mwaka wa
tatu afya yake ilirejea tele kwani hakuwa akiiona tena picha kubwa ya Adam
machoni pake hali hiyo ya afya kurejea ilizusha msemo mpya tena,tofauti na
mwanzo walivyosema ana Ukimwi,sasa walisema "Akikonda ana virusi,akinenepa
ameanza kutumia dozi" yote hayo alituhumiwa Reshmail lakini kamwe hakuwahi
kuthubutu kunyanyua mdomo wake kujibu vijembe hivyo yeye alikuwa mkimya huku
akipambana na masomo hadi alipoumaliza mwaka wake wa nne vyema.
Mnamo mwezi wa kumi na
moja familia yake yote ilisafiri kuelekea jijini Mwanza kusheherekea kwa pamoja
mahafali ya mtoto wao,Eveline ambaye tayari alikuwa kazini baada ya kuwa
amemaliza miaka yake mitatu chuoni na kufaulu vizuri pia alijumuika katika
kukamilisha furaha hii ya rafiki yake mpenzi huku akiongozana na mchumba wake
Benjamin Simon. Reshmail alifurahishwa sana na ujio wa Eve kwani alizidi
kudhihirisha kuwa ni kiasi gani yeye ni rafiki wa kweli.
Yalikuwa ni mahafali makubwa na ya kipekee kuliko yote yaliyowahi kutokea
ambapo chuo cha Mt.Augustino kilifanya mahafali ya pamoja na matawi yake yote
Tanzania,yaani Iringa,Mtwara na Tabora. Kwa ufupi yalikuwa yamefana.
Ni katika pirikapirika na pitapita za huku na huko
za sherehe hiyo ndipo Reshmail akiwa na
Eveline ana kwa ana anakutana na familia ya Adam yaani baba na mama
yake,aliwatambua kwa uwepo wa Rosemary yule mdogo wake Adam. Rosemary alikuwa
ndio kwanza amehitimu shahada ya elimu katika chuo kikuu cha mtakatifu
Augustino tawi la mtwara hivyo yeye na familia yake pia walikuwepo katika
viwanja vya Raila Odinga kusheherekea mahafali
yale."Mchawi...mchawi!" alianza kupiga kelele mama yake Adam wakati
Reshmail akisogea taratibu katika eneo walilokuwepo kwa furaha
"Uuuwii" alipiga makelele kwa sauti ya juu jambo lililovuruga usikivu
katika eneo lile na watu kuanza kumwangalia yeye kama mtu
aliyechanganyikiwa,Reshmail na Eve walikuwa wameganda tu na mama Adam akizidi
kupiga kelele,jitihada za baba yake Adam kumtuliza mkewe hazikufua dafu,mara
ghafla mama Adam akakurupuka akiwa na chupa iliyokuwa na soda ambayo
haijafunguliwa bado na kwa kasi akaenda kumkabili Reshmail ambaye akili yake ni
kama ilikuwa imesimama na umati uliokuwa umemkazia macho kwa kitendo cha kuitwa
mchawi ulimzidishia hofu na fedheha kwake,Eve alimshika mkono Reshmail na
kujaribu kumvuta watoke eneo lile lakini tayari mama Adam alishawafikia na kwa
nguvu kabisa akaituliza chupa ile juu ya kichwa cha Reshmail palepale akaenda
chini huku damu nyingi ikimtoka kichwani. Wanaume watatu akiwemo pia baba yake
Adam walifika na kumbeba juu juu,mama Adam ambaye alionekana dhahiri kuwa bado
hajaridhika na kipigo alichotoa kwa Reshmail kwani bado alikuwa anaangaza huku
na huko kama palikuwa na silaha nyingine. Alikuwa kama mwendawazimu
Wengine walimbeba Rshmail ambaye joho lake la
kipekee kabisa lilikuwa limechafuliwa vibaya na vumbi la uwanja wa mpirawa
miguu wa Raila Odinga ambapo ndio sherehe zilifanyika. Hali ya sintofahamu
ilitawala sherehe zile kwa takribani nusu saa nzima hadi Reshmail
alivyoondolewa na familia yake kuelekea hospitali na mama Adam kutiwa katika
nguvu ya dola
---------------------------------------------------------------------
Halikuwa jeraha kubwa sana nyuzi mbili
zilipita katika kichwa chake kushona jeraha lile
“kwa nini mama mkwe wako akutende hivi” eve
alimuuliza Reshmail akiwa pale kitandani
“ni haki yake hata kunipiga risasi mimi ni
chanzo cha maumivu haya wanayoyapata” alijibu Resh huku akilazimisha tabasamu
“kwa hio hapa amenionea huruma sana mimi ni
sawasawa na muuaji tena wa kukusudia na haki yangu ni kuuawa pia” aliendelea
Reshmail huku akitoa tabasamu hafifu tena
“usiseme hivyo mamii sio wewe uliyetaka iwe
hivyo ni Mungu pekee” aliongea kwa upole Eve huku akivibinyabinya vidole vya
Reshmail
“mama mwambie baba afatilie mama mkwe asije
kulazwa selo hata kwa saa moja hana kosa lolote” Reshmail alimwambia mama yake
alipoingia katika chumba cha hospitali ya Agha khan aliyokuwaelazwa kwa ajili
ya matibabu maneno hayo yalimshangaza sana mama yake aliyetegemea Reshmail
atakuwa na hasira ya kutendwa vile mbele ya hadhara
Nafsi
ilikuwa inamsuta sana mama reshmail,moyo uliomba msamaha lakini mdomo ulikuwa
mzito sana kufanya hivyo. Hali hiyo ilimkondesha sana na kumkosesha raha ndani
kwa ndani unene wake wa asili uliyafunika yote hayo na hakuna aliyejua jambo
zito alilobeba mama huyu.
Kweli
badala ya bwana na bibi Manyama kuegemea upande wa mashtaka ili mama Adam apewe
adhabu la wao waliunga mkono kwamba Reshmail alikuwa na makosa mahakama
ikatupilia mbali mashtaka hayo na mama Adam akawa huru,jambo hilo badala ya
kurudisha undugu liliongeza chuki na uadui
“si nilikwambia ukabisha?? Kama hawajamtoa
mwanetu kafara kwanini sasa wamekubali niachiwe huru??” mama Adam alimwambia
mumewe jambo ambalo wakati huu hata yeye alikubaliana nalo kuwa motto wao
mkubwa wa kiume(Adam) alitendwa vibaya na familia ya reshmail . kuamini kwa
mzee Michael baba yake Adam ni sawa na familia nzima kuamini kabisa na sumu ya
chuki ikamwingia kila mwanafamilia na kuwa aadui wakubwa wa familia ya mzee
Manyama.
-------------------------------------------------------------------------------------------
Siku mbili alizokaa pale hospitali hakuja hata
mwanafunzi mmoja kutoka pale chuoni kuja kutoa pole kwa Reshmail wote waliogopa
wakiamini alikuwa mshirikina . Eve hakukubaliana hata kwa mbali na shutuma hizo
kwani alimwamini sana Reshmail hivyo aliendelea kuwa pale hospitalini pamoja na
mchumba wake kumuuguza Reshmail ambaye alitoka siku tatu baadaye.
“baba mimi nitaenda na Eve kwake nitakaa siku
tano ndio nitakuja huko” Reshmail alimpa taarifa hiyo baba yake naye hakupinga
kwani amani aliyokuwa nayo Resh akiwa na Eve ilikuwa kubwa mno hali iliyowapa
faraja hata wazazi wake hivyo walimruhusu bila kusita.
Siku
hiyohiyo walipanda ndege kwa gharama za mchumba wa Eveline aitwaye Benjamin
Simon,kuelekea Iringa ambapo Eve alikuwa amepata ajira katika benki ya N.B.C
tawi la hapo.
Maisha yao
yalikuwa mazuri sana kwani Benny alikuwa mwalimu wa shule ya sekondari hivyo
katika majukumu waliweza kusaidiana na upendo wa dhati kati yao ulipendezesha
zaidi nyumba yao.Reshmail alivutiwa sana na maisha hayo na kumkumbuka sana Adam
wake “laiti angekuwepo tungeishi hivi siku moja “ alijiwazia Reshmail wakati
akiwaangalia Eve na Benny wakiwa kwenye kochi wamebebana kwa furaha huku
wakitaniana
Ilikuwa jioni moja
Reshmail na Eve wakiwa katika mizunguko ya hapa na pale mizunguko ambayo kwa
namna moja au nyingine iliibua ghafla safari ya kuingia sokoni,waliingia hapo
kununua matunda matunda,zilikuwa zimepita siku tano na tofauti na alivyowahaidi
wazazi wake hata hakuwa amefikiria kurudi Dar maisha ya Iringa yalikuwa
yamempendeza sana .
“Eveline ona eveline
jamani angalia kale katoto!!!” Reshmail alimgusagusa begani Eveline huku
akimwonyesha kikundi fulani cha watoto pale sokoni
“wewe achana hao machokoraa walionikwapua
pochi langu sina hamu nao hata kidogo,kisimu changu cha mchina na shilingi elfu
thelathini zikapotelea hewani looh!! Wabaya hao” aliongea kwa hasira Eve huku
akisitisha zoezi la kula chungwa aliliokuwa anafanya kwa wakati ule.
“mh!! Eve jamani achaga uongo yaani katoto
kama kale jamani hebu kaone kale kadogo “Reshmail alizidi kusisitiza lakini Eve
alionyesha bado ana uoga na uchungu moyoni wa kuibiwa vitu vyake na watoto
aliowaita machokoraa
“Reshmail shauri zako vitakuliza hivyo we
endelea kusema ni vitoto………..mh!! Resh lakini kale kadogo kazuri
kweli” aliongea Eve alipokaona kale katoto ambako Reshmail alisisitiza sana.
“toto zuri jamboo!!”
“sijambo shkamoo!!” kalijibu katoto kale kwa
uchangamfu sana baada ya Reshmail na Eve kukasogelea na kukasalimia.
“marahaba mtoto mzuri mbona upo hapa! Mwenyewe
au hawa ni kaka zako?” Resh alimuuliza
“a a sio kaka zangu mi namsubiri
mama ameondoka na watu wameenda huko amesema anarudi nimsubiri” alijibu tena
kwa sauti ya kitotototo
“umekula??” aliuliza Eve.
“looh!! Eve hujaacha tu maswali yako ya kichoyo
ya uchagani kwenu mh! Unataka aseme amekula ili umnyime au ?”
Reshmail alimshushua Eve kiutani
“mh! Limeniganda shoga,una mashushu
wewe!!” alijibu Eve kiaibuaibu huku akimpa yule mtoto
chungwa lililokwisha menywa tayari.
“mama anarudi saa ngapi??” Reshmail alimuuliza
yule mtoto tena
“sijui nimemsubiri hata hajaja amenipa chai tu
akaondoka na wale wanaume wawili” alijieleza vizuri motto yule
“mh!! Mjini mjini tu katoto kanajieleza
utadhani mtu mzima dah!” Eve alimnon’goneza Reshmail
“haya twende ukale eti motto mzuri!” Reshmail
alimwambia yule motto naye akakubali kwa ishara ya kichwa,akiwa pekupeku
akafuatana na Reshmail hadi kwenye mgahawa ulioandikwa “MAMA FRED MGAHAWA”
uliokuwa pembeni kidogo ya soko kuu la Iringa.
“utamsalimia mama eeh!!” baada ya kumnunulia
chakula walilipa na kumuaga
“haya mamdogo!” alijibu yule motto
“unaitwa nani vile”Eve akamuuliza
“naitwa Christian motto wa mama Bite” alijibu
na wote kwenye mgahawa wakacheka
Kuifananisha na picha ya Adam,dimplez za yule
mtoto zilimfananisha kabisa na Adam,achilia mbali rangi yake ya maji ya kunde
na ucheshi wake.
"Eve hapana,mbona kesho naenda kumtafuta Christian ili nimjue baba yake
anavyofanana,haiwezekani kufanana kwa kiasi hchi hapana "Aliongea Resh
huku akiifunika album ile . Eve alikubaliana naye na siku iliyofuata majira ya
saa nne,walikuwa katika hoteli ya yule mama ambapo walimwacha Christian.
"Nyie watoto ni kesi gani hyo mmetaka kuniachia jana" mama mnene
kiasi mmiliki wa mgahawa wa Mama Fred aliwapokea kwa maneno hayo makali huku
akifunga kanga yake vizuri kiunoni. Resh na Eve hawakuwa na jibu la kutoa
walidhani amewafananisha labda "Mama ni nini tena,mbona sisi...."
alijaribu kujieleza Eve huku akiishiwa maneno ya kujieleza.
"Mmenitekelezea mtoto hapa anaanza kunililia hapa usiku he! jamani mnataka
mniuwe kwa presha mkurya wa watu mie" aliongea kwa ghadhabu na mshangao
mkubwa sana yule mama.
"Mama sisi tumempata hapo sokoni,ndio kumleta hapa kwako kwa ajili ya
kupata chakula tu mama yangu" Reshmail alinyanyua mdomo wake na kuzungumza
kwa sauti iliyojaa mshangao pia.
"He! mauzauza gani haya jamani,mi nimempeleka pale kituo cha polisi usiku
uleuule ndugu
----------------------------------------------------------------------
Baridi kali ya Mbeya ilikuwa imemkataa motto
wa Bite (Christian) kwa hali hiyo alipotimiza miaka miwili waliondoka na kurudi
tena Iringa ambapo Bite alitaka kukaa kidogo halafu aende Mwanza kuweka makazi
mapya huko. Jambo la kushangaza licha ya baridi ya Iringa hali ya Christian
ilianza kuwa njema kama awali jambo lililosababisha Bite aendelee kukaa katika
mkoa huo.hadi anatimiza miaka mine hali yake kiafya ilikuwa njema sana na
tayari Bite alikuwa amesahau suala la kwenda Mwanza.akaanzisha genge la kuuza
uji na karanga mida ya jioni na mihogo ya kukaanga majira ya asubuhi. Ilikuwa
biashara ndogo lakini iliyomuingizia kipato kizuri tofauti na matarajio
yake.aliweza kupanga nyumba ya chumba kimoja na sebule aliyoishi na mwanae kwa
furaha sana tu bila masumbufu yoyote hadi siku hiyo asubuhi alipokuwa anauza
mihogo yake ambapo wanaume wawili ambao sura zao hazikuwa ngeni machoni pake
walipofika eneo la biashara yake.Aliwapokea kwa furaha sana na bashasha kama
wateja wengine aliozoeana nao.”Bite tukuone pembeni kidogo samahani lakini’
wawili wale walimvuta pembeni Bite
“mh! Mikopo asubuhi asubuhi hamna kwakweli
mtadhalilisha hizo suti zenu” aliongea Bite kwa utani huku akiwafata walipo
wawili hao
“funga biashara tunaondoka na ukithubutu
kupiga kelele au kukimbia nasambaratisha ubongo wako nadhani hujawahi kufikiria
kifo cha namna hiyo,hivyo basi fanya kama unavyoagizwa” aliambiwa Bite na wale
wanaume huku mmoja akifunua koti lake jeusi la suti na kumwonyesha Bite kitu
ambacho hakujiuliza mara mbili mbili kuwa ile ilikuwa ni Bunduki,kwa kuutambua
uoga alioupata Bite,yule mwenye bunduki alimbandika kitu mfano wa kishikizo cha
nguo na kumwambia “hiyo ni sound recorder nenda ukawaambie
wateja wako sisi ni ndugu zako tumekuletea taarifa za msiba nitakuwa
nakusikiliza hapa,ole wako nasema ole wako usifuate maelekezo” alipewa masharti
hayo ya uongo Bite ambaye laiti isingekuwa pensi yake ya jinsi ambayo huwa
anavaa kwa ndani ili kuhifadhia pesa zake za mauzo basi mkojo uliopenya bila
yeye kujua ungemwagika palepale hadharani na wala asingepatwa ma aibu yoyote ile.Kama
alivyoagizwa aliwaeleza wateja wake wawili waliokuwa wanamalizia kuitafuna
mihogo waliyokuwa wameinunua,wakampa pole za dhati . jasho lilikuwa linamtoka
alitamani kutumia ishara kuwaambia kwamba yupo katika hatari lakini alipowazia
mdomo wa bunduki alikaa kimya kabisa,bila kificho Bite aliiogopa sana bunduki
na hakupenda kumwacha Christian katika umri ule.Tayari akili ilisharudi nyuma
akatambua hasa,hao watu alikutana nao wapi,walikuwa ni baadhi
ya wafanyakazi katika ile ngome aliyekaa miaka miwili na ni
hao waliomleta Adam pale ngomeni “nimekwisha mimi Beatrice”
alijiwazia Bite huku akitetemeka.
Baada ya
kuifunga biashara yake aliwafuata akiwa na mwanae amemshikilia mkono.
“nadhani unajua hatuhitaji mtoto!!!
Tunakuhitaji wewe tena sasa hivi” aligombezwa Bite na bila kujijua akajikuta
akimwacha mwanae pale “Christian narudi sawa nisubirie pale sokoni sawa
mwanangu! “haya mama alijibu Christian kwa furaha kwani alijua amepata fursa
kubwa na ya kipekee kwenda kucheza na watoto wenzake pale mtaani
“ulidhani unaweza kutuzidi ujanja
sisi,umepotea sisi hatupimiki hata kidogo umeumia tena umeumia sana
aliambiwa Bite na wale wanaume wakiwa kwenye gari kuelekea kwenye gari kuelekea
kule katika ngome jambo hilo Bite hakulitamani hata kidogo,japo alimpata
Christian kwa bahati mbaya lakini alikuwa akimpenda sana kutoka moyoni na
hakuwa tayari kutenganishwa naye kwa namna yoyote ile.Alijiuliza maswali mengi
sana ni nani atakayempa chakula mwanaye siku hiyo na nyingine zitakazoendelea
wakati yeye hayupo,michezo ya kukimbizana aliyoipenda Chriss pia ilimtia hofu
Bite na kuhisi huenda mwanae anaweza kupoteza uhai wake kwa kugongwa na gari.
Funda la hasira lilimkaba kooni alitamani kufanya lolote lile wakati huo lile
jambo liwe ndoto kwake, machozi yaliyotoka ndio yaliyeyusha lile fundo japo
kidogo,hasira kali ilikuwa imemkaba Bite aliyekuwa amekaa siti ya nyuma na
jamaa mwenye Bunduki katika koti lake lakini maskini hakuwa na la kufanya hadi
gari lilipoingia ndani ya ngome ile
------------------------------------------------------------------------------------------
Macho ya Reshmail yalitawaliwa na taswira ya
yule mtoto Christian,zilikuwa ni siku nyingi zimepita tangu afungue album yake
kumwangalia mpenzi wake (Adam) aliyeaminika kuwa tayari ni marehemu.Ni katika
usiku huu alipokuwa akipitia album ya Eveline ndipo tena anakutana na picha ya
Adam ambayo yeye (Adam) alimpa Eveline walipoenda
Mwanza.”Eveline,Eveline,Eve……….huyu hapa ni nani???”
“we umechanganyikiwa tena eti hebu
acha mambo yake ya ajabu huyu Adam” Alijibu Eve kwa uoga.
“ na tuliyemwona leo kule sokoni ni nani??”
aliuliza Reshmail
“we Reshmail jamani wanafanana Mungu wangu
mbona wamefana hivyo lakini eeh!! Eve alijikuta picha ya mtoto Christian
ikiumbika kichwani mwake na
Zangu kwa sababu nimekaa naye hadi saa nne
tumemsubiri huyo mama yake aje wapi!! Nikaona isiwe shari ngoja nimpeleke
polisi penye usalama kuepuka balaa kumbe na nyie hamjui ni wa nani he!!” alitoa
maelezo hayo yule mama na kueleweka vyema kwa Reshmail na Eveline.
“hicho kituo cha polisi umesema kipo wapi?”
aliuliza Eve
“kile pale kinaonekana hata kwa hapa,lile
jingo la bluu nyuma yake” alielekeza yule mama
Ndani ya dakika tano tayari Reshmail na shoga
yake walikuwa mbele ya mapokezi ya kituo cha polisi Iringa mjini
,na walikuwa kwenye foleni wakisubiri zamu yao
ya kuhudumiwa ifike.
“nyie ni ndugu zake? Au mmoja wenu ndio mama
yake?”
“hapana sisi si ndugu zake ila……”aliishia
njiani katika maongezi yake Resh baada ya kukatishwa na yule askari “ila nini?
Yaani nyie wanawake wa siku hizi suala la kujali watoto wenu hamtaki kabisa
kulisikia mnachojali ni urembo tu wa sura zenu”
“jamani sio kwamba kuna ndugu yake hapa kati
yetu ila sisi tumemkuta jana kule sokoni ndio tumemnunulia chakula halafu
tukajiondokea zetu,leo hii ndio tunapita pale kwa mama Fred yule mwenye mgahawa
yeye ndiye ametupatia taarifa hiyo tukaona sio vibaya nasi tukifika kumwona
huyo motto” aliongea Eve aliyeonekana kutokuwa na hofu na kituo cha polisi
lakini Reshmail alikuwa ana uoga kwa mbali kama vile anatuhumiwa kwa lolote
lile.
“haya yupo tumemuhifadhi na tumepeleka taarifa
kwenye vyommbo vya habari wataanza kutangaza kama mama yake bahati
mbaya haya atakuja kumchukua na kama amemtelekeza akajiandae kwenda kuishi kwa
watoto yatima sisi hatuna uwezo wa kuhifadhi watu hapa zaidi ya mahabusu”
alijieleza askari yule huku akijipepea joto kwa kutumia kofia yake iliyochakaa
Majuma mawili yalipita bila mama wala ndugu wa
motto kupatikana licha ya kituo cha redio maarufu mjini iringa cha Ebon fm
kutangaza kila siku bila kukoma
“eve naenda kumchukua yule motto nafsi yangu
inanishauri hivyo na ni lazima nifate ambacho nafsi yangu inaniamuru” Reshmail
alimwambia Eve siku moja wakiwa wamekaa sebuleni wakiangalia habari katika
luninga.Eve alikuwa amejenga tabia ya kutobishana na rafki yake huyo kwani
furaha yake ilikuwa ni kumwona Reshmail akiwa na furaha tele
“lakini Resh,mama yake si atamtafuta ssana??”
“Eve yaani imetangazwa hivyo redioni na
hajajitokeza leo hii mie tu kumchukua ndipo ajitokeze? Looh! Acha nae ahangaike
kidogo” alijibu Reshmail kwa jeuri
“mh! Haya sikuwezi mwanasheria wangu”
Polisi hapakuwa na usumbufu ni wazi kwamba
walikuwa wamechoshwa na matukio ya watoto kutelekezwa na wazazi wao pasipo
sababu zilizo wazi,hivyo kitendo cha Resmail kuamua kumchukua Christian ilikuwa
ahueni kwao.aliandiokishwa maelezo mafupi tu kabla ya kuruhusiwa kondoka na
mtoto ambaye alikuwa dhaifu tayari kutokana na lishe duni na upweke wa
kutomuona mama yake kwa siku hizo zote.
Reshmail alikuwa
ameyafurahia sana maisha ya Iringa,kampani kubwa kutoka Eveline na mchumba wake
ilibeba nusu ya furaha yake huku nusu nyingine ikikamilishwa na uwepo wa
Christian mikononi mwake,mara kwa mara alipenda kuwa naye karibu huku akimwita
mume wako jambo lililompa faraja kubwa moyoni
”Eve jamani nitakumiss kipenzi changu lakini nitarudi tena asanteni sana kwa
ukarimu wenu mlionionyesha tangu mwanzo nimeishi kwa furaha kubwa sana hapa”
Reshmail aliyazungumza hayo alipokuwa anawaaga Eve na Benny usiku ambapo kesho
yake alitegemea kurejea Dar-es-salaam akiwa ameandamana na Christian mtoto
aliyempata katika mazingira ya kutatanisha
Kwa Christian safari ya kutoka Iringa kwenda
Dar ilikuwa safari yake ya kwanza ndefu zaidi kuwahi kusafiri
Siku iloyofuata wawili hawa walikuwa ndani ya
basi la ‘budget’ litokalo Mbeya kwenda Dar likipitia Iringa.
“Mama alisema baba yupo pale kwenye ile
nyumba, tushuke nikamsalimie!” Chriss aliongea hayo huku akielekezea kidole
chake kwenye jingo lililoonekana kwa mbali mno kutokea pale barabarani na
hapakuwa na dalili ya kuishi mtu pale hivyo Reshmail akachukulia kuwa ni akili
ya utoto imemtuma Chriss kuzungumza akaamua kupuuzia
“chriss alikwambia nani we muongo!!”
“alinambia mama siku moja hivi tulipita hapa
,halafu mama alinikataza kusema uongo ni dhambi” alijieleza Christian haraka
haraka
“mh! Haya tutakiuja siku nyingine sawa mfalme
wangu” Reshmail alimjibu Chriss ili kumlidhisha kwa aliyokuwa anasema
------------------------------------------------------------------------------------
Nyumba tulivu kabisa ya mh.Manyama ililipuka
kwa furaha kwa kurejea kwa Reshmail akiwa mwenye furaha tele “umetuletea na
mjukuu!!” alitania mama Resh.”mtoto wa Eve huyu anamwita mama mdogo” Resh naye
akdanganya “kazuri kweli kama………………” alisita kumalizia baba yake “ni kama Adam
baba usiogope kufananisha wamefanana kweli” alimtoa baba yake wasiwasi huku
akimkumbatia baba yake kasha mama yake.
“mh!! Tulikuwa wapweke kweli jamani dada”
msaidizi wa kazi za ndani aliyeitwa Fatuma alimwambia Reshmail huku
akimkumbatia na kumbusu shavuni
“na huyo mtoto kama mwanao vile hebu kaone”
aliendelea Fatuma
“sio kama wa kwangu ila ni wa kwangu humwoni
alivyonifanana?” alijibu kimzaha na wote wakacheka kwa pamoja
------------------------------------------------------------------------------------
Hali ya sintofahamu iliwakumba wale
wafanyakazi wa lile jumba (ngomeni) alipokuwa anatunzwa Adam. Mkuu wa ngome
hiyo bwana Lwebe alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila mbua alikuwa na
ghadhabu kubwa sana,kila kitu kilikuwa shaghala baghala kila mara aliongea
kwenye simu hukuakitoa vitisho vikali sana na hata kutishia kuua. Wafanyakazi
hawakumwelewa lolote walizitambua hasira za bosi wao huyo ambaye mara chache
anazokuwa katika hali kama hiyo humalizia hasira zake kwa kutoa roho ya mtu
“mlete Adam hapa mara moja !!” aliamrisha huku
akijikuna ndevu zake kwa kutumia mdomo wa bunduki aliyokuwa nayo
“maskini Adam sijui amekosa nini” alijiuliza
aliyekuwa anaenda kumwita. Bila wasiwasi wowote Adam akamfikia Lwebe D kwa
ishara ya mkono akamwamrisha kumfuata,pamoja na mabaunsa wawili waliotinga suti
nyeusi . lwebe hakuongea neno lolote hadi walipofika kwa nje,tayari kigiza cha
saa mbili kilikuwa kimetawala
“mlete na yule mwingine wa nyumba ya chini”
alitoa amri nyingine tena baada ya tano walioagizwa wakarejea na mtu mwingine
“we kinyamkera una bahati sana aliyekuleta
hapa amesema haujasambaza taarifa zozote mbaya laiti kama ungethubutu
ningeiondoa shingo yako sasa hivi. Nakuacha uende tena lakini tambua mtandao
wangu upo popote katika nchi hii sasa ole wako uthubutu kunyanyua mdomo wako
kutangaza ujinga” aliambiwa yule binti aliyeletwa pale huku akionyeshwa njia ya
kutokea
“we kidume kwa jeuri ya bosi wako kujaribu
kunidhurumu pesa yangu wakati wewe unakula na kulala bure hapa;lazima
nimwonyeshe mimi ni nani na ni wewe utakayeumia” aliongea Lwebe huku akipuliza
moshi wa sigara hewani.
----------------------------------------------------------------------------------
Ilikuwa ni mwezi mmoja tangu Bite arejeshwe
kwenye ile ngome lakini katika chumba kingine,hakuwa msaidizi wa kazi tena bali
mtuhumiwa na hakupata fursa ya kuonana na Adam hata siku moja . siku
alipotolewa nje usiku na kwa mahesabu ya miaka mitano ambayo Adam angekaa pale
machale yalimcheza,alivyopewa uhuru wa kuondoka hakwenda mbali sana alifika
eneo moja kwenye mtaro na kuanza kusubiria ni nini kitatokea japo hakusikia
vizuri maneno lakini alisubiri hata vitendo
Mkataba wa miaka
mitano alioandikishana Bi.gaudensia na Lwebe wa Adam kuhifadhiwa pale ulikuwa
umeisha tayari na miezi mitatu zaidi ilikuwa imepita,suala hilo la kuchelewesha
pesa lilimkera sana Lwebe na pia ahadi za uongo kutoka kwa Gaudencia
zilichochea sana hasira za Lwebe kufikia hatua ya kuamua kuzipooza kwa huyo
Adam aliyehifadhiwa hapo.ni usiku huo alipoamua kwa mkono wake mwenyewe Adam
duniani kama kisasi kwa Bi.Gaudensia
“paa!! Paa!!” mlio mkali wa risasi ulisikika
na kumzindua Bite ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi pale kwenye mtalo,kidogo
apige kelele lakini viganja vya mkono wake vikawahi kuuziba haraka sana.
Hakusikia hata chembe ya kilio na baada ya dakika kama saba akasikia milango
imefungwa
Kwa ujasiri na tahadhari kubwa Bite
akajisogeza hadi karibu kabisa na eneo ambalo aliamini hakika ndipo mlio wa
risasi umetokea huku kichwani kwake akiwa ana jibu la “nimesahau saa yangu”
iwapo atakutana au kushtukiwa na mlinzi,kwa hofu alizurura katika lile eneo
dakika tatu bila kuona chochoten”au wameingia nae ndani??” alijiuliza bila
kupata jibu
“koh!! Koh!! Alishtuliwa na sauti
ya kikohozi nyuma yake,mawazo yake alidhania ni mlinzi eneo lile lakini
alipogeukz hakuwa mlinzi tena ni mwili wa binadamu ukiwa chini,hakutambua mara
moja yule ni nani hadi macho yake yalipolizoea giza la pale “Adam!!!!!”
“we ni nani??” alijibiwa kwa sauti ya chini
sana iliyokuwa inaunguruma kama mnyama anayechinjwa
“Bite mimi jamani Adam”
“ondoka watakuua hao Bite ondoka niache mi
nife hapa” alijibu Adam
“hapana Adam usife,usife Adam twende
tukamtafute mwanetu Chrstian anatamani sana kukuona,usife Adam tafadhali” Bite
alibembeleza
Risasi mbili
zilizopenya katika paja lake la kulia zilikuwa zimemsababishia Adam kuvuja sana
damu na mbele yake alichokitarajia ni kifo hakuna kinginelakini maneno ya Bite
nguvu zilirejea upya kabisa tena kwa kasi”Bite ulijifungua,mtoto wangu yuko
wapi? Ni wa kiume au wa kike?” alihoji maswali mfululizo Adam huku akijitutumua
kusimama kwa nguvu alizokuwa amezipata
“ni stori ndefu na hapa sio mahali pake tuondoke
tafadhali jitahidi kuna hatari kubwa kama unampenda mwanao jitahidi tuondoke”
aliongea Bite huku akiuweka mkono wa Adam katika bega lake na kuanza
kumkongoja kutoka eneo lile huku (Adam) akitumia mguu mmoja na ule uliojeruhiwa
ukiwa juu juu.kutoka pale walipokuwa hadi barabarani haukuwa umbali mrefu sana
na walifanikiwa kufika,kwa giza nene lililokuwepo hawakuweza kuonekana na mtu
yeyote,nguvu zilikuwa zinamwishia Adam kutokana na kuvuja damu lakini alijikaza
kijasiri sana na kuendelea mbele
-------------------------------------------------------------------------------
Lwebe na kundi lake baada ya kumpiga
risasi mbili Adam waliamini katu asingeweza kunyanyuka kutoka katika
eneo lile,na hata angeweza kuinuka hakuwa na pa kwenda hakuujua mkoa huo hata
kidogo. Waliingia ndani na kupiga simu kwa Bi.Gaudensia kwamba mtu wake tayari
ana risasi mbili mwilini
“msimuue jamani,tafadhali sana kesho naileta
pesa yenu mapema kabisa”
“nimechoshwa na ahadi zako mheshimiwa jiandae
kuchukua maiti yako siku yoyote utakayotaka utaikuta nimeihifadhi na kama na
kuizika nitakusaidia” alijibu kwa ghadhabu kasha akakata simu
Bi Gaudencia akapiga tena
“nakusikiliza”
“basi nielewe kwa leo na hili ni ombi la
mwisho tafadhali usimuue kesho asubuhi sana nakuja huko,ninaondoka huku saa
nane usiku tafadhali” alibembeleza
“na iwe hivyo atalala nje leo na hata kula
hadi utakapokuja
“sawa mkurugenzi” alijibu kwa unyenyekevu
Gaudensia
Akini ya Bi.Gaudensia ilifanya kazi
haraka haraka akapekua kila kona katika chumba anacholala na mumewe na kwa
bahati nzuri kwa akakutana na kadi ya benki ya mume wake ambayo alikuwa
akifahamu vizuri kabisa namba zake za siri. Bila kupoteza muda akampigia dereva
wake wa siri ambaye huwa anampeleka Iringa naye haraka haraka bila kuhoji
akatii amri aliyopewa.bila Reshmail kujua Bi.Gaudensia akaondoka majira saa
saba usiku,nafsi ilikuwa ikimuhukumu juu ya baya lolote litakalomkuta Adam
“damu ya Adam ipo juu yangu”
“naenda kwa rafiki yangu ameugua ghafla “ mama
Reshmail alimuaga mlinzi wa getini
“sawa bosi” alijibu mzee yule wa makamo huku
akifunga geti baada ya mama kuwa ametoka nje
Kwa kasi ya ajabu gari iliondoka jijini
Dar-es-salaam kwa kuwa ilikuwa usiku sana vizingiti vya watu wa usalama pamoja
na foleni havikuwepo sana hivyo dereva alikimbiza gari kwa kadri ya
uwezo wake. Breki ya kwanza ilikuwa ni katika benki ya C.R.D.B maeneo ya Ubungo
ambapo mama Reshmail alishuka na kuvuta pesa kutoka katika akaunti ya akiba ya
mzee Manyama
Badala ya masaa matano kwa gari binafsi kufika
Iringa walitumia masaa matatu pekee
“mh!! Huku napo kijijini kweli huyo nae sijui
ni mgonjwa sasa usiku huu atapata wapi lifti ya gari” mama Reshmail alimwambia
dereva wake alipoona watu wawili wakisimamisha gari
“ah!! Ndo maisha ya Tanzania yalivyo” alijibu
dereva huku akiongeza zaidi mwendo wa gari hadi wakaifikia ngome ya vigogo
waliyokuwa wakiifua
---------------------------------------------------------------------------
Magari makubwa ya mizigo yatokayo Morogoro
kwenda Zambia na Malawi ndiyo yaliyotoa msaada kwa Bite na Adam ambapo Bite
alijitambulisha kama mke wa Adam na kwamba wamevamiwa na majambazi na mumewe
(Adam) amepigwa risasi. Laiti kama madereva wangekuwa watanzania kwa jinsi
walivyo waoga katu wasingewapandisha wawili hawa lakini wakongomani wale ambao
vita kwao ni jambo la kawaida waliwachukua Adam na Bite hadi Iringa mjini
walipowaacha jirani kabisa na hospitali ya rufaa.
“bila RB hatupokei mgonjwa wa aina hii”
alisema muuguzi wa kike wa hospitali ile wakati Bite anajieleza.ni kweli yule
muuguzi(nesi) alikuwa na haki zote za kupingana na ujio ule kwani hali
aliyokuwa nayo Adam ilihitaji taarifa za polisi kwanza
“haa!!! Mama Christian,ni wewe hata siamini au
nakufananisha?” wakati Bite akijiegemeza kwenye ukuta huku akiwa amekata tama
alishangaa kutambulika kwake na nesi yule
“Mungu wangu mama wawili jamani!!!” baada ya
kumkazia macho naye Bite akamtambua yule nesi kuwa waliwahi kufanya nae
biashara katika soko la Uyole Mbeya na pia alikuwa jirani yake pale alipokuwa
anaishi,ulikuwa mshangao mkubwa sana
“ehe!! Kulikoni tena ndugu yangu yamekukuta
yapi tena mwenzangu?” alihoji nesi huku akiwa amechangamka sana safari hii
“ni makubwa sana,lakini ningeupata msaada wako
kwanza kwa mume wangu ndio tungeongea vizuri shoga” alijibu Bite akiwa na
matumaini tele
“ondoa shaka shoga huduma mnaipata sasa hivi
tena huduma bora,daktari tunaheshimiana naye sana na pia ni shemeji yangu” nesi
aliongea hayo huku wakisaidiana kumwingiza Adam ndani ya chumba cha
wagonjwa,hapakuwa na maswali mengi,undugu ulitawala pale. Adam akafanyiwa upasuaji
mdogo wa kuondoa risasi katika ambao haukuchukua hata hata nusu saa damu na
maji pia vikaongezwa katika mwili wake uliokuwa dhaifu sana.kufikia majira ya
saa kumi na moja alfajiri Adam alikuwa amepata nafuu kubwa na aliweza kutembea
japo kwa kuchechemea
“shoga nikueleze wazi tu kwamba sisi pa
kufikia hapa Iringa mimi na mume wangu hatuna! Tangu niondoke ghafla niliacha
sijalipa kodi nina uhakika chumba sio changu tena kwa hiyo pa kwenda hatujui”
Bite alimweleza hayo mama wawili baada ya kuwa amemsogeza pembeni ili mtu
mwingine asiweze kusikia
“ondoa shaka Bite miim kwangu pana nyumba
kubwa tu!! Nimejengewa na mnyakyusa mmoja,nimemweka kwenye kiganja kwangu mimi
hasikii,haoni wala hasemi,ni kaka yake na huyu daktari we mwenyewe si umeona
alivyowashughulikia haraka” kwa sauti ya chini kabisa nesi alijibu
Wote watatu
katika teksi wakaongozana hadi nyumbani kwa nesi ni kweli nesi hakuwa na chembe
ya utani hata kidogo nyumba ile ilikuwa kubwa sana na haikuwa haki
kukaliwa na watu wawili pekee vilikuwa ni vyumba sita pamoja na sebule
“karibuni! Karibuni sana! Nesi aliwakaribisha
walipofika nyumbani kwake.
“asante sana ndugu yangu ama kweli ishi na
watu uvae viatu” alisema Bite kwa upole sana
“usijali Bite tumeishi vizuri,hatukuwahi
kugombana hata siku moja,tumetwishana matenga ya nyanya kwa nini sasa nishindwe
kukutendea wema!!!” nesi alimtoa hofu Bite
Chumba walichopewa kilikuwa kikubwa cha
kuwatosha kabisa,kitanda cha tano kwa sita kilikuwa saizi yao kabisa. Adam
alishangazwa sana na wema huo wa nesi lakini mshango wake uliongezeka maradufu
baada ya kukutana na mume wa nesi siku ambayo walikuwa wakitambulishwa kwake
kama shemeji zake yaani ndugu zake Bite.mzee huyu wa kinyakyusa aliyeitwa
Gwakisa ni kama heshima ilipitiliza na kuwa kama anawanyenyekea wawili hawa.
Adam alihudumiwa na yule daktari kana kwamba alikuwa ni mgonjwa wa kisukari au
alikuwa ni mtoto wa mfalme,Adam alipata farijiko kubwa sana kuishi pale
Bite kama kawaida alikuwa mwanamke wa
kujituma sana,ndani ya wiki moja tayari alikuwa amepata kazi ya ndani
katika nyumba nzuri waliyoishi wanafamilia watatu,mwanaume na mke pamoja na
mtoto wa kama miaka mitatu wa kike aliyekuwa anasoma shule ya awali
-------------------------------------------------------------------
“bite mama!!”
“bee mama”
“mpeleke mtoto shule halafu baadaye mpeleke
pale zahanati akapimwe jana usiku amekohoa sana” ilikuwa sauti ya Eveline
akimpa maelekezo Bite ambaye alikuwa mfanyakazi wake mpya na wa kwanza wa ndani
ya nyumba yake na mchumba wake. Ratiba ya Bite ilikuwa ni kazi kuanzia asubuhi
ya saa mbili ambapo alikuwa akimpeleka Loyce {mtoto wa kaka yake Benny} shuleni
na kisha akirejea anaandaa chakula cha mchana kwa siku ambayo Benny hurudi
nyumbani mchana na baada ya hapo humfuata Loyce shuleni,kisha maandalizi
ya chakula cha jioni na majira ya saa kumi na mbili huaga na kuondoka,ilikuwa
kazi ambayo haikumtoa jasho Bite na malipo ya shilingi laki moja kila mwezi
yalimtosheleza kabisa kupanga chumba kidogo walicholipia shilingi 15000 kwa
mwezi
“tunashukuru sana kwa ukarimu wenu bwana na
bibi Gwakisa Mungu awazidishie baraka katika kazi zenu” alitoa shukrani za
dhati Adam kwa niaba ya mke wake wa bandia (Bite).uchangamfu wake na wingi wa
vituko ulifanya nyumba ya Gwakisa iwe iwe yenye shangwe na tabasamu kila
siku,kitendo chake cha kuaga pale kilimsononesha Gwakisa na mkewe lakini
hawakuwa na jinsi,kutoka mfukoni mwake aliwakabidhi shilingi laki mbili za
kuanzia maisha yao huko waendako
Tayari Adam alianza kumpenda kwa dhati Bite
uchapakazi wake na jinsi alivyomwokoa kutoka katika kifo ulichangia sana lakini
kiunganishi cha mtoto Christian ndio ilikuwa chachu kubwa ya mapenzi
yao.walivyohama katika nyumba yao ya kupanga walianza rasmi kuishi maisha ya
mke na mume Adam hakuwa na amani hata kidogo na familia ya Reshmail hasa baada
ya kukuta katika nyumba hiyo ndogo waliyohamia magazeti
yaliyobandikwa kama mapambo likisema “imani za kishirikina zamwondoa mheshimiwa
Manyama bungeni” alitamani sana kuisoma habari hiyo kiundani iliyotoka
takribani miaka mitano iliyopita lakini ilikuwa imeandikwa inaendelea ukurasa
wa pili anbao haukuwepo pale ukutani
“au walikuwa wanataka kunitoa kafara? Mungu
wangu!! Niliwakosea nini mimi” alijiuliza Adam wakati wakiingiza yao ya Rambo
ndani ya chumba hicho kimoja kilichotenganishwa na pazia kufanya sebule na
chumba
Hisi hizo mbaya zikamfanya Adam aamue
kuanzisha rasmi uhusiano na mwanamke ambaye amezaa naye mtoto pia aliyeokoa
maisha yake bila kutarajia mwanamke ambaye hajawahi kumkwaza,mwanamke mpiganaji
anayempa furaha tele kila siku
“Bite nataka uwe mke wangu”
“Mh!! Niwe mkeo mara ngapi mimi
mkeo tayari jamani” alijibu Bite huku akichezea ndevu za Adam ikiwa ni siku ya
pili tu tangia wahamie katika makazi hayo mapya
“una utani wewe mbona ulikuwa hujaniambia wala
sijawahi kusikia ukiniita mume wako?
“sio lazima nikwambie tayari nina mtoto wako
halafu humu ndani kuna kitanda kimoja tena kidogo tu,ulidhani chako
mwenyewe!!!” aliuliza Bite kisha wote wakacheka huku wakikumbatiana na
kuangukia kitandani
-----------------------------------------------------------------------------------------
Maisha ya Reshmail jijini Dar-es-salaam
yalikuwa yamebadilika sana akiwa anasubiri wakati baba yake akimtafutia kazi
itakayompendeza alifurahia mara zote na Christian huku akiwa amewabadili watu
wote wanaomfahamu kwa ukaribu kutokea kumwita Reshmail na sasa walimwita mama
Christian na alikuwa amejivika pete ya ndoa katika kidole chake cha
shahada ikwa na jina Adam na nyingine ndogo akiwa amemvisha Christian ikiwa
imeandikwa Reshmail.
Hakuwa mtu wa kulialia tena wala msongo wa
mawazo haukumsumbua tena aliamini nafasi ya Adam ilikuwa imezibwa vyema na
Christian ambaye alikuwa Adam mpya kwake. Walilala wote,walicheza wote na
kusimuliana mambo mbalimbali.alipoenda kusalimia rafiki zake walienda wote
Christian mkono wa kulia. Harakaharaka Christian alijikuta akimpenda mno
Reshmail kuliko hata ilivyokuwa kwa mama yake mzazi,maisha ya kifahari ya kwao
Reshmail yalimfanya Christian anawiri sana ungewakuta wakicheza bustanini kama
vile wanalingana umri walibembea pamoja na kupigana kiuongouongo,kwa ufupi
waliishi maisha ya kusisimua kwa kila aliyewaona. Akiugua Reshmail ni Christian
atamuuguza kwa kukaa pembeni yake bila kutoka nje hadi apone hivyo hivyo kwa
Reshmail abaye alimwogesha na kumlisha. Wakati huo Reshmail ndio alikuwa
mwalimu wa Christian akimfundisha kusoma na kuandika jambo ambalo hata baba
yake alilipenda na Christian alikuwa mtu anayeelewa haraka akifundishwa
,reshmail alifurahia sana.
Baada ya kukaa na Christian mwezi sita
reshmail kwa mara nyingine Iringa kwa rafiki yake jambo kubwa lililompeleka
huko ni harusi ya rafiki yahe huyo ambapo alitarajiwa kuwa matron wa kipenzi
chake hicho.
“shoga shughuli kesho kutwa hata haujaonekana
jamani au ndio mambo yetu yale haja ya kufanyiwa make up….”aliuliza kiutsni .Eve
katika simu alipokuwa anaongea na Reshmail.
“Kesho asubuhi na mapema nakujua ,mume wangu
alikuwa na mafua ndio tatizo si unajua tena.”alijibu Reshmail.
Haya mume huyo anavyoringiwa shauriro “alijibu
Eve .Christian alikuwa amependekezwa kuwa bwana harusi mdogo pamoja na
Loyce (mtoto wa kaka yake Benny).
“He unatoka mume wangu asiuze sura,na jinsi
alivyoandaliwa huku Dar es salaam ,utachoka mwenyewe na simtoi mpaka
siku ya shughuli,atakayeruhusiwa kumuona ni bibi harusi mdogo(Loyce) peke yake
wakati wa kujifunza,sitaki mwingine amuone mpaka siku yenyewe”alijibu Reshmail
kwa furaha.
“Haya umeshindwa ambao hatuna waume
tunalo,alijibu Eve kisha wakaagana.
Asubuhi ya siku iliyofuata majira ya saa nne
asubuhi tayari Reshmail,Christian,mpambaji pamoja na dereva walikuwa ndani ya
gari la baba yake (Resh)taratibu safari ya Iringa ikaanza.
“Usitupeleke kwa kasi sawa eeh,alitoa malekezo
Reshmail na kukubaliwa na dereva kwa sababu hawakuwa na haraka yeyote ila mbele
yao yalikuwa bado masaa mengi sana kabla ya harusi kufanyika.
Kwa mwendo wa kinyonga kabisa gar lilifika
mbele ya nyumba ya Eve majira ya saa nne usiku na hakuna aliyekuwa ameschoka
sana.Shamrashamra zilikuwa kubwa sana maeneo ya pale kwa Eve kelele zilizidi
alipofika Reshmail, na kama alivyoaahidi kweli alishuka yeye peke yake kutoka
katika gari akifuatiwa na dereva,urembo wake utadhani alikuwa amepembwa tayari
kuingia ukumbini.
“Shoga tabia gain hiyo kupendeza
kuliko bibi harusi?”aliuliza eve kiutani baada ya Reshmail kuingia katika
chumba ambacho Eve alikuwa amehifadhiwa akiwa na wapambaji wake.
“Hebu acha utani wako,kila mara
unadhani tuko shuleni?mwone,”alijibu Reshmail,Eve akajiziba mdomo
kwa aibu huku akiwatazama wapambaji wake waliokuwa wamejizuia kucheka lakini
uvumulivu ukawashinda wakacheka kwa nguvu.
Chumba kile kikageuka kijiwa cha story kati ya
Reshmail na Eve ,stori zingine zilikuwa juu ya mume wa Reshmail
(Christian),shoga hadi pete?
“Sina utani mie mbona”?alijibu Resh huku
wapambaji wakiwa hawajui hata kinachoongelewa.
“Mama kuna mtu anataka kukuona,ilikuwa ni
sauti ya kike ikimueleza Eve.
“Heh!!ushazaa na wewe?”aliuliza kiutani
Reshmail.Mh!!niringe huyu ni msaidizi wangu tu wa kazi anaitwa Bite,nampenda
naye ananipenda pia.
“Sio kama mimi na Christian “alidakia Reshmail
ambaye tangu aingie chumba kilitawaliwa na vicheko.
“Bite humuwezi huyu anaitwa mam Christian ni
rafiki yangu tangu utotoni.
“Nafurahi kukufahamu mama Christian hata
mimi.alitaka kuondelea kuongea Bite akakatishwa na Eve.”Anayetaka kuniona nani
huyo tena?,mwambie nina mgeni Bite akajiondokea bila kumalizia kauli yake.
Sherehe ilifana kuanzi kanisani lakini mambo
yote yalikuwa saa mbili usiku maharusi wadogo walipokuwa wametangulia mbele
wakifuatiwa na wana ndoa wenyewe(Eveline na Benjamin)huku nyuma yao Reshmail na
Fredrick wakifunika kila kitu kwa pale mbele Christian aliteka macho ya watu
huku kamera zimemulika yeye. Tabasamu lake pana la wakati wote lililoonyesha
vishimo katika mashavu yake yote lilisababisha watu wengine wahisi huenda
sio kutoka Tanzania , suti yake iliyoendana kabisa na mwili wake na viatu
vyake pia jinsi mkono wake ulivyokuwa umemshika kiustadi Loyce (bi
harusi mdogo) ulimfanya MC ashindwe kukaa kimya “nani mwenyewe harusi,wa
mbele,nyuma au kati” aliuliza kwa mbwembwe
“mbeleeeeeeeee!!!.......nyumaaaaa!!!!” ndio
majibu yaliyosikika kutoka kwa wengi
“hayaa wageni waalikwa wanasema maharusi wa
katikati wamefunika sana” alidanganya MC aliyefahamu wazi Christian na Reshmail
wameteka macho ya watu wengi pengine kuliko maharusi wenyewe.
Picha zilipigwa kwa wingi lakini
Christian hakuonyesha wasiwasi wowote “mh!! Katoto kazuri halafu kajanja hako”
wanawake walikuwa wakinon’gonezana huku wakimtazama Christian anavyozidi
kusonga mbele
“wamekatoa nje,baba yake ni mreno” alidakia
mama aliyesifika kwa umbea pale mtaani aliyejulikana zaidi kwa jina la mama
mwingi.hata hawakuhangaika kujibishana nae kwani walishamzoea
Taratibu kabisa kwa mwendo
wa kunyata jozi hizi tatu za kuvutia ziligawanyika huku jozi mbili za wakubwa
zikienda katika meza kubwa kabisa na watoto wakienda katika meza yao ndogo
iliyokuwa akimeremeta soda na vinywaji vingine baridi,”kusema ukweli sherehe
imependeza,siongei kama MC bali kama ndugu Kidagaa Peter Kubalunga wengi
wananiita MC K.P” alichombeza Msema Chochote (MC) na kushangiliwa sana na umati
mkubwa uliohudhuria sherehe hiyo.
-------------------------------------------------------------------------------
“dah!! Umependeza kweli sitaibiwa huko na
wajanja,hebu ona ona mgongo wako utadhani huna mamba ulivyopendeza,ona kifua
chako mpenzi wangu hapana nitaibiwa mke mie” Adam alikuwa akimtania Bite huku
akim funga zipu yake ya mgongoni
“acha wivu mwanaume wewe,kaa ndani usubirie ya
kwako aniibe nani wataishia kutamani tu!!” alijibu Bite huku akimun’gunya
midomo yake ili lipstick aliyopakaa ikae vizuri zaidi na kioo kikiwa mbele yake
“nakupenda sana mke wangu,tambua hilo niliamua
toka moyoni mwangu na wala sijutii hata kidogo najionamwenye bahati sana” Adam
kwa sauti ya chini iliyomaanisha anachokisema alimwambia Bite ambaye alitulia
tuli akamtazama Adam kisha akamkumbatia na kumbusu.
“nakupenda pia nakupenda sana” Bite akamwambia
Adam halafu akatoka nje na kupanda teksi iliyokuwa inamsubiri kwa nje na
kuondoka,Adam hakuthubutu kutoa hata pua yake nje kwani bado alikuwa na uoga wa
kurejea mikononi mwa watu wabaya
Majira ya saa tatu na nusu Bite tayari alikuwa
mlangoni akionyesha kadi yake ya mwaliko kwa watu wa ulinzi kisha mwanadada
kutoka kamati ya maandalizi akamwongoza Bite kuelekea katika upande ambao ndugu
zake na mwanamke walikuwa wamekaa,eneo la chini ya meza ya bwana na bibi harusi
mdogo.Bite alikuwa tayari kama ndugu wa damu kwa Eveline walitokea kuheshimiana
sana na hawakuwahi kuingia katika malumbano makubwa sana.
Amani ilitoweka katika
meza ya bwana na bibi harusi wadogo,Christian alikuwa amekosa utulivu mara kwa
mara alikuwa ananyanyua shingo yake aweze kuona kitu Fulani ambacho hakuna
aliyefahamu ni nini kimemsibu
“au kanaumwa tumbo?” alijiuliza matron huku
akienda kwenye ile meza kumsikiliza Chriss ana shida gain
“Chriss ni nini baba umekuwaje?” alimuuliza
baada ya kumfikia
“nataka kwenda kwa mama” alijibu kwa sauti
iliyojaa manun’guniko sana
“subiri kidogo mtoto mzuri nitakupeleka sawa”
matron alimdanganya Chriss huku akiamini shida yake ilikuwa kwenda kwa
Reshmail,kidogo Chriss alitulia japo bado hakuwa na katika hali ya uchangamfu
kama awali
Muda wa kutoa zawadi ulipofika
maharusi wote katika jozi tatu walitakiwa kuwa mbele ya umati kwa ajili ya
kupokea zawadi zao.Christian na Loyce waliwekewa viti wakakaa wakati
Eve,Benny,Reshmail na Fredrick walisimama wima kupokea heshima hizo
“he! We mtoto vipi? Jamani huyu mtoto
kulikoni” yule mwanamke aliuliza baada ya kushikwa gauni lake na
Christian alipotaka kuondoka baaba ya kutoa zawadi. Bahati mbaya muziki ulikuwa
umezimwa hivyo ukumbi mzima ulishuhudia tukio hili la kushangaza
“mamaaaa!! Mamaaaa!!” Chriss
alimpigia kelele alipotaka kuondoka
“Chriss…….Christian……Christian wanguuuu!!!
Jamani ni mwanangu..ni mwanangu huyu” alipiga kelele mwanamke huyu,alikuwa ni
Bite na tayari akili yake imemgundu Christian,watu wote waliamini
amechanganyikiwa lakini alikuwa anasisitiza bado kwa maneno hayohayo. Hakika
mbele yake alikuwepo mwanaye waliyepotezana zaidi ya nusu mwaka sasa na dalili
za kumpata zilikuwa zimeanza kufifia. Mayowe yake yalivyozidi yakapoteza
usikivu pale ukumbini na kila mtu kuanza kujiuliza kulikoni eneo lile
“mama mama mama,huyu ni mwanangu…..Christian
jamani” Bite kwa sauti ya juu sana akaanza kumwambia Eveline ambaye alikuwa
amekodoa macho kuangalia anachofanya Bite pale mbele
“kuna nini jamani” Reshmail alishindwa
kujiuliza akamvagaa Eve na kumuuliza
“huyu ni Christian,mtoto wangu jamani mtoto
wangu kabisa” alisisitiza Bite. Nguvu zilimwisha Reshmail japokuwa hakuzimia
lakini alianguka chini,alishuhudia kila kitu lakini hakuweza kuzungumza,ulikuwa
mshtuko wa hali ya juu sana haikuwa sherehe tena bali kasheshe,huku Bite na
mayowe yake huku Reshmail akiwa chini. Wapiga picha hawakuwa mbali walilichukua
hili tukio kikamilifu tayari kwa kuuza katika vyombo vya habari.
Mwanamama mwenye nguo nyeusi
alikuwa anapambana kupenya katika msitu mkubwa wa watu pale ukumbini,mwanzoni
hakuwemo kwenye sherehe “vimama vya Kiswahili navyo,hapo umbea tu ndo amefata
humu,akipigwa hapo au akikanyagwa atamlalamikia nani” mwanaume mmoja aliyekuwa
amevaa suti aliwaambia wenzake huku wakimtazama mama huyo mwenye baibui
iliyovaliwa kwa staili ya ninja hasa hasa kwa waumini wa dini ya uislamu
anavyopambana kwa juhudi ili apenye. Watu kwa huruma wakampisha,moja kwa moja
akiwa anakimbia kwa kasi alifika mbele ya ukumbi akaanza kuzubaa na mara ghafla
akakimbilia alipolala Reshmail na kuanza kutikisa
“huyu maza vipi mwehu nini? Yaani mtu
ameachiwa hewa impige yeye anaenda kuweka usiku tena na manguo yake” kijana
mmoja aliyekuwa amevaa jinsi kwa staili ya mlegezo aliwaambia wenzake
“tulia wewe huenda ni mamake huyo” alijibiwa
na wenzake
“reshmail amka amka mpenzi” alimwambia kwa
sauti ya chini.
--------------------------------------------------------------------------
Wivu wa utani utani aliouonyesha mbele ya mke
wake ulukuwa unatoka moyoni mwake,Adam alihisi huko nje labda kuna mjanja
anamchukulia mke wake.”ngoja nikamfumanie mtu leo” alijiwazia Adam huku
akipekua pekua nguo gani anaweza kuvaa iweze kumziba sura yake asiweze kufahamika
kwa urahisi mbele za watu,’baibui’ ndio jibu alilopata,harakaharaka akajitanda
kwa ustadi,alifahamu vyema pesa ya mkewe ilipokuwa inahifadhiwa akajichotea
kiasi kilichotosheleza kwa nauli “Mountain view” alijikumbusha jina la hotel
ambayo sherehe ilikua inafanyika,ni jina alilolikariri kwenye kadi ya mwaliko.
Akiwa na baibui lake alipanda teksi
ikamfikisha moja kwa moja eneo la tukio,kukuru kakara aliyoikuta pale ilimtia
hofu kubwa sana aliamini lazima kuna kitu kimeharibika eneo lile hakuwaza kitu
kingine bali usalama wa mkewe (Bite) moja kwa moja naye alijichanganya humo
ndani n
Tofauti ya malengo yake ya kumjulia hali
mkewe,macho yake yanakutana na Reshmail akiwa sakafuni na vazi lake zuri la
harusi,sura yake bado ilikuwa haijasahaulika katika kumbukumbu za Adam.
Nguvu zilizokuwa zimemwisha Resh pale chini
zilirejea kwa kasi kutokana na kusikia sauti ya kiume kutoka katika nguo za
kike “mamaaaaaaaaaaa!!!!” alipiga kelele kwa sauti ya juu huku
tayari akiwa amesimama wima akijaribu kukimbia,kamera zikageukia eneo lao tena
nyingi zikimmulika mwanamke mwenye baibui (Adam). Kabla hajakimbia Reshmail
alidakwa mkono wake.”Adaam……Adaaaam!!!” alipiga kelele kali zaidi wakati huuu
Reshmail. Adam alikuwa amejivua baibui kwa upande wa usoni,akiwa hajapewa jibu
lolote reshmail palepale alifika Bite,”Adam! Umefikaje hapa mume wangu…si
ulisema hauji…” Bite aliuliza
“nini? Nani? Umemwitaje? Na huyu ni…….”
Hakuweza kumaliziankauli yake wakati huu,mawazo yakauzidi nguvu ubongo wake
akazimia palepale.Wakati huo Chriss alikuwa analia tu hgajui kinachoendelea,Eve
na Benny walikuwa wanahaha huku na huko bila kukumbuka kwamba alikuwa na shera
safi kabisa tena ya gharama za juu kabisa,Benny ndio alikuwa kama tahira hajui
hata pa kuanzia alikuwa ameshtuka sana. Ilikuwa kama vita vile lakini hakuna
hata aliyejeruhiwa wala aliyekuwa anapigana vilikuwa si vita vya risasi bali
vita vya mapenzi. Wgeni waalikwa waligeuza tukio hilo kuwa kama filamu ya
kusisimua lakini waliyokuwa wameianzia katikati bila kujua ilianzia wapi na inaenda
wapi.,nani nyota wa filamu na nani adui.
***
Ni katika nyumba ya Eveline.Reshmail akiwa
mbele ya Beti amepiga magoti akilia kwa uchungu
“Bite wewe ni mwanamke mwenzangu nionee huruma
kwa haya niliyopitia,nimeteseka sana,nimedhalilishwa kwa ajili ya Adam,ni kwa
ajili yake hadi leo mimi ni bikra,kwa ajili yake familia yake imetuchukia,kwa
ajili ya Adam baba yangu haeshimiki tena mtaani kwetu,Bite sitamani mwanaume
yeyote yule,ukininyan’ganya Adam na Christian mimi nitakufa Bite,ni furaha gani
utaipata kwa kifo changu kwa ajili ya upendo?,sitajali huyu mtoto uliyezaa nae
wala sitaumizwa na ujauzito wake uliombebea,ninakuomba Bite niache na mimi
nipate furaha japo kidogo tu katika siku zangu zilizobaki hapa ulimwenguni,nisaidie
niweze kurudisha upendo uliogeuka chuki kati ya familia yangu na Adam.Bite
uamuzi upo mikononi mwako,ukikataa utaniumiza sana na nina uhakika nitakufa na
pendo langu kwa Adam” Kilio kilimzuia kuendelea kuongea,lakini nay eye mgongoni
mwake alilowanishwa kwa machozi ya Bite yaliyokuwa yanatililika muda wote
wakati Reshmail anaongea,kwa hali halisi alimwonea huruma lakini pia kwa dhati
kabisa aliwapenda Adam na Christian.Eve na mumewe Benny walikuwa
watazamaji,wenyewe hawakuwa na uwezo wa kutoa maamuzi yoyote yale. Christian
alikuwa ametulia kwenye kochi,hali ya utulivu aliyokuwa nayo ilipita siku zote.
“Adam tulipokutana unapajua,yote tuliyofanya
unayajua,upendo wangu kwako nadhani unautambua pia……labda sikupangwa kuwa wako
milele ndio maana aliyepangwa amejitokeza wakati muafaka,asante kwa zawadi ya
penzi lako,asante kwa mtoto na huu ujauzito hii ni heshima kubwa kwako
milele,neno gumu ninaloweza kulisema sasa ni kuwa kwa moyo mmoja nakuruhusu
uendelee na Reshmail,nayasema haya mbele ya mama yanngu Eveline” alizungumza
Bite kisha akashindwa kujizuia kuangua kilio kikuu kilichoamsha hisia za kila
mtu pale ndani wote wakadondosha machozi yao. Adam,Reshmail na Bite wote kwa
pamoja wakakumbatiana huku machozi yao yakitua juu ya Christian aliyekuwa ktikati
yao,ilikuwa ni picha ya kusisimua na kuumiza sana.
****** *****
Kilikuwa kikao kikubwa cha familia yao
Reshmail,watu wote muhimu walikuwemo jasoro mama wa familia hiyo aliyesusia
kikao,mzee Manyama,Reshmail,Eve,Benny,Bite,na Paskalina walikamilisha kikao
hichi,Christian alikuwa bustanini akibembea.Reshmail alikuwa anatoa siri nzito
nzito za kushangaza ambazo kwa namna kubwa kabisa zilitoa taswira ya mambo
yaliyokuwa yamefichika kwa muda mrefu,uhusiano wa kimapenzi kati yake na mama yake
mzazi ulimwacha kila mtu mdomo wazi,Reshmail aliomba msamaha kwa hilo na
alieleweka na kusamehewa. Ni katika usimuliaji wa upande wa Bite kuhusu ngome
ya vigogo iliyoleta fikra za mazingira ya kupotea kwa kadi yake ya benki katika
mazingira ya utata mkubwa,Benny hakuongea neno kwani yeye alikuwa kama mgeni tu
katika mkutano huo.Mzee Manyama alikuwa kimya akimtafakari mkewe kwa maovu
aliyoifanyia familia yake,kwa mateso aliyompa Adam na kwa uvunjifu wa amani
aliouleta baina ya familia hizi mbili,kwa fedheha aliyomletea na kumvunjia
heshima yake bungeni na hata mtaani,akiwa mwingi wa hasira alisimama bila kuaga
na kuelekea chumbani,kwa hali aliyokuwa nayo Reshmail aliamua kumfata kwa nyuma
ili asije kufanya jambo baya huko anapoenda,hasira yake ilipokelewa na na mwili
wa mkewe ukiwa sakafuni,tayari alikuwa maiti. “ulistahili hukumu hii” bila
kushtuka alisema mzee Manyama huku akimpisha Reshmail aingie humo ndani.
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
Mapema baada ya mazishi ya mama yake mzazi
Reshmail akiongozana na Adam katika gari ya baba yake,dereva akiwa Adam
walifunga safari ya kwenda Mwanza kwa wazazi wake (Adam).
“utabaki ndani ya gari nitatangulia mimi najua
watakuwa wakali hao lakini wakikuona ndipo mzizi wa fitna utakapokuwa umekatwa”
Reshmail alimpa maelekezo Adam ambaye alikubali kwa ishara ya kutikisa kichwa.
Gari ilipaki nje kidogo ya nyumba ya kina
Adam,kama walivyoelewana akashuka Reshmail akiwa amependeza sana,akaifunga gari
kwa kutumia rimoti aliyoshuka nayo na kwa mwendo wa kunyata akaanza kuusogelea
mlango akausukuma akaingia ndani,kupitia kwenye kioo Adm lishuhudi Reshmail
akitoweka machoni pake.
“umefata nini hapa we mchawi Adam hajakutosha
unamtaka na Rosemary ngoja sasa….Rose!!!!” aliita mama Adam,Reshmail akiwa
anatabasamu kwani alijua ni muda mfupi wote watakuwa na furaha kubwa. Akiwa
bado hajaanza kuongea alishuhudia mama Adam akimfuata na kisu huku Rosemary
akifika pale na mwiko mkubwa,wakati huu akili yake ilifanya kazi haraka akaanza
kukimbia lakini nguo yake ndefu ilimsaliti baada ya kunasa kwenye geti la
kutokea nje.
Kwa macho yake mawili Adam alishuhudia
Reshmail akiwa chini huku watu wawili wakimshambulia kwa fujo,alijaribu
kufungua mlango lakini ulikuwa umewekwa ‘loki’ sauti yake haikuweza kusikika
nje alipigapiga vioo vya gari lakini hakuna aliyemsikia. Alishuhudia damu
nyingi sana ikiruka juu. Kwa akili ya haraka haraka akakumbuka kushusha kioo
akatokea dirishani
“mamaaaaaaaaaaaaaaa!!!” Adam akaita kwa nguvu
palepale mama yake akageuka na kudondosha kisu alichokuwa nacho,”Adam mwanangu
ni wewe!!!” alisema mama Reshmail huku aimfuata Adam ambaye hakumjali bali
alifika alipokuwa Reshmail “Reshmail,Reshmail” “ mama na dada
mmemuua mke wangu jamani mamaaaa!!” alilia Adam baada yakuona hajibiwi
kitu.”A.d….am!! ninaku….fa mume
wangu….ninakufa kwa furaha…..ni..meku..rudish…sha
kwenu…naku…panda..sana” Reshmail aliongea kwa kujiumauma huku akivuja damu,raia
wengine walikuwa katika harakati za kutafuta msaada lakini msaada mkubwa
uliopatikana ni wa polisi waliowatia nguvuni mama Adam na mwanae Rosemary huku
roho ya Reshmail ikimaliza muda wake palepale Igoma jijini Mwanza.kama
usingekuwa ujasiri wa Adam basi tukio lile lingegharimu maisha yake,tayari mama
mkwe amepotea,na sasa mpenzi wake Reshmail,mama na mdogo wake wakitupwa jela
kwa kesi ya mauaji.
--------------------------------------------------------------------------------
“mapenzi yamenipotezea muda wangu nimekuwa
mfungwa miaka mitano,mapenzi yameivunja vunja familia yangu,mwanamke
niliyempenda ametoweka tayari tena mbele ya macho yangu,ni heri niisome hii
sheria vizuri zaidi ili ikiwezekana siku moja niwatetee ndugu zangu walioko
gerezani hao pekee ndio furaha yangu,kamwe siwezi kuhangaika tena na watoto wa
hapa chuoni hata siku moja sidhani kama wana maana sana kwangu nikithubutu tena
huend yatakuwa makubwa zaidi ya awali,usiku mwema Mosenya.” Alimaliza simulizi
yake Adam,wote tulikuwa tunatokwa machozi ya uchungu,lakini lengo langu
likatimia na swali la muda mrefu likapata jawabu baada ya simulizi hii kuanza
kuandikwa katika gazeti la chuo.
Olivia alimalizia hadithi yenyewe
niliyoisikiliza kwa makini.
“Mh ilikuwa nzuri simulizi yenyewe.”
Baaedae tulilala maana ilikuwa imefika saa
tisa usiku kwa sababu hadithi ilikuwa ndefu sana.
Wakati
usingizi unanipitia nilijisemea. Halafu nikalala fofofo.
MWISHO
MAPENZI NA
MASOMO
Olivia alikuwa mpenzi wangu na hadi sasa bado tunapendana kimapenzi.
Wakati nipo naye chumbani tumemaliza shughuli yetu ya kuondomola.
Olivia alianza kunisimulia hadithi moja kali aliyosimuliwa na mpenzi wake wa zamani.
Nikamkubalia “Haya Olivia nipe hiyo hadithi mpenzi”…………”
Rashimail want to be your friend.'confirm' 'ignore' ulikuwa ni ujumbe ambao macho yangu yalikutana nao nilipofungua mtandao wa kijamii wa ‘facebook’,sikumbuki kama nilijifikiria mara mbili kwani niliona ni jambo la kawaida sana kukutana na 'notifications’ kama hizo,na mara zote neno confirm(kubali) lilipata fursa ya kutumika.hivyohivyo hata kwa Rashimail nilifanya hivyo."You and reshmail are now friends" ndio ujumbe ulionisindikiza baada ya kukubali ombi lile kutoka kwa Rashmail.
--------------------------------------------------------------------------------------
Ni kijana mtanashati niliyebahatika kukutana nae pale chuo kikuu cha mtakatifu Augustine Mwanza,alijipenda kuanzia ndani ya chumba chake hadi mwili wake,ilikuwa ni nadra sana kumfumania akiwa amevaa nguo aliyoivaa jana,bila kumnyima haki yake nasema alikuwa anapendeza kila siku,macho yangu ya kipelelezi na kamera zangu za kipaparazi kamwe hazikufanikiwa kumjua aliyekuwa ubavu wa pili wa bwana huyu yaani 'MPENZI'. Ukipenda waweza kuniita kimbelembele lakini ukiniita hivyo basi majina hayo yatakuwa mengi pale chuoni kwani wengi walikuwa na shauku kubwa ya kujua siri hiyo na kamwe hawakufanikiwa.
Binadamu hatuna dogo watu washaanza kusema eti huenda jamaa ana matatizo makubwa tu mwilini mwake ndio maana yuko peke yake licha ya kushobokewa na wasichana warembo, mh! mimi sikuwa mmoja wao lakin nilijiuliza pia kulikoni??
Makala mbovu zilizokuwa zinaandikwa na gazeti la chuo lililojulikana kama ‘Saut voice’ ndo zilinizonivuta zaidi kutaka na mimi siku moja kuandika katika gazeti hilo lililokosa mvuto siku za hivi karibuni makala nzuri itakayorudisha heshima ya gazeti hilo.Taratibu nilijenga mazoea na hatimaye nikafanikiwa kumzoea "THE MOST WANTED" ucheshi wangu ndio uliomvutia zaidi kupenda kuwa karibu nami pamoja na mchezo wa mpira wa miguu kwani wote tulikuwa mashabiki wakubwa,haukupita mwezi mzima nikawa nina uwezo wa kuanza kazi yangu,ni mimi na Adam kwenye meza moja chumban kwangu ananipa hadithi yake ya maisha yaliyomfanya awe kama alivyo.
"Aah!! jamani Rashmail..." alianza Adam,yangu masikio na macho nikaanza kusikiliza kwa makini.
---------------------------------------------------------------------------------------------------
Hadi anafika mwaka wa pili kimasomo chuoni mtakatifu Augustine Mwanza kitivo cha sheria Adam aliitumia simu yake ya mkononi kwa ajili ya kupiga,kutuma ujumbe (sms) na kupokea ni hayo tu na kwa upande wa pili alipenda sana kucheza michezo ya simu (game) ya kwenye simu.
Alikuwa ni Hughorito Hamada ama maarufu kama 'HUHA'.hakuwa tu rafiki yake adam bali pia alikuwa ni mshirika wake wa chumba (room mate) na pia walisoma darasa moja la sheria pale chuoni,ni huyu aliyemuingiza Adam katika ulimwengu ambao hatausahau kamwe,tabia yake ya kupenda kuazima simu ya Adam aina ya Nokia Express music kwa dhumuni la kuchat katika mtandao maarufu wa kijamii wa ‘facebook’ ndio ilimshawish Adam naye kuanza kujiuliza kulikoni hasahasa alipokuwa anamwona Huha akicheka mwenyewe kila anapokuwa anachat,"Mh! we jamaa yangu chizi kweli yaani unacheka na watu usiowaona" Michael alimkebehi Huha alipokuwa anacheka na simu yake punde tu baada ya kuanza kuchat
"Kwani we ukiwa unaota unaongea huwa kuna watu mbele yako?" Huha alijibu mashambulizi na Adam akabaki kimya na taulo yake kiunoni akaenda bafuni kuoga.
"Mwanangu nimekuunga na wewe namba yako ya siri ni..,.." hata kabla Huha hajamaliza adam akamkatisha "Nini? huo upumbavu wako sitafanya kamwe bro" ..."Hv kwan inakuwaje huo upuuzi" Michael akajikuta anauliza baada ya kuwa amevaa nguo zake "Hii kitu inaitwa FACEBOOK,yan adam ukijiunga wewe hutoki na utakuwa nayo bize kweli" Adam alisikiliza kwa makin japo alijidai kufanya dharau machon,Huha hakujali aliendelea kutoa somo had Adam akapata mwanga,"Mh. Sidhan kama itanivutia bt i wil try". Alijisemea adam wakat anachukua simu yake.
-----------------------------------------------------------------------
Tabia ya Adam ilikuwa imebadilika ghafla ni Michael na facebook,facebook na yeye,iwe barabaran,club,lecture room,hostel yani kasoro mskitini tu ndio Adam aliweza kuhfadh simu yake.Sio Huha wala rafiki yake yeyote aliyejua nini zaid ya facebuk kimemuathiri adam wa watu.Hakumuazima tena Huha simu,hakutaka mazoea na wasichana ni yeye na simu yake tu!! "Adam mbona washkaji wanalalamika eti wanakuomba urafiki facebook unachomoa? siku moja Huha aliamua kumuuliza Michael baada ya kuona tabia yake imekuwa ya ajabu mno kupindukia."Sitaki that's all". Ndio jibu fup alilopewa.kisha adam akajiondokea.Huha akabaki ameduwaa asijue la kufanya,mara ghafla adam akarudi tena "Huha naomba ukamwambie Halima simtaki,usiniulize kwa nini mwambie SIMTAKI!" Michael alimwambia Huha kana kwamba alimfumania huyo Adija.
Mpenz msomaj Halima alikuwa binti matata pale chuon kwa kipind kile,Michael ndo alipata fursa ya kuangukia penz lake,penz lao chuo kizima walifahamu,gari ya Halima ilikuwa kama ya Adam..chumba cha Cha Halima kilipambwa picha na kad za Adam lait na Michael angekuwa anakaa peke yake basi hata yeye chumba chake kingekuwa had na nguo za ndan za Halima pamoja na pedi bas tu alikuwa anakaa na Huha.
Huha alibak mdomo waz akijiuliza ni Adam au kivuli chake kinaongea.Alikuwa Adam sio kivuli.....
Ubize aliokuwa nao mheshimiwa mbunge ulimkosesha raha mkewe bi.Gaudensia Ogunde,hakuipata haki yake ndoa kwa takribani mwezi mmoja sasa,mume alikuwa anachelewa kurudi na akirudi anakuwa amechoka sana kutokana na majukumu mazito ya kiserikali,na ikitokea siku akathubutu kujaribu kutoa huduma basi alikuwa hamridhish mkewe,taratibu mama akajaribu kuzoea lakini kuna wakat uvumilivu ulikuwa unamshnda,nyumba nzima alikuwa akiish yeye,mtoto wake wa kike na msaidiz wa kazi (House girl)."Mwanangu ni siku ya tatu baba yako halali nyumbani,najisikia mpweke sana kulala mwenyewe" bi.Gaudensia alimweleza mwanae kwa unyonge "Pole sana mamii hata mi sipend hyo tabia ya baba,leo nakuja kulala na wewe mama" alijibu yule binti mwenye miaka 17 akiwa ndio kwanza amemaliza kidato cha nne.Mama hakujibu kitu badala yake alimkumbatia mwanae kwa sekunde kadhaa kisha akamwachia huku machozi yakimlengalenga.
Majira ya saa tatu usiku mama na mwana walikuwa kitandan wote wakiwa na night dress,kitanda kilikuwa kikubwa lakin umbali wao ulikuwa karibu mno,mapigo ya moyo ya mama yalikuwa juu sana,jasho lilikuwa likimtoka mtoto kwa kasi air condition iliyokuwa inapuliza haikuwa na maana tena mama na mwana walijikuta katika hisia nzito sana za mahaba,sio mimi wala wewe tunaojua walipoanzia.
----------------------------------------------------
Reshmail Mtoto wa mwisho na pekee wa kike kati ya watoto wanne wa mbunge wa jimbo la Kinondoni Mheshimiwa Msuruli Haruna,hakupata kujua shida katika maisha yake na urembo aliojaliwa pia hakuufaham kwa sababu hakuwepo wa kumwambia kuwa yeye ni mrembo,kuta na fensi ya sen'gen'ge iliyozunguka mji wao haikumruhusu kutoka nje hovyo hovyo,tofauti na siku ya kwenda msikitini Resh alilazimika kusubiri hadi alipofikisha miaka kumi na nne alipojiunga na kidato cha kwanza katika shule ya st.marry's international ndio alipata wasaa wa kujumuika na wananch wengne wa Tanzania na nchi za jirani,elimu yote ya darasa la kwanza hadi la saba aliipatia katika jumba la kifahari la baba yake.
Mazoea ya kuish maisha ya peke yake peke yake yalimtesa sana Resh kiasi kwamba hadi anamaliza kidato cha nne aliweza kuwa karibu kiurafiki na wanafunzi wachache na weng wao wakiwa wasichana tena watoto wa matajiri na vigogo mbalimbali wa serikali.Kampani kubwa ya Reshmail alikuwa ni mama yake mzazi,yalikuwa ni mazoea makubwa sana lakini yasiyoshangaza,mara nying walikuwa wanatembea pamoja huku wameshkana mikono huku wakifurah sana.
Kidato cha tano na sita katika shule ya Arusha international school ndio kwa mara wa kwanza ilimpeleka nje ya jiji la dar-es-salaam.
Resh alilia sana kutenganishwa na mama yake lakini hakuwa na jinsi ilimlazimu kuondoka,mama alishindwa kujizuia alilia kwa uchungu ambao mumewe hakuutambua maana yake. "Nitakuwa nakuja kukusalimia" bi Gaudensia alimnon'goneza mwanae wakati akipanda gari la baba yake kuelekea airport."Usiache mama".alijibu resh huku akimbusu mama yake shavuni.
Mwanzoni ilianza kama utani pale Adam alipokubali ombi la Reshmail kuwa marafiki,walikuwa wakiulizana mambo ya kawaida sana huku katika orodha ya marafiki wa Reshmail ni Adam peke yake alikuwa mwanaume,"Mbona una marafiki wachache au ndo umejiunga facebook?" adam alimuuliza reshmail katika moja ya 'chatings' zao "No ni uamuzi 2 iam nt interested with boys i wonder why you?" "May be iam someone special,who knows" alijibu Adam, "You might be" alijibu reshmail."Yani hadi mchumba wako hujamweka kwenye orodha?" "Sina huyo mchumba unayemdhania" "What? msichana mrembo kama wewe,au hizi picha sio zako?" "Ni zangu kwani ukiwa mrembo lazima uwe na mpenzi?"alisisitiza Resh kisha akaendelea "Naona we upo kwenye uhusiano,hongera" aliandika Resh,ni wanaume wachache sana akiulizwa na msichana mrembo kama ana mpenzi halafu akubali na hata kwa Adam ilikuwa hivyo,"Mh! nimejiandikia tu,mi sina mtu nani wa kunipenda mimi?". Alidanganya Adam,"What! hawakioni hcho kifua chako au na wewe hiyo sio picha yako?"
"Ni ya kwangu,Reshmail una utani wewe"
"Sina utani nimekipenda sana"
"Haya asante,kwako wewe sina la kusema unavutia kila upande"
"Asante lakini we zaidi,Adam naingia kuoga nisindikize basi"
"Wee,si umeniambia mnakaa wanne sa wenzako watanielewaje?" alijibu Adam huku akiamini kwamba hayo yote yanayotokea ni utani mtupu.
"Kwa hyo ningekuwa peke yangu ungenisindikiza?" "Yeah? ningekusindikiza lakini ningefumba macho" alitania Adam.
"Vp ninatisha sana au,yan hadi ufumbe macho sawa tu" alilalamika Resh,"Natania mrembo lakin si unajua tena nitajiumiza"
"Ok! tuachane na hayo,simu yako inauwezo wa kufungua e-mail?"
"Inafungua tena sasa hivi nilikuwa ninasoma emails" alijibu adam.
"Ndio hii Adamboy@Yahoo.com?" "Yap ndio hyo" "Fungua baada ya dakika tano uone zawadi yako"
Jasho jembamba huku mikono ikitetemeka,macho yakiwa yamemtoka Adam hakuamin anachokiona kwenye simu yake.
-----------------------------------------------
Mazoea ya Reshmail na mama yake kujigeuza mtu na mpenzi wake yaliwaathiri sana wawili hawa,mara kwa mara Bi.Gaudensia alifanya safari za ghafla kwenda Arusha kufaidi penzi la jinsia moja kutoka kwa mwanae mpendwa,raha alizozipata hakuwa na muda wa kumfikiria mumewe tena,tabia hii ilimuathri sana Reshmail pale shulen,licha ya urembo wake hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume yeyote pale shulen bila kujalisha uwezo wao kifedha wala sura na utanashati wao,aliwaona hawana maana kwake zaid ya mama maskin Resh hakujua tamtam ya penzi la wanaume.
Alikuwa ni Eveline,binti aliyekuwa anaish chumba kimoja na Resh,akiwa ni mzaliwa wa hapohapo Arusha anayezijua kona zote za Arusha,pombe,club na ngono ndio walikuwa marafiki zake wakubwa,alikuwa mchesh na mzuri wa sura lakin kubwa na jema zaid alikuwa mwelevu sana darasani katika mchipuo wa "H.G.E" pamoja na reshmail,ni jambo hilo lililowaweka wawil hawa karibu.Mshipa wa aibu haukuwepo kichwani mwa Eveline,na kama ulikuwemo basi haukuwa unafanya kazi vizuri,picha alizozipenda ni za uchi na movie za ngono ndio alizokuwa anaangalia tena kwa anapandisha sauti hadi vyumba vingne wanasikia.Ni huyu Eveline aliyemwingiza Resh katika maswali ya kwa nini,na inakuwaje "Mbona nikifanya na mama silii kama hao? alijiuliza Reshmail akiwa ndan ya kitanda chake huku pemben Eveline akiwa bize na laptop yake akiangalia filamu ya ngono "Ponographics" ......."Nitamuuliza Eve siku moja lakin nitaanzaje?" alijiuliza
Mara zote walizokuwa wakipeana burudani kitandani au sakafuni Mama yake alikuwa ndiye mwalimu wa kila kitu,yeye ndio alijua wapi amguse,wapi amtekenye ili mradi kuleta raha na wote kuridhika.Lakini safari yake ya mara ya tano kwenda Arusha kwa mpenzi wake huyo haramu ndipo alipokutana na mshangao.Reshmail yuleyule aliyekuwa zuzu kitandani akihudumiwa kila kitu na mama yake ili aridhike alikuwa moto wa kuotea mbali.Alimgalagaza mama yake ipasavyo kwa ku2mia vidole vya mikono yake pamoja na ulimi wake kutambaa kila kona ya sehemu husika .Mama reshmail (Bi.Gaudensia) alijikuta akiongea lugha ambazo hazipo katika ulimwengu huu.Hoteli ya Tanzanite chumba namba 18 kiligeuka kama pepo kwa wawili hawa,mama alikuwa analia sana machozi ya furaha na mbaya na ya kuchekesha eti akasema "Darling UTANIOA eeh!" jaman raha zikizidi sijui kilimfurahisha nini mama huyu kwa mwanae.Kulipokucha Bi.Gaude alimrudisha mwanae shuleni kama alivyokuwa amemwombea ruhusa."Mama huyu ni rafiki yangu anaitwa Eveline,Eve huyu ni mama yangu mpenzi" Reshmail aliwatambulisha baada ya kumkuta Eveline pale ofisini."Shkamoo mama" "Marahaba" alijibu mama bila kumwangalia usoni Eveline ambaye hakujali hilo sana "Punguza wivu sweet" Resh alimnon'goneza mama yake,ambae alitabasamu "Nakupenda mwanangu" "Nakupenda mama" waliagana mama akaondoka kurudi kwa gogo lake (Mumewe) huko dar.
---------------------------------------------------
"Ukitaka kuujua utamu wa ngoma ingia ucheze" ndio jibu alilopewa Resh baada ya siku moja kumuuliza eti anafaidika nini kuangalia filamu za ngono,mwanzoni alikuwa akiangalia kwa aibu san lakini baada ya kufanikiwa kuzihamishia kwenye "Laptop" yake mambo yakawa ya kawaida japo kwa kujificha,mara nying alijifunika shuka na kuweka earphone masikion kisha burudani.Ni mchezo huohuo mchafu Resh aliuiga na kwenda kujaribisha kwa 'mpenzi mama'."Hivi Eveline kuna raha kufanya au kuangalia peke yake inatosha?" "Haha haloooooo! unalo shosti,wenzio wakata viuno we wafurahia miguno looh!" Vidole vikiwa juu kama muimba taarabu Eve alimchambua Resh,"Mh! shoga si unifunze kuliko kunichambua?" alijitetea resh kwa saut ya chini,"Ulisema huna bwana weye sasa kulikoni ya nini haya tuachie sie wamama wa shughuli" "Eve we ni rafiki yangu ngoja nikwambie ukweli.....mimi nampenda mtu ambaye sijui kama ananipenda au tutaendana"
"Vipi hujawah kumwona au?"
"Nimemwona kwenye picha"
"He! una makubwa we mrembo au ndo yule kwenye kompyuta yako?"
"Haswaa ndio yeye"
"Hata kama hujamuona yule pale dume la ukweli,kile kifua usimlete kwangu nitakuibia," alitania Eve.kisha akaendelea "Najua hujui jinsi gani utampata niachie hyo kazi mimi ndan ya wiki moja nakukabidh mali yako." "Asante evely asante sana" alishukuru
* * * *
Ilikuwa ni picha ya binti mrembo sana akiwa amejifunga taulo kwa chini huku chuchu zikiwa nje,"Ndio natoka kuoga,vp nimetakata?" iliambatana na ujumbe ule.Adamu alibaki mdomo wazi,mh!! hivi inawezekana akawa Reshmail dah! alishangaa Adam.Akiwa bado mdomo wazi email nyingne iliingia ilikuwa picha tena,safari hii ilionyesha sehemu yote ya nyuma "NIPAKE MAFUTA" ndio ujumbe uliobeba picha hyo.Bila kujua muda gani na kwa misingi ipi Adam alikuta pensi laini ikiwa imembana,kuja kugundua chanzo ni sehemu flani kwenye mwili
wake ilikuwa imeongezeka ukubwa (Ha ha ha ha wanaume dhaifu sana.
Majukumu ya hapa na pale yalikuwa yamembana sana Bi.Gaudensia ambaye ni mama yake na Reshmail,pia uwepo wa mumewe katika himaya yake ilimnyima kabisa raha mama huyu na alikuwa anakosa nafasi ya kwenda Arusha mara kwa mara kufurah na mwanaye jambo ambalo lilimtesa kwa takribani mwezi mmoja na nusu.Vipindi vya bunge vilipoanza tena ndio hapo nafasi ilipatikana tena,kwa muda wote ambao alikuwa jijin dar-es-salaam Bi.Gaude alikuwa akiwasiliana na mwanae karibia kila siku kwa njia ya simu,alijua ni jinsi gan hata mwanae huyo alivyo'm-mis' hvyo aliamua kumfanyia 'surprise' ya kwenda huko Arusha shuleni bila kumwambia ili kuinogesha furaha yao ambayo ilikuwa inakamilika kitandan."Baba Resh mie kesho naenda kumsabah mwanetu,lakin hata simwambii nataka ashtukie tu,mama huyo"
"Atashangaa kweli,msalimie sana mwambie nitakuja kumsalimia bunge likimalizika" "Haya,zimefika"
-------------------------------------------------------------------------------
Penzi la ku-chat katika mtandao wa facebook lilikuwa limemchanganya sana Reshmail wa watu,Adam hakuwa nyuma kumpa maneno matamu ya hapa na pale ambayo kamwe alikuwa hajawah kuyasikia masikion mwake,Eve mwenyewe alimshangaa huyu shoga yake lakin hakuwa nyuma kumpiga tafu katika mpango mzima wa kumtia Adam majaribuni ndio maana alimshawish Resh kupga picha mbaya ambazo mwanaume yeyote akiziangalia lazima ajiulize mara mbilimbili kuhusu urembo asilia wa binti yule.
"Mi nipo peke yangu siku hizi rum-mate wangu ameenda kwao babake anaumwa" "Don't tell me kuwa unalala mwenyewe"
"Nitafanyaje sasa na wewe upo mbali?"
"ooh! my ghosh! assume nipo hapo"
"Aah,nitajiumiza bure tu mpenzi wangu"
"Anarudi lini kwani?"
"Mh! amesema atatumia kama wiki mbili hivi,njoo basi unipe 'kampan' kiaina"
Yalikuwa mazungumzo kwa njia ya simu kati ya Adam na Reshmail yaliyokatishwa na na mlio wa 'low battery' katika simu ya Reshmail "Baby boy tutaongea kesho,pole sana na ninakupenda sana" alimaliza Resh na simu ikawa imezima.
"Eveline nataka kwenda Mwanza" asubuh ya siku iliyofuata Resh alimwambia Eve.
"He! makubwa haya,imekuwaje kwan shoga" aliduwaa.
"Mi sijui lakin nataka kwenda tu" alisema Reshmail "Haya lini wataka kwenda?"
"Hata kesho mi naenda tu" "Mh! sikuwez haya jiandae kutoroka coz ruhusa hapa kupata sahau" "Vyovyote poa ninachotaka ni kuondoka na kwenda Mwanza that's all" alijibu kijasiri Resh hali iliyomduwaza eveline.
----------------------------------------------------------------
"Reshmail hayupo? mbona jana alikuwa hapa ofisin?" mwalimu wa zamu alikuwa anamuuliza mwanafunzi aliyeagizwa kumuita Reshmail baada ya mama yake kuwa amefika,"Hata mi sijui mwalimu"
"Hapana sio jambo la kawaida reshmail kutokuwa mazingira ya shule tena jumatatu! hebu mwambie time-keeper agonge kengere mara moja" aliamrisha mwalimu.
----------------------------------------------------
Hakuwa hata na chembe ya utani Reshmail wa watu,majira ya saa moja asubuhi tayari alikuwa kwenye gari la KIMOTCO ninalotoka Arusha kwenda Musoma kwa kupitia Mugumu Serengeti,kitu kinachoitwa hofu moyoni hakikuwepo hata kwa mbali,ndani ya kipochi chake kidogo alikuwa na pesa taslimu za kitanzania shiling laki mbili zikisindikizwa na kadi ya viza ya CRDB iliyokuwa na uwezo wa kutoa shiling laki tano kwa siku mara nne yaani milioni mbili zilikuwa zimehfadhiwa katika acount yake ya akiba.Mamaa wa shughuli (Eveline) alikuwa pembeni ya Reshmail,hofu kwake haikuwepo wala hakuiwaza tayari alikuwa mzoefu wa mambo hayo."Eveline yani akili ndo inakuja sasa hivi eti kwa nini tusingepanda ndege dah! gari linaenda taratibu hilo jaman" alilalama Reshmail kwa wananch wa kawaida waliomsikia walidhani ni mashauzi na majigambo ya watoto wa kike
"Mh? shoga ulivyokuwa na hamu ungekumbuka hayo,tutafika weye acha papara"
Gari lilizidi kuchanja mbuga za ngorongoro kwa kasi ya kawaida hadi majira ya saa saba tairi chakavu za gari hili zilikuwa tayari kwenye mbuga za Serengeti,Resh alikuwa macho anatazama safari inavyokwenda huku akihesabu masaa yanavyokatika kwa kasi huku mwisho wa safari ukiwa haufiki.Eve yeye alikuwa ameuchapa usingzi huku akiwa amejifunika uso wake kwa kofia yake nyeusi ambayo vumbi ilikuwa imeibadili rangi yake na kuwa ya ugoro.(Brown).
"Eve Eve Eve,amka uone wewe" Resh alikuwa anamwamsha kwa fujo."Angalia hii sms imeingia sasa hv" "Resh mazako kaja unatafutwa uko wap?" jasho jembamba likaanza kumtoka Resh lakin Eve hakushtuka sana.Walikuwa wametumiwa ujumbe mfupi na mmoja wa viranja."Eve tumeisha tumeisha"
----------------------------------------------------------------------
Ulikuwa mshikemshke wa ghafla pale shuleni mwalimu aliamuru kila mmoja aje mstarini hata kama ni mgonjwa,viranja walitii amri na kuita wanafunzi wote kwa haraka hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyebaki ndani ya bweni.
Wakiwa hawajui nini kinachoendelea mwalimu wa zamu aliyeitwa Mwl.Chipeta alikuwa mbele ya wanafunzi waliokuwa kimya kumsikiliza yeye.”Kabla sijatoa tangazo hili,ni nani anatambua mwanafunzi ambaye hayupo eneo hili? (Kimya)
"Nani anaumwa na amepewa ruhusa?" (Kimya)
"Kwa hyo wote mpo?" (Ndiooo)
"Haya mchepuo wa H.G.E wote pita mbele" aliamuru mwalimu Chipeta na kwa haraka wakaanza kujongea mbele."Mamaaaaa," ghafla kelele ilisikika kuna mwanafunzi aliyekuwa mgonjwa alikuwa ameanguka chini kwa sababu ya kizunguzungu.Ustaarabu ukatoweka pale ghafla kila mwanafunzi akawa anasema lake,mara hivi mara vile. Hata mwalimu Chipeta alitimua mbio kuelekea kwenye tukio.
Ni wakat huohuo Joyce ambaye alikuwa kiranja alipata mwanya wa kutuma ujumbe kwa Reshmail kumpa taarifa.
-------------------------------------------------------------------
Roho ilikuwa inamdunda Reshmail kwa kasi sana,aliamin kila kitu kitakuwa wazi na atafukuzwa shule,"Eve watanielewaje wazazi mie mh! nimerokoroga" alijisemea Reshmail.
"Upo na steringi lazima tushinde haka kavita kadogo" Eve alimpa moyo wa ujasiri Resh,"Naomba hiyo simu si ina salio kidogo"
"Imo elfu tatu"Alijibu huku akimpa simu Eve.
"Sihitaji zote hizo natumia shiling 60 tu hapa"Alijibu kwa jeuri Eve huku akionekana kujiamini zaidi.
"Sasa hyo 60 itafanya nini shogangu au umesema elfu sitini?"Alitania Resh na wote wakajikuta wanacheka.
"Dakika tano nyingi majibu mazuri yatakuja,chukua simu yako ikiingia meseji uisome mi nalala bibie tuliza roho yako hii sio movie ya kihindi eti stering anauwawa,hili picha la kichina stering anachomwa kisu bado anapona" alimaliza Eve na kushusha kofia yake ikafunika macho.
Ni kama alivyosema dakika tano zilikuwa nyingi sana ujumbe kujibiwa
"Na ufanye kweli mi narekebisha mambo nyie tanueni kwa raha zenu na pia kuhusu yule wa H.G.L vipi?" ulisomeka ujumbe."Mungu wangu amakweli Eve steringi jamani yaani kirahisi hvyo" alijisemea Resh kwa sauti ya chini akidhani Eve amelala tayari "Futa sms ya huyo mjnga nitamalizana nae" kwa saut ya kivivu Eve alimwambia Resh.
-----------------------------------------------------------
Ndege ya Precion Air ilikuwa inaondoka kutoka Musoma kwenda Dar-es-salaam kupitia Mwanza majira ya saa kumi na moja wakati basi la KIMOTCO lilifika saa kumi na nusu jioni,Resh aliona akipanda gari anaweza kuchelewa kwa Adam Mwanza japo hata umbali wa Musoma kwenda Mwanza hakuufahamu."Resh ndege ya wapi tunapata sasa hv jaman" Eve alimuuliza Resh wakiwa ndani ya 'Teksi’ kutokea stendi kuu ya Musoma maeneo ya Bweri."Tunajaribu steringi wangu"
"Haya!! utamu na uchungu wa mapenzi mwachie aliyeyabeba" alitoa fumbo Eveline.
"Dereva dereva zuia kidogo tafadhali" ghafla Resh alimwomba dreva naye bila hiana akazikanyaga breki bila kuuliza kulikoni. Mbio mbio Resh akashuka akaanza kutimua mbio kurudi nyuma huku akiwa peku viatu ameacha garini Eve,Dereva na wananchi wengine wakabaki kumshangaa.
Mwalimu Chipeta aliongoza zoezi zima la kumshughulikia mwanafunzi aliyeanguka pale mstarini,shule ya Arusha international ilisifika sana kwa kujali afya za wanafunzi hivyo tukio lile lilisababisha Mwalimu Chipeta kumsahau kabisa Bi.Gaudencia mama yake Reshmail na kwenda kushughulika ipasavyo kwenye lile tukio,aliyekuwa ameanguka alikuwa Naomi Holela mwanafunzi aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua na pale kilikuwa kimembana hasa kutokana na baridi iliyokuwepo nje. Gari ya shule ilifika haraka Mwalimu Chipeta na viranja wawili pamoja na 'matron' walimsindikiza Naomi hospitali. Akiwa ndani gari Mwalimu Chipeta alisikia simu yake ikitoa mlio wa kupokea ujumbe mwanzoni alipuuzia kutokana na ubize uliokuwa ukimkabili lakini punde alitoa simu yake na kufungua ujumbe ulioingia
"Niaje ticha mi Wa ukweli nipo na Resh mbali kimtindo kama vipi rekebisha mambo huko mi nikija nakuletea geto yule Amina wa H.K.L,niandalie tu mapene yangu" uso wake ulisahau matatizo yote yaliyokuwa mbele yake,ni muda mrefu sasa tangu Mwalimu Chipeta muhitimu wa shahada ya elimu ya fasihi andishi katika chuo kikuu cha Dodoma alikuwa amemfukuzia binti mrembo wa kawaida tu Amina bila mafanikio tegemeo lake alikuwa ni Eve au Wa ukweli kama walivyomzoea,bila kupoteza muda Chipeta alifungua sehemu ya ku'forwad' meseji na akaituma kwa Mwalimu.Madege ambaye wote lao lilikuwa moja,alikuwa ni mwalimu Madege aliyeijibu ule ujumbe na kuulizia kuhusu yeye na mpango wa kumpata binti wa H.G.L.
"Samahani wewe ndio mama yake na Reshmail "Mwalimu Madege aliuliza baada ya Bi. Gaude kuingia katika ofisi ya makamu mwalimu wa zamu .
"Ndio ni mimi baba"
"Kwanza samahan sana kwa usumbufu uliojitokeza"
"Usijali na mimi niwape pole kwa matatizo yaliyojitokeza hapa"
"Tunashukuru ndio mambo ya shule haya,eeh! mama nimepokea ujumbe sasa hivi kwamba mwanao yupo katika mbuga za Serengeti ambapo wanafunzi watano waliofanya vizuri walipelekwa kufanya utalii wa siku tano" alidanganya mwalimu Madege.
"Jaman huyu mtoto mbona hakuniambia?... baba yake atafurahi sana akisikia maendeleo ya mwanae"mama Resh alijieleza kwa furaha iliyozidi wasiwasi aliokuwa nao.
"Tuliwashtukiza hawakuwa na taarifa hata wao wameshangaa mno" aliendelea kupanga maneno huku akichorachora mezani kwa kutumia karamu isiyokuwa na wino.
Moyo wa mama Reshmail uliridhika japo mwili ulikuwa na kinyongo kwa kukosa haki yake. Ilimbidi siku hiyo hiyo afunge safari kurudi jijini Dar na zawadi alizokuwa amemletea mwanae zikiwa mikononi mwake.
----------------------------------------------------------
A.T.M ya N.B.C aliyoiona maeneo ya Nyasho ilimkumbusha kuwa kadi yake ni 'VISA' inafanya kazi mashine ya A.T.M ya benki yoyote bila kujali macho ya watu alitimua mbio pekupeku hadi kwenye mashine ambapo kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni na mtandao ulikuwepo "You can withdraw up to 1000000 with your A.T.M card daily N.B.C WE CARE" kijitangazo kwenye kioo cha mashne kiliibua tabasamu la Reshmail,na bila ajizi akabonyeza chaguo la kutoa laki tano kwa mikupuo miwili na kutimiza kiasi cha milioni moja, kisha kwa mwendo wa mbio kama alivyoingia akatoka akisindikizwa na miluzi ya wauza mitumba wa Nyasho ambayo kwake haikuwa na madhara hata chembe
"Samahani safari yenu imeahirishwa tafadhali hadi kesho asubuhi!" sauti nyororo ya mwanadada wa mapokezi aliyehusika na masuala ya Booking aliwaeleza mwanaume mmoja aliyekuwa na mpenzi wake wakitegemea kusafiri muda mfupi ujao kwenda Mwanza.
Sura zao zilizokuwa na furaha zililegea na kuwa kama watakavyokuwa pindi wakipata wajukuu,"Haiwezekani huu ni upumbavu tena ujinga ujinga ujinga,yani safari yangu inahairishwa ghafla kama vile safari za baiskeli,hapana sipo tayari nas...."
"shhhhh!!" kwa ishara ya kidole kimoja kuziba mdomo alinyamazishwa yule baba aliyetaka kuugeuza ukumbi ule uwanja wa mapambano na matusi. Kwa ishara nyingine yule dada akamwita akasogea pale alipo akamnon'goneza "Unawaona wale wasichana wawili,mmoja kimada wa mtoto wa raisi mwingne mtoto wa kamanda wa jeshi ni simu kutoka ikulu,kwa usalama wako acha kelele" alimwambia huku akimwelekezea walipo Resh na Eve. Bila kuhoji huku uoga ukimtawala hadhi yake ikashuka haraka haraka akamvuta mkewe wakaondoka wakawapisha kwa mbali Resh na Eve kama vile wanatema cheche za moto.
------------------------------------------------------------------------------
Ni kweli nafasi zilikuwa zimejaa lakini pesa iliongea nafasi ya mtu mwingine wakapewa wao tena harakaharaka,huku mtendaji wa jambo hilo akiweka shilingi laki mbili na nusu kibindoni. Huku Resh na Eve wakipata nafasi katika ndege ya Precision Air kiulaini,kwa mara ya kwanza Eve anapanda ndege "Mh! ushoga nao raha wakati mwingine” alijisemea wakati muhudumu wa ndani ya ndege akitoa maelekezo madogomadogo.
Ilikuwa kama safari ya kutoka Kimara Dar kwenda Mbagala,tayari walikuwa jiji la Mwanza
"Eve rushwa tamu wewe,naamini haitaisha ona sasa tupo Mwanza tayari" Resh alimwambia Eve wakati wanasafisha macho yao wajue nini cha kufanya baada ya kushuka kutoka kwenye ndege.
"Hoteli yenu ni nzuri?" Eve alimuuliza muhusika aliyekuwa ndani ya kigari kidogo kilichoandikwa Millenium Hotels kilichokuwa hapo kwa lengo la kutafuta wateja wanaotua na ndege uwanjani hapo,"Ni nzuri sana hautajuta kuwa pale.”
"Mh! haya,Resh twende giza linaingia" Eve alimwita Resh wakajitoma ndani ya gari na safari ikaanza.
"Darling umetoka kwenye michezo tayari pole mpenzi" ulikuwa ujumbe mfupi kutoka kwa Adam kuja kwa Resh,tabasamu pana likameza mdomo wake looh! lilikuwa tabasamu lililoelezea furaha ya moyo.
Adam alituma ujumbe huo akijua Resh yupo shuleni tena ilikuwa siku ya michezo ambayo Resh alipenda kushiriki hasahasa mpira wa kikapu.
"Mamaaaaa!!"Resh alipiga kelele ghafla gari ikayumba huku na huko,dereva akajaribu kwa uwezo wake wote kuirudisha barabarani "Paaaa!!" mlio mkubwa ukasikika.
--------------------------------------------------------------------------------------
Adam alipokea ujumbe kutoka kwa Reshmail akiwa maeneo ya kijiweni barabara ya lami kuelekea chuo kikuu cha mtakatifu Augustino,kupitia shule ya wasichana ya Ngaza.Adam alikuwa pamoja na rafiki yake (Huha) katika pikipiki ya rafiki yao aliyekuwa amewaazimisha wazungukiezungukie maeneo.
"Huha hebu endesha twende hapo Nyegezi kona kuna mtu nataka kuonana naye mara moja" Adam alimwomba Huha.
"Tayari Halima ametuma meseji mwambie hatuna mafuta atufate na gari yake bwana" Alitania Huha huku akianza kuiondoa pikipiki taratibu
"Ungejua hata usingesema wewe twende ukajionee maajabu ya mwaka" alijibu Adamu huku pikipiki ikizidi kushika kasi.
Ndani ya dakika tano tayari walikuwa Nyegezi kona ambapo Huha alipaki pembezoni kidogo na barabara iendayo stendi kuu ya Nyegezi jijini Mwanza,Adam alielekea dukani kununua vocha,na Huha akasogea pembeni kidogo aweze kuvuta sigara yake.
------------------------------------------------------------------
Dereva akiwa mwingi wa mawazo yake binafsi yasiyomuhusu Reshmail wala Eve na hata kama yangekuwa yanawahusu ule haukuwa muda muafaka wa kuwaambia.Macho ya Reshmail yalikuwa yamekutana na bango kubwa lililoandikwa "KARIBU CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AUGUSTINO" kwa hamu kubwa aliyokuwa nayo ya kumwona Adam ambaye alikuwa pia mwanafunzi ndani ya chuo hicho ndio sababu kuu ya kujikuta akipiga kelele kwa nguvu hali iliyomshtua dereva kutoka katika mawazo mazito na kujikuta akiyumbisha gari huku na huko hadi ilipokutana na pikipiki iliyokuwa imepakiwa pembezoni mwa barabara na kuirusha umbali ambao si wa kutisha sana,iligeuka vurumai madereva wa teksi na bodaboda za pikipiki walikuwa wakali sana hawakutaka kusikia la mtu,wengine hasira za kukosa abiria tangu waingie kijiweni asubuhi walizihamishia katika tukio hilo. Usingekuwa upole wa yule dereva basi mawe waliyobeba wananchi yangeigeuza ile gari kuwa mkweche. Eveline alitelemka garini kwenda kumsaidia dereva kujitetea lakini Reshmail uoga ulimtawala akawa amejibana kwenye viti vya nyuma vya ile gari huku akitetemeka. "Mh! Adam hawezi kukosa mwenyeji maeneo haya ngoja nijaribu kumpigia,ah! hii safari imetawaliwa na mikosi dah!" aliwaza Resh huku akichukua simu yake kutoka katika kipochi chake.
Lakini kelele zilizokuwa pale aliamini hawezi kusikilizana vizuri na upande wa pili,taratibu huku akitetemeka alifungua mlango akashuka na kuanza kutembea kuelekea pahali ambapo kidogo pametulia. Zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wenye hasira eneo lile wakageuza vichwa vyao kuangalia kazi ya Mungu ilivyotendeka vyema katika mwili wa Reshmail,badala ya kumpigia kelele dereva,miluzi mikali ikiongozwa na dereva mkongwe wa teksi eneo lile ndugu Sanya Bonda ikahamia kwa Reshmail,Resh akajifanya kama hasikii vile "Ilikuwa haki ya dereva kupotea njia jamani" Bonda alisema kwa sauti ya juu na kugeuza hasira za watu kuwa vicheko. Resh taratibu akaufikia mti mdogo mbali na eneo la tukio akabonyeza namba za Adam. Simu iliita muda mrefu bila kupokelewa. Alipopiga mara ya pili simu ilipokelewa."Helow Resh subiri nisogee pembeni nakupigia kuna tatizo limenipata" alijibiwa na Adam katika simu.
"Hata mi....." kabla hajamalizia kauli yake Reshmail simu ilikatwa akiwa bado anaduwaa kama dakika mbili pembeni yake alizengea kijana mmoja ambaye Resh hakutaka hata kumwangalia machoni,alijua ni walewale waliokuwa wakipiga miluzi na kumwita majina waliyotaka. Resh taratibu akajisogeza pemben."Vipi dada mbona wanikimbia au mi nanuka halafu we mrembo haya basi umebarikiwa sana najua unataka kusifiwa" aliongea yule kijana lakini Resh hakujibu.Simu yake ya mkononi iliyokuwa katika mfumo wa kimya(Silence mode) ilikuwa inatoa mwanga kuashiria aidha kuna ujumbe umeingia au kuna simu inaingia,lakini kwa jinsi alivyoandamwa na yule kaka kwa maneno hata hakuweza kugundua.
Baada ya dakika kadhaa akaondoka yule kaka ndipo kuangalia simu akagundua ilikuwa imeita mpaka imekata na hakuwa mwingine bali ni Adam alikuwa amepiga,harakaharaka akapiga tena. Ulikuwa mshangao wa hali ya juu sana Reshmail hakuamini alipomwona yule kijana aliyekuwa ametokea pale dakika chache zilizopita kuelekea kwenye zile vurugu ndio anapokea simu."Resh mbona nimekupigia hupokei mamaa" alimshuhudia yule kaka akiongea kwenye simu huku akirejea lile eneo kukwepa kelele,kama ilivyo kwa mtu aliyenaswa na umeme Reshmail alikuwa ametulia tuli na simu sikioni huku yule kaka akizidi kulikaribia eneo lile “Reshmail mbona huongei!!” aliendelea kuuliza bila kupata majibu."Adam" alijitutumua Resh na kutamka akiwa jirani naye kabisa,bila kujua yule kijana akaangusha simu yake hakuamini msichana aliyetoka kuongea nae dakika kadhaa ndio Reshmail wa Arusha.
----------------------------------------------------------------------------------
Vurumai lilisawazishwa haraka sana Adam na Huha ndio waliokuwa wamiliki wa ile pikipiki iliyogongwa na gari waliyokuwemo akina Reshmail."Jamani huyu hapa ni dada yangu,ndio alikuwa amenipigia simu tuonane hapa naomba haya mtuachie sisi" Adam aliuambia umati ule ambao hasira zao zilikuwa zimeanza kupoa na haraka walimwelewa wakaacha kumzonga dereva.Reshmail bila kupoteza muda akamwongoza Adam wakaingia garini akampa pesa taslimu shilingi laki tatu kwa ajiri ya matengenezo ya ile pikipiki naye Adam akamkabidhi Huha kisha akajumuika na Eve pamoja na Reshmail katika gari,huku Reshmail akiwaacha watu hoi kwa uzuri wake wa asilia ambao hata Adam alikuwa amechachawa nao na kukubaliana na ukweli kwamba picha zilizotumwa zilikuwa za Resh kweli.
---------------------------------------------------------------------------------
Bi Gaudensia alifika Dar-es-salaam majira ya saa tatu usiku,bado alikuwa hajaridhika kumaliza siku yake bila kuongea na mwanae,hivyo punde tu baada ya kuingia chumbani mwake aliamua kujaribu kupiga namba za simu za Reshmail ambazo zilikuwa hazipatikani siku nzima. Furaha aliyoipata ilikuwa haisimuliki,pale simu ilipoita upande wa pili"Mh! kalala nini huyu?" alijiuliza simu ilivyoita kwa muda mrefu bila kupokelewa,lakini mara ikapokelewa
"Helow! samahani Reshmail amelala" sauti ya kiume ilijibu baada ya kupokea kisha simu ikakatwa na kuzimwa. Mama Resh hakuamini kuwa amesikia sauti ya kiume katika simu ya mwanae alidhani amekosea namba lakini alipohakikisha zilikuwa zenyewe,wivu mkali ukamshika,akajaribu kupiga mara nyingi lakini bado hali ilikuwa ileile simu ilikuwa imezimwa usingizi ulipaa,alitokwa na jasho,hisia mbaya zikamvuruga na kufanya kichwa chake kiume sana,mama huyu alikuwa amejisahau kabisa kuwa Reshmail ni mwanae wa kumzaa, alizurura kama mtu anayetafuta kitu ambacho amesahau alipokiweka pale chumbani,alitamani kupiga kelele lakini aliamini hazitasaidia kitu.
---------------------------------------------------------------------
Reshmail akiwa usingizini Adam pembeni yake,yeye(Resh) alikuwa hoi kwa uchovu wa safari na misukosuko yote waliyopitia,na alipomaliza kuoga tu na kupata chakula alisinzia,hata simu yake ilipoita hakuisikia hata kidogo na hata angeisikia asingeweza kunyanyuka kupokea "Resh ni kipetito anapiga" Adam alimuuliza Resh aliyekuwa hoi kitandani."Ah! ni rafiki yangu mwambie nimelala" alijibu kwa taabu akiwa hata hajui anachokiongea. Naye Adam bila kugundua kwamba Resh hajui anachokisema na ile namba ni ya mama yake Resh alipokea na kuzungumza
Kitendo cha Adam kumkuta Reshmail akiwa bado ni bikra kilimzuzua sana,mapenzi yake kwa Halima yalipungua sana na kuisha kabisa hatimaye. Siku tatu mfululizo walizotumia pale Millenium Hotel zilitosha kuvunjilia mbali penzi la Adam na Halima na kujenga penzi imara kati ya Adam na Reshmail.
"Mwezi wa pili uje ujitambulishe nyumbani Adam yaani siwezi kusubiri kwa kweli nakupenda Adam wewe ni mwanaume wangu wa kwanza na ninakuahidi nitajitunza kwa ajili yako" Reshmail alikuwa anamsisitiza Adam siku alipokuwa amewasindikiza uwanja wa ndege tayari kwa wawili hawa kurejea Arusha shuleni.
"Mama anapiga! Eve" Resh alimwambia Eve pale simu yake ilivyoita."He! usiniambie huyo ndio mama,sasa mbona ulikubali niongee nae usiku ule? aliduwaa Adam.
"Eti! uliongea nae? Yesu wangu!" alishtuka Resh lakini Eve akamshauri azime simu kwanza mengineyo watajua mbele kwa mbele naye Resh akatii amri hiyo haraka akaizima simu bila kupokea Resh kwa kiasi kukuwa alikuwa amemzoea na kumwamini Eve.
Adam,Resh,na Eve waliagana kama watu waliofahamia na kukaa pamoja siku nyingi sana,Resh alimkumbatia Resh alimkumbatia Adam kwa muda mrefu hadi Eve alipowatenganisha na kuambiana Kwaheri.
---------------------------------------------------------------------
Ilikuwa imebaki miezi minne wafanye mtihani wa kumaliza kidato cha tano,Resh akiwa amekolea katika penzi la Adam na kusahau kuhusu
Mama yake ambaye alikuwa amezuiwa na mwanaye huyo kwenda pale shuleni kumsalimia kwa madai kwamba yeye(Reshmail) anataka ajikite zaidi katika masomo. Reshmail kwa maksudi akabadilisha namba yake ya simu ili mama yake asiweze kumpata mara kwa mara badala yake muda mwingi akawa anawasiliana na Adam.
Mwezi wa pili ilikuwa ni likizo ya mwezi mzima kwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita na pia wakati huohuo wanafunzi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino huwa katika mapumziko mafupi baada ya kumaliza muhula(Semister) ya kwanza. Kwa Reshmail ulikuwa wakati muafaka wa kumtambulisha Adam kwa wazazi wake jambo ambalo aliamini lingesaidia kupunguza makali ya mama yake. Tangu akiwa mtoto kamwe hakuwahi kuwakwaza wazazi wake kwa sababu ya wanaume hata siku moja hivyo alitegemea hawatampinga.
Ilikuwa siku ya furaha kubwa sana kwa Bi. Gaudencia na familia yote kwa ujumla kumwona tena Reshmail nyumbani baada ya miezi mingi tena akiwa mwingi wa furaha. Lakini tofauti na mama yake alivyofikiria kwamba mwanae huyo anafurahia kurudi katika ulimwengu wao wa mapenzi haramu yeye(Reshmail) alikuwa anafuraha ya kumtambulisha Adam ndani ya siku chache.
Kwa kujua wazi kabisa mama yake atachukizwa na maamuzi yake hayo,Reshmail aliamua kulifikisha hilo mbele ya Mzee. Manyama ambaye ni baba yake.
"Kwa sababu ni uchumba tu na hakupeleki popote hamna tatizo hata kidogo,mlete tu mwanangu mlete una maamuzi mazuri sana sio kama wasichana wengine wanafanya upuuzi kimyakimya mambo yanapokuwa mabaya ndio wanasema" alijibu mzee.Manyama huku akimshika mwanae huyo shavuni,Resh akatabasamu na kumkumbatia baba yake "I love you dad(Nakupenda baba)" Resh akamwambia kwa furaha tele mzazi wake huyo,huku moyoni akijiaminisha kwamba hapatakuwa na kikwazo tena kwa mama yake kwani baba ndiye kichwa cha familia.
Baada ya siku tano Adam aliwasili ndani ya kasri la mbunge huyu.Alikuwa anaogopa na hakuamini kama angepokelewa na kama angepokelewa alijua yatakuwa mapokezi mabaya sana kwani katika simulizi mbalimbali anazozisikia kwa watu zilimwonyesha kwamba ni vigumu sana kwa wazazi kumwelewa mtoto wa kike linapokuja suala la kumtambulisha mwanaume kama mchumba wake.
"Da Rosemary nina hofu mie" Adam alimwambia dada yake kipenzi waliyekuwa wameongozana naye "Acha uoga bro mbona hata sisi babu yetu alikuwa chifu? kwani chifu na mbunge nani zaidi" alitania Rosemary kumwondoa hofu kaka yake.Mapokezi waliyoyapata kutokea kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo yaliwashangaza mno waliwakuta watu wa kuwapokea na kwenda nao kwenye gari mbili walizokuja nazo,waliwafikisha hadi getini ambapo kina dada wawili kwa heshima kabisa waliwaongoza hadi sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao,japo usoni waliuficha mshangao wao lakini moyoni uliwajaa tele.Adam akiwa ndani ya suti nyeusi wanazotumia wanasheria katika shughuli zao na Rosemary aliyevaa suti pia walielekezwa wapi walipo wazazi wa Reshmail wakaenda kutoa salamu zao,ilikuwa ni hafla kubwa sana ndugu,jamaa na marafiki wapatao miamoja walikuwa wamealikwa na mheshimiwa huyu. Ilikuwa kama harusi kwa asiyejua lakini ulikuwa utambulisho tu.
Bwana na bibi Manyama walipendeza kwelikweli na walikuwa na kila haki ya kuitwa wakwe na Adam. Furaha ya Bi. Gaudencia ilificha chuki aliyokuwa nayo moyoni dhidi ya Adam kwa kumchukua mwanae ambaye ndio alikuwa anampa raha zote za dunia.
Hadi hafla inafikia tamati majira ya saa mbili usiku kila mtu alikuwa amepata furaha kubwa sana,wabunge na madiwani ambao ni marafiki wa karibu wa Manyama walitoa zawadi nyingi kwa wawili hawa huku babu yake Reshmail akitoa mawaidha yenye maana kubwa sana katika maisha waliyotarajia kuyaishi Reshmail na Adam siku za usoni.
Mzee Manyama kwa ombi la mwanae aliwasiliana na wazazi wa Adam kuwa muda wa mapumziko ya siku tano alizobakiza Adam amalizie katika familia yake,hapakuwa na kinyongo wala kipingamizi chochote walikubali kwa moyo mmoja na Adam akaendelea kuishi pale huku dada yake akirejea Mwanza kwa usafiri wa ndege ambao gharama zote zilikuwa juu ya mheshimiwa Manyama. Kila alipowasiliana na wazazi wake Adam hakusita kuelezea upendo wa kipekee anaoupata kutoka familia ya Reshmail hata wao walifarijika sana.
---------------------------------------------------------------------
Ilikuwa jumapili moja tulivu sana baada ya kutoka kanisani familia yote akiwemo pia Adam,baba yake Reshmail aliongozana na mwanae kwenda mjini kwa lengo kuu la kuonana na walimu mbalimbali wa masomo ya ziada(Tution) watakaompendeza Reshmail basi waweze kumfundishia nyumbani.
Huku nyuma alibaki Adam pamoja na mkwewe (Mama Reshmail) baada ya kupata kifungua kinywa Adam alimwaga mkwewe kuwa anaenda kuzungukazunguka bustanini "Tena nilitaka nikwambie leo unataka uondoke hata bustanini hujawahi kufika,afadhali nenda mwanangu" alijibu mama Reshmail.
Ulikuwa mpango kabambe uliosukwa na Bi. Gaudencia,kwa dhumuni kuu la kumwondolea mamlaka Adam ya kuwa na Reshmail. Kwa kuwatumia vijana kutoka katika ngome ya vigogo,ngome maalum iliyokuwa inatumiwa na watu wenye pesa zao kwa ajili ya kuwatenda vibaya watu wanaoonekana kuingilia mambo yao aidha kimapenzi au kibiashara.Alipoaga anaenda bustanini Gaudencia alitumia fursa hiyo kupiga simu kwa wanaume hao wa shoka ambao tayari alikiwa ameelewana nao bei.
"Ndani ya dakika tano tutakuwa hapo” ndio jibu lililotolewa upande wa pili
Bila kuongezea lolote Bi.Gaudencia alikata simu yake na kutoka nje.
"Babu kwa mama Veneranda si unapajua?" alitoa swali hlo Bi. Gaudencia kwenda kwa mlinzi wao wa getini.
"Ndio si yule mama anayesuka pale mbele"
”Hapo hapo haya haraka nenda kaniangalizie kama kuna foleni kubwa" aliamrisha Bi. Gaude na mlinzi akatii amri hiyo haraka haraka akaondoka katika lindo lake akaenda kutimiza amri ya bosi wake.
Baada ya dakika takribani kumi alirejea mlinzi yule "Yupo mmoja tu anamaliziwa" alileta taarifa hiyo kwa furaha.
"Haya mi ninatoka nimemwacha Adam ndani amelala akiamka mwambie nimetoka kidogo" alisema mama Reshmail huku akiondoka.
“sawa bosi nitamwambia”
Masaa mawili badae alirejea akiwa amesukwa tayari nywele zake,ni muda huohuo Reshmail na baba yake walikuwa wametoka mizungukoni,walimkuta Gaudencia anatokea ndani. "Babu Adam alivyoamka ameenda wapi? au bustanini?"Aliuliza Gaudencia na kuongezea "Maana nimegonga chumbani kwake kimya,hebu Reshmail ingia ukamwangalie ndani mwake humo huenda amelala bado" kwa mwendo wa maringo lakini harakaharaka Reshmail alijongea ndani.
"Babu unasema Adam hajatoka?" Resh aliuliza baada ya kurejea akiwa na hofu kidogo usoni.
"Hajatoka na mimi hapa sijatoka tangu mama alipoenda kusuka na kumwacha Adam amelala" alijieleza mlinzi yule jibu lililopokelewa kwa furaha na Bi.Gaudencia.
Jambo gumu zaidi kwa ambao hawakujua janja ya mama huyu ni kwamba simu ya Adam ilikuwa haipatikani hali hiyo ilileta wasiwasi sana,walisubiri huenda atarudi hadi jioni hali ilikuwa tete ndipo mzee Manyama alipoamua kupiga simu kituo cha polisi maeneo ya jirani kwa sababu alikuwa mbunge msako ulianza usiku huohuo.
Siku tatu zilipita bila taarifa yoyote kutoka katika kituo cha polisi,Reshmail alikuwa amepooza sana kupita maelezo mara kwa mara alimpigia baba yake simu na kuuliza kulikoni lakini jibu bado lilikuwa lilelile kuwa hajapatikana.
"Mama niache tafadhali,tena niache nasema upuuzi wako siutaki tena niache!" alifoka Reshmail pale mama yake alivyomkuta amekaa sebuleni na kujaribu kumpapasa huku akimpa pole ya kupotelewa na Adam wake ghafla.
"Mwanangu usiwe na hasira kiasi hicho polisi watafanikisha upelelezi na watamrejesha Adam akiwa mzima wa afya" alibembeleza Bi. Gaudencia lakini Reshmail hakujibu kitu akajiondokea akiwa ameuvuta mdomo wake sana.
Siku ya tano polisi waliopewa jukumu la kufanya upelelezi huo walirejea na taarifa yao huku wakiambatana na ushahidi. Zilikuwa nguo aliyokuwa amevaa Adam kwenda kanisani ikiwa na matundu sita ya risasi na ikiwa imetapakaa damu pote,suruali ilikuwa na matundu matatu ya risasi.
"Hapana hawezi kuwa Adam hata kidogo nasema hawezi kuwa yeye" alifoka Manyama huku akiwa wimawima mbele ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai jiji la Dar-es-salaam Chacha Boniphace au maarufu kama Chacha B.
"Mheshimiwa lakini huu ni upelelezi wa awali tunaendelea zaidi na zaidi tutazidi kutoa taarifa kadri tunavyopata majibu mapya" alijieleza kwa utulivu bila wasiwasi kabisa jambo ambalo kidogo lilirejesha amani ya Manyama japo hofu tayari ilishaukumba moyo wake kwamba huenda Adam ameuwawa tena kikatili.
Ilikuwa ni shughuli pevu kwa Reshmail kuamini kile ambacho alikuwa anaelezwa na baba yake kwamba Adam anadhaniwa kuuwawa kwa risasi nane kisha mwili wake hauonekani. Bi. Gaudencia tayari alikuwa anaangua kilio kikubwa hata kabla maelezo hayajaisha ikawa kazi kwa mumewe kumbembeleza.
"Mke wangu Adam hajafa ila inadhaniwa pia upelelezi bado unaendelea jamani,ukilia hivyo unakuaribisha msiba mama watoto sawa" alibembeleza mzee Manyama huku amemkumbatia mkewe.
"Baba haiwezekani baba haiwezekani nguo za Adam zipatikane katika hali hiyo halafu mnasema hajafa,jamani Adam wangu wamemuua" alipiga mayowe Reshmail ikamlazimu mzee Manyama kufanya kazi mara mbili jambo ambalo lilimtoa jasho mzee huyu.
"Reshmail mwanangu,tulia hiyo siyo taarifa rasmi jamani ni majibu ya awali mbona mnanifanyia hivyo au mnataka nipate presha nife?" alijieleza Manyama huku akijifuta jasho kwa kutumia shati lake. Reshmail mbio mbio akaondoka pale sebuleni akaanza kuzipanda ngazi kuelekea chumbani kwake huku akilia,mzee Manyama nae huyo nyuma yake.
"Reshmail mwanangu,njoo malkia wangu,njoo mwanangu" aliyazungumza hayo huku akimkimbiza kwa nyuma. Wakati huo Bi. Gaudencia tayari alikuwa amenyamaza kimya kabisa,akijaribu kupikicha
macho yake.Reshmail hakusimama hadi chumbani kwake akajifungia,baba yake alibembeleza mpaka akachoka hakupata jibu zaidi ya kilio cha kwikwi kutoka ndani.
"Baba Resh twende chumbani mume wangu,twende utakaa hapa hadi saa ngapi cha msingi tumwombe Mungu asije akajidhuru mwanetu" Gaudencia alimnyanyua mumewe wakajikongoja kuelekea chumbani kwao,Manyama akiwa amelegea kabisa.
Asubuhi ya siku iliyofuata naibu waziri wa ulinzi na usalama,alifika na msafara wake wa magari matano kwa mbunge Manyama kuja kutoa pole ya kutokewa tukio hilo lenye utata kwa mwenzao. Shughuli ngumu iliyokuwa mbele yao ni jinsi gani watawaeleza wazazi wake Adam ambao hadi dakika hiyo waliamini Adam yupo salama na mwenye furaha kwa mchumba wake Reshmail,Manyama alimuomba waziri ashughulikie hilo suala na bila kupoteza muda alinyanyua simu yake ya mkononi na kutoa taarifa hiyo kwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mwanza pamoja na mawasiliano anayoweza kumpata baba yake Adam. Ilikuwa vigumu sana kwa baba Adam kuelewa anachoelezwa lakini kwa kadri ya uwezo wake na taaluma yake mkuu huyo alifanikiwa kumwelewesha ambapo baba yake Adam aliondoka akiwa na matumaini kwamba ipo siku Adam atapatikana.
Nyumba nzima ya kina Adam ilipooza sana dada yake Adam (Rosemary) alikuwa analia muda wote kwa uchungu hakuamini kwamba siku ile pale uwanja wa ndege alivyosindikizwa na familia nzima ya mhe.Manyama ndio ilikuwa mara ya mwisho kumwona kaka yake kipenzi(Adam).
Uongozi wa polisi uliifikisha taarifa hiyo pale chuoni ambao pia walipokea kwa simanzi kubwa.
"MAUAJI YA KUTISHA", ndivyo mandishi meusi kabisa kwenye magazeti mbalimbali yalisomeka,hali hiyo ilithibitisha kabisa kuwa Adam hayuko hai tena. Picha yake iliyoambatanishwa na habari hizo akiwa na mtoto wa mbunge iliteka na kuumiza mioyo ya watu wengi hasahasa vijana."Tumempoteza mwanasheria" ndilo neno la pamoja walilosema wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino Mwanza katika misa ya pamoja kumwombea mema Adam kama yupo hai au kumtakia pumziko jema la milele kama tayari Mungu ameichukua roho yake,kila uso ulikuwa na simanzi kubwa ilikuwa kama tamthilia.
Reshmail alikuwa kama zezeta,hamwelewi mtu yeyote,roho yake ilimwambia kwamba mama yake mzazi anahusika kwa namna moja au nyingine katika tukio hili lililojaa utata. Lakini ataanzia wapi kumweleza baba yake,atajisikiaje mzee Manyama akigundua kwamba mke na mtoto wake walikuwa katika ndoa haramu ya siri ndani ya nyumba yake."Hapana sitaki kuongeza tatizo juu ya tatizo nitasubiri liwalo na liwe,kama Mungu alimpanga Adam awe wangu naapa sitaolewa na mwingine kamwe,lakini kama hakuwa halali yangu basi ataletwa mwanaume duniani kwa ajili yangu tena"Alijipa ujasiri wa hali ya juu Reshmail huku akijipigapiga kifuani."Nitarejea shule na nitasoma tena kwa bidii sana,sitamwaza mwanaume yeyote tena alikuwa Adam na atabaki kuwa Adam hadi Mungu aamue tena" aliendelea kujipa matumaini."Bibi yangu aliniambia maneno ya mdomo huumba halisi,na nina uhakika ninachokiongea kwa mdomo wangu Mungu ataniumbia" aliendelea kuongea huku machozi yakifumba macho yake na kitambaa alichokuwa anatumia kujifuta kilikuwa kimelowana tayari kwa wingi wa machozi alikuwa kama yatima vile,Resh alikuwa akifungasha baadhi ya mizigo yake tayari kwa kurejea shuleni tena,tangu tukio la Adam kupotea hakuna aliyetegemea hata siku moja Resh atawaza kurudi tena shuleni kwani waziwazi akili yake ilionekana kuathirika kwa kiasi kikubwa kwa kumpoteza Adam katika mazingira yasiyoeleweka.
"Baba kesho narejea shule si unajua tayari shule imefunguliwa?" Reshmail alimkurupua mzazi wake huyo kutoka alipokaa kwa mshangao
"Umesema nini malkia wangu!" alihoji Manyama huku akiwa wima
"Narejea shule kesho" kwa msisitizo na tabasamu alijibu Reshmail. Mzee Manyama hakuamini kwani alikuwa akiwaza ni namna gani atamshawishi mwanae aweze tena kurejea shuleni baada ya matatizo yote yaliyojitokeza kwa mchumba wake Adam ambaye hadi wakati huo bado mwili wake ulikuwa haujapatikana wala taarifa yoyote zaidi ya nguo zikiwa na matundu ya risasi na damu."asante sana mwanangu nakupenda sana" mzee Manyama aliongea kwa furaha huku akimkumbatia mwanae.
Tangu kupotea kwa Adam aliyehisiwa kuwa tayari amekufa kulipokelewa kwa hisia tofauti na wananchi huku asilimia kubwa ikiegemea upande wa imani potofu za kishirikina wakihusisha tukio hilo na utajiri alionao Mh. Manyama na uchaguzi uliokuwa mbele yake.
------------------------------------------------------------
"Wamemtoa mwanangu kafara ili waongeze utajiri,nilimwambia Adam aoe msukuma mwenzake ona sasa,watoto wa siku hizi wabishi wanajifanya wanajua sana na elimu yao inawadanganya" mama yake Adam alikuwa analaani vikali mbele ya mume wake wakiwa ndani ya nyumba yao maeneo ya Igoma kwa 'one-way'
"Usiseme hivyo mama Adam kumbuka sisi ni wakristu,tumwachie Mungu yeye ndio atajua nini cha kufanya" Babaye Adam alimtuliza mkewe huku akimgongagonga mgongoni kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kuume.
Mawasiliano baina ya familia hizi mbili ya Adam jijini Mwanza na ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamekatika licha ya baba yake Adam (mzee Michael) kutangaza kuwa kutoka moyoni mwake amesamehe yote yaliyotokea na anaamini ni mipango ya Mungu lakini kinyongo kilionekana dhahiri kwa matendo,upendo wa zamani haukuwepo tena jambo hilo lilimfadhaisha sana mzee Manyama kiasi cha kukondeana na kukosa umakini katika utendaji wake wa kazi jambo lililoishusha sana heshima yake kama mbunge aliyekuwa anaheshimika sana kuanzia bungeni hadi jimboni kwake,wapinzani walitumia fursa hiyo kumchafua hasahasa na kweli uchafu huo ukakubalika kwa wananchi kwa ujumla Manyama hakuwa na lake tena pale,wananchi walimpuuzia sana tofauti na zamani na hata hiyo miaka miwili iliyobaki wananchi waliiona kama ni mingi sana kuwa na kiongozi wa aina yake.
Kuliko fedheha yote hiyo Mh. Manyama kwa hiari yake mwenyewe alipitisha kura ya maoni ya wananchi kuhusu imani waliyonayo kwake kama mbunge wao. Asilimia 70 ya waliopiga kura walidai hawana imani naye huku asilimia kumi na nne tu ndio wakidai bado wana imani naye na kura zilizobaki zikiharibika,rasmi Manyama akawa ametolewa bungeni na katika uchaguzi mdogo uliofanyika akachaguliwa mbunge kutoka chama cha upinzani na maisha yakaendelea huku Mh.Manyama akiendelea na biashara zake mikoani.
-------------------------------------------------------------------------
Adam akiwa pale bustanini alivamiwa ghafla na wanaume wawili wa shoka wakiwa na bunduki,ishara ya kidole mdomoni ilimfanya atulie tuli kisha wakamwonyesha ishara kwamba awafuate alifanya kama walivyotaka hadi kwenye gari iliyokuwa imepaki pembeni kidogo ya nyumba yao Adam alishangazwa sana na ukimya uliokuwepo hakuwepo mlinzi wala mama mkwe wake.Safari yao ilikwenda mpaka Iringa gari iliyokuwa na vioo vyeusi 'tinted' ilimzuia Adam kujua ni wapi alipo,gari ilizimishwa ndani ya jumba kubwa sana ambapo alipelekwa kwenye chumba kikubwa tu,hofu kubwa ilimtawala hakujua kwa nini yuko pale,hakupigwa wala kupewa bughudha yoyote,hali hiyo ilzidi kumshangaza "au ndio wachuna ngozi" alijiuliza Adam kwa hofu tele.
Hayo ndio masharti ambayo mama Reshmail alitoa kwa vijana aliowapa tenda hiyo ya kumtorosha Adam pale nyumbani. Shida yake haikuwa kumtesa Adam bali kumweka mbali na mwana (Reshmail) ambaye alikuwa amempagawisha ipasavyo katika mapenzi ya jinsia moja.Suala la pesa halikuwa tatizo hata kidogo alichohitaji ni kutimiziwa alichotaka. Mkataba wa miaka mitano ndio alioingia na watu hawa kukaa na Adam bila kumruhusu kutoka nje ya jingo.Bi Gaudencia aliamini kwamba kwa kutokomea Adam mbele ya uso wa Reshmail ilikuwa fursa nzuri ya kurudisha tena uhusiano wake na Reshmail ambao ulikuwa unaelekea kufa lakini kinyume chake alikuwa ameibua chuki kubwa baina yake na mwanae “heri wote tukose kama ni hivyo” alijiapiza mama Reshmail baada ya kuona dalili za kumshawishi Reshmail hazipo tena
Alikuwa ni Reshmail mwingine kabisa mkasa uliomkumba ulimbadilisha sana na kuitanua akili yake sana,Eveline naye alisikitishwa na yaliyomkumba shoga yake akajitahhdi sana kuwa karibu naye kumpa moyo huku akijiepusha sana kufanya vitendo ambavyo vitamkumbusha Resh jinsi alivyoweza kukutana na Adam. Ni katika kujiepusha na kumkera rafiki yake huyo kipenzi Eveline akajikuta amefuta picha za uchi na filamu za ngono katika kompyuta yake akawa si mtu wa kutoroka shule,hakuwa tena mtu wa wanaume na hatimaye akawa Eveline wa kuigwa na wanafunzi wenzake jambo hilo liliwaduwaza sana wanafunzi pale shuleni lakini ndio hivyo Eve alikuwa amekubali mabadiliko katika maisha yake. Juhudi zao katika masomo ziliendelea kuwaweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri mtihani wao wa mwisho. Hawakuyazungumzia tena yaliyopita tena walijadili mapya na yanayowanufaisha "Eveline wewe ni kama dada yangu nakupenda sana"
"Nakupenda pia Reshmail umebadili maisha yangu moja kwa moja nina maisha mazuri sasa" alijibu Eva kwa upole huku akimwangalia Reshmail aliyekuwa anaishusha chandarua yake aweze kulala. Ni kweli walitokea kupendana wawili hawa.
"Hivi Resh una mpango bado wa kusomea uhasibu mi lazima niwe mhasibu"
"Mh! unavyojiaminisha utadhani tumefaulu tayari" alijibu Resh.
"He! mi najua sisi kufaulu kwetu sio swali ni jibu,swali ni je tunaenda chuo gani na kusomea nini." alijiaminisha Eveline.
"ok! nilidhani nitasomea uhasibu lakini kwa heshima ya Adam nitasomea sheria" alijibu Reshmail kwa furaha.
"Mh! na upole wako huo na mambo ya kutoa hukumu wapi na wapi? mwenzio naangalia ankara" alisema Eva.
"Wala hata siendi kuhukumiana naenda kwa heshima tu" alisisitiza Reshmail.
"Mh! haya mheshimiwa hakimu napenda kujitetea kama ifuatavyo" Eve alitania akifuatiwa na kicheko kikubwa kutoka kwa Reshmail.
------------------------------------------------------------------------------
Maisha yaliendelea vyema sana tu japo yalikuwa maisha ya mashaka Adam aliruhusiwa kuongea na kuuliza kila kitu kasoro swali moja tu "Kwa nini niko hapa?",ndio hakuruhusiwa kuliuliza hata kwa mbali,watu wote pale hawakuwa na ubaya nae hata kidogo,hawakumtesa,hakugombezwa wala hakufanya kazi,alipewa huduma zote za msingi,aliweza kutoka nje na kwenda bustanini lakini nje ya geti hakuruhusiwa. Tayari aliyazoea maisha haya lakini kumbukumbu ya jinsi alivyochukuliwa ndani ya jumba la wakweze bila kupata msaada wowote ule "Nani atakuwa nyuma ya haya yote mlinzi alikuwa wapi? Mama Resh je?" alijiuliza sana bila kupata wa kumpa jibu.
"Hivi unaitwa dada nani vile?" Adam alimuuliza dada mmoja ambaye kila baada ya siku tatu alikuja kufanya usafi katika chumba chake.
"Naitwa Beatrice Cosmas niite Bite" alijibu huku anafuta vioo kwa dirisha la chumba cha Adam.
"Una jina zuri wewe mh!"Alisanifu Adam.
"Asante wewe ni Adam eeh!" aliongezea yule binti huku akiwa ameacha shughuli yake aliyokuwa anafanya.
"Ndio mimi ni Adam! samahani nikuulize maswali machache"
"Uliza tu lakini sitakujibu sasa hivi"
"Kwa nini?"
"We uliza yote ndo nitakwambia kwa nini"
"Hivi hapa ni wapi? kwa nani? na kwa nini nipo hapa?"
"Ndio hayo matatu tu?...sawa nitakujibu kwa sharti dogo sana yaani"
"Sharti gani hilo mi nipo tayari"alitoa uhakika Adam bila hata kulijua sharti lenyewe.
"Sikia Adam sina haja ya kuzunguka zunguka nina mwaka wa pili hapa kitu kinaitwa mwanaume katika mwili wangu ni kama ndoto sasa ni wewe wa kutii kiu yangu na mimi nitajibu maswali yako" alijieleza Bite,jambo ambalio lilikuwa zito na la kumshangaza Adam.
"Mh! au ndo mtego tena kutoka kwa Reshmail? dah! ikiwa hivyo nitaaibika kweli mimi"Alijiwazia Adam kwa mashaka makubwa kabla ya kujibu.
"Basi utakuja kunijibu baadaye!" alisema Adam.
"Haya usiku na wewe jiandae" alijibu na kuaga Bite.
Hayawi hayawi mara yakawa usiku wa saa tatu,Bite tayari ndani ya chumba cha Adam ndani ya khanga moja peke yake.
"Haya nipe nikupe hakuna longolongo hapa" alizungumza Bite.
"Subiri taratibu basi,sikiliza" alianza kujitetea Adam wakati Bite anajisogeza kitandani,Adam alikuwa amechelewa tayari joto la Bite lilipenya katika mwili wake na kumchanganya hadi kujikuta akifanya kinyume na alivyotarajia kwamba atafanikiwa kutegua mtego wa Bite badala yake alikuwa ameshafanya mapenzi na Bite. Kwa Bite ulikuwa ushindi mkubwa sana kwani tangu aletwe hapo kuwa msaidizi wa kazi za ndani ya vyumba hakuwahi kutoka nje ya jengo hilo,sio kwamba alikuwa amefungwa hapana kila kitu kilikuwepo ndani kila siku pia alikuwa ameridhika kuwa hapo.
"Hapa ni Iringa,nimejibu swali lako la kwanza tuendelee tena nikujibu swali la pili na tatu" alisema Bite kwa shauku kubwa sana.
"Hapana Bite imetosha kwa leo sijisikii vizuri,siku nyingine basi sawa!" alidanganya Adam na Bite hakuwa mbishi akambusu Adam shavuni akajiondokea zake.
Ilimchukua takribani siku tano Bite kugundua kwamba tayari ameshika ujauzito jambo ambalo halikuruhusiwa katika jumba hilo na alipewa onyo kali wakati anaingia hapo. Kwa usalama wake na Adam alifikiria suala la kutoroka lakini haya yote aliyafanya baada ya kuongea na Adam na kumweleza hali halisi. Ni katika wasaa huo alimweleza Adam chanzo ambacho kinaweza kuwa kimemsababishia yeye kuwepo pale "Umemchukulia kigogo mpenzi wake,umemendea mtoto wa kizito au umemkataa kimapenzi mtu maarafu" hizo ndizo zilikuwa baadhi ya sababu alizoorodheshewa na Bite,lakini kwake yeye aliona hakuna hata moja inayomuhusu kwani wazazi wote wawili wa Reshmail walimpenda sana hakuwa tayari kuweka hisia kwamba pengine moyoni wanamchukia.
"Usijali lakini hutakaa milele humu,huwa unafika
Muda aliyekuweka humu akiridhika unatoka.
"Nitamlea mtoto,napenda watoto hata kama usipokuwa mpenzi au mume wangu nitampenda sana na nitamwita....."
"Christian akiwa mvulana au Christina akiwa msichana" alidakia Adam ambaye kwa mbali alianza kumtamani Bite kimapenzi.
------------------------------------------------------------------------------------------------------
Biashara za baba yake zilikuwa zinaendelea vizuri na skendo lake lilikuwa linafifia taratibu. Hadi anamaliza kidato cha sita Reshmail mapenzi kwa wazazi wake yalikuwa palepale na japo hakutaka kumwongelea Adam jena alikuwa na picha yake waliyopiga pamoja siku moja kabla ya tukio lile la kushangaza na kuumiza. Reshmail kwa ruhusa ya wazazi wa Eveline alienda nae mpaka kwao ambapo walikaa wote kwa siku tano kisha akarejea tena Arusha. Urembo wa Reshmail ulipagawisha kila mwanaume na hata baba yake ilifikia kipindi akakiri kwamba kweli pale alizaa mtoto mmoja wa kipekee na kweli alikuwa wa kipekee. Mama Resh bado alikuwa na matamanio lakini kwa ssa alimwogopa sana Reshmail tofauti na miaka mingi iliyopita.
"Baba na mama wiki ijayo nataka kwenda Mwanza kwa wazazi wa Adam" Resh alitoa hoja yake wakiwa mezani wanakula.
"Wapi? Mwanza! hawatakuelewa mwanangu utakuwa kwa maksudi kabisa unafufua shari iliyopoa tayari.
Tayari"Kwa busara tele na upole mzee Manyama alimweleza mwanae ambaye pia aliyapokea kwa nidhamu ya hali ya juu na kichwa chake kuyakubali kuwa yana maana kubwa ndani yake."Nimekuelewa baba sitaenda tena" alijibu kwa unyenyekevu sana Reshmail.
Muda mwingi wakati anasubiria matokeo aliutumia kuimba na kusikiliza muziki na mara chache sana kwenda kutembelea rafiki zake walioishi jirani naye.
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Matokeo ya kidato cha sita yalipotoka hayakuwa ya kushangaza sana kwa upande wake kwani alikuwa amevuna alichokipanda. Reshmail alikuwa amepata daraja la kwanza na ndivyo alivyotarajia,furaha yake iliongezeka baada ya kumwona katika orodha Eveline Maige rafiki yake kipenzi naye akiwa amepata daraja la kwanza huku wakitofautiana pointi kadhaa. Akiwa anajiandaa kumpigia simu tayari simu yake iliwakawaka na kuandika "pacha" jina ambalo alikuwa amemwandika Eve katika simu yake,badala ya kuongea wote kwa pamoja wakaanza kucheka,walicheka sana hadi simu ilipokatika. Zilikuwa ni furaha kutoka moyoni,kwa nini wasifurahi wakati ndoto zao zilikuwa zinatimia?
Tanzania Commission of Universities (T.C.U) ilipotoa uchaguzi wa kwenda vyuoni Reshmail kama alivyopenda alichaguliwa chuo kikuu cha mtakatifu Augustine Mwanza kwa masomo ya sheria huku Eveline Maige akipelekwa Mzumbe chuo kikuu kwenda kuchukua masomo ya uhasibu shahada ya juu.
"Ndugu hakimu naomba kujitetea!" Eve alimtania Resh utani wao wa shuleni siku walipokuwa wanaagana.Walikuwa wametenganishwa hatimaye lakini mawasiliano yao yalidumu
Kama alivyojiwekea kiapo chake cha kutopenda hovyohovyo ni hivyohivyo alivyoingia pale chuoni,hakuringia uzuri wake lakini hakutaka pia usumbufu unaopitiliza kutoka kwa wanaume yaani kwa kifupi alikuwa na msimamo mkali sana,ni rafiki yake (Eve) pamoja na wazazi wake ambao wangeweza kubashiri sababu hasa inayomfanya binti huyu awe hivi na si mtu mwingine pale chuoni.
Maringo yake yalifichwa na werevu wake darasani,kwani ilikuwa ni warembo wachache sana wa aina yake waliofanya vizuri kimasomo,jambo hilo lililowavutia waalimu wengi sana na wanafunzi ambao wanapenda maendeleo kimasomo. Reshmail hakuwa mtu wa mambo mengi hakunywa pombe wala kwenda kumbi za starehe usiku starehe yake ilikuwa ni kusoma na michezo.
Mnamo mwezi wa pili michezo ya FAWASCO ilipoanza michezo hiyo inayohusisha vitivo vyote pale chuoni,kwa maksudi alichaguliwa kuwa mhamasishaji kwa wasichana wajibu alioufanya vizuri ipasavyo na kikubwa zaidi akawa pia mdhamini mkubwa sana. Moyo wake wa kujitolea uliwavutia sana wanadarasa wenzake ambao baadhi walimpenda huku wengine wakidai ana maringo, msimamo wa Reshmail ulibaki palepale.
Mwaka wa pili pale chuoni ndio ulikuwa mbaya kwake. Darasa walilolitumia mwaka wa pili wanafunzi wa kitivo cha sheria,lililojulikana kama Mombasa Raha kwa mbele lilikuwa na picha kubwa sana ya Adam ambayo ilikuwa pembeni ya ubao wa kufundishia hiyo ikimaanisha kwamba kila atakapoingia darasani lazima aione,"ADAM THE GREAT" yaliandikwa maandishi haya chini ya picha kubwa ya Adam. Amani,ikatoweka kabisa moyoni mwake kumbukumbu mbaya za kumpoteza mpenzi wake Adam zikaanza kumrejea kwa kasi sana.Reshmail akaanza kujihisi yeye ndiye chanzo cha yote hayo,tofauti na waalimu wake hakuna mwanafunzi aliyemfahamu Adam zaidi ya kujua tu historia ya yaliyomkuta na wengi kuichukulia kama simulizi tu ya kusadikika. Reshmail alianza kuwa mtoro darasani na hata alipoingia badala ya kumwangalia na kumsikiliza mwalimu,mawazo yake yote yalivutwa na picha ya Adam yenye tabasamu pana mara zote aliamini inamuangalia yeye na kumlaumu kwa kumkatisha masomo yake kwa penzi la mtandaoni. "Adam stop blaming me!!(Adam usinilaumu)" alipiga kelele kwa nguvu Reshmail bila kujitambua,mwalimu alimshangaa na hakuelewa kilikuwa kimemsibu nini "Is she dreaming? (Anaota?)" aliuliza mwalimu Sijjo aliyekuwa anawafundisha somo la mawasiliano (Communication skills),darasa zima likacheka kwa fujo sana,lakini Reshmail alikuwa analia huku akitetemeka sana,kwa ghadhabu akasimama na kutoka nje. Japo ulikuwa ni mwezi mmoja tu tangu waanze masomo ya mwaka wa pili lakini
tabu na mateso aliyokuwa ameyapata yalitosha kumshawishi kuwa huenda amesoma hapo kwa miaka kumi.Wazazi wake hawakuwa na la kufanya,Eveline alibaki kumwonea huruma shoga yake huyu alijaribu mara kwa mara kumpigia simu lakini haikuwa tiba ya tatizo la Reshmail. Ni kweli Reshmail asingeweza kujilazimisha kuwa na furaha kwani ni yeye aliyemshawishi Adam awe nae kimapenzi na ni yeye huyuhuyu alimshawishi Adam aende kwao kwa ajili ya kujitambulisha na safari hiyo ikawa ya mwisho ya Adam. "Nikiwaambia waalimu wangu watanielewaje,na hata wakinielewa itakuwaje wanafunzi wenzangu wakijua siri hii? watajenga picha gani tena kuhusu mimi,mh! niepushe na hali hi bwana,kama uliweza kuniondolea mawazo haya hadi nikamaliza kidato cha sita vyema hebu baba na sasa ondoa tena na hili jaribu zito mbele yangu na jina lako lisifiwe." aliweka ombi fupi Reshmail katika mawazo yake hayo. Lilikuwa ni jambo gumu sana kwa Reshmail alikonda sana na punde si punde maneno ya wakosaji yakaanza tena "Mh! kumbe ndio maana anakataa wanaume kumbe anaishi kwa matumaini maskini,dada mrembo kama huyu" yalisikika maneno hayo katika vijiwe vya wanafunzi pale chuoni. Ilikuwa ni kero kubwa kila alipokatiza vidole vilimwelekea yeye umaarufu wake wa awali kwamba ni mrembo ukaongezeka maradufu karibia chuo kizima lakini wakati huu ilikuwa ni sifa mbaya kwamba ana virusi vya UKIMWI hata yeye aliyasikia maneno hayo yalikuwa yakivuma kwa kasi,hakuwa na uwezo wa kuzuia tetesi hizo "Wangejua kwamba mi ni bikra na wanayoyasema yote ni uongo,hata wasingenyanyua midomo yao michafu kuropoka upuuzi huo,lakini bila Adam watajuaje?" alijiuliza Reshmail akiwa chumbani mwake katika hosteli ya Ngulelo aliyokuwa amepanga chumba alichoishi peke yake. Marafiki zake taratibu wakaanza kumtenga wakiamini ameathirika,hilo halikumuumiza kichwa kwani alilitegemea sana hasa hasa dhana ya unyanyapaa kwa waathirika iliyokuwa inatawala chuoni hapo.
-----------------------------------------------------------------------------
Bite alifanikiwa kutoroka katika ngome ile kubwa aliyokuwa amehifadhiwa Adam. Kwa jinsi alivyokuwa amezoeleka pale haikumchukua muda mrefu kumshawishi mlinzi amfungulie geti atoke kidogo na ndio ikawa jumla hakwenda mbali sana na mkoa wa Iringa bali aliweka kambi yake maeneo ya Uyole Mbeya mkoa uliopo jirani na Iringa ambapo kipesa kidogo alichoondoka nacho pale ndani alifungua kibanda chake sokoni na kupanga nyumba eneo jirani la Igawilo akianzia maisha ya kulala chini hadi aliponunua godoro.Biashara ya kuuza nyanya
na mbogamboga ilimkimu sana maisha yake kwani wazo wala tegemeo lake halikuwa kununua gari,au kujenga nyumba hapana lengo lake lilikuwa uhai pekee,na shilngi elfu moja alizozipata zilikuwa zinamtosha kabisa. Alikuwa mchangamfu na mstaarabu sana,wateja walivutika kwake kwa kasi kufaidi ukarimu wake katika biashara.Tumbo lake lilianza kukua taratibu,kina mama sokoni wakaanza kuhisi tayari Bite kapata mjanja Mbeya amemjaza mimba,lakini miezi yake ya kujifungua ndiyo ilifungua akili za waliokuwa na maswali na kugundua kwamba ile mimba alikuja nayo pale na sio kwamba aliipatia pale. Salama bin salmin Bite alijifungua mtoto wa kiume miezi tisa ilipowadia.
"Mh! baba yake atafurahi tena alimpa jina pale tu nilipomwambia nimeshika mimba" Bite kwa furaha tele aliwaambia kina mama wa pale sokoni,akiwemo jirani yake mama wawili,ni hao ndio walikuwa ndugu zake."Hongera Bite,sijui ndio unakuwa mama nani vile" Bite alihojiwa na mama wawili
"Mwanangu anaitwa Christian" alijibu Bite huku akibusu kichanga chake hicho ambacho kilikuwa kinarusharusha miguu na mikono yake huku na huko.
Christian alizaliwa akiwa na afya tele na hakusumbuliwa na magonjwa wakati wa ukuaji wake mwaka wa kwanza,ilikuwa furaha kubwa kwa mama yake.
----------------------------------------------------------------------------
Miaka ilizidi kukatika wazo la Bi. Gaudencia kumtoa Adam katika jumba lile lilikuwepo kichwani mwake kwani udhaifu alioupata Reshmail pamoja na kashfa mbaya anazozipata pale chuoni zilimsononesha sana lakini ataanzia wapi kuificha aibu yake pale ambapo Adam,akasababisha uovu wa mama huyu uwekwe hadharani. Ni jambo hilo lililomuumiza kichwa mama huyu. Reshmail na baba yake watanielewaje kwa mabaya niliyowafanyia,nimeishusha heshima ya mume wangu aliyekuwa na heshima kubwa bungeni" alizidi kuwaza
Huku Iringa maeneo ya Ruaha Adam alikuwa anauanza mwaka wa tatu,akiishi kama nyumbani kwake,lakini hakuridhika hata kidogo maisha hayo ya ufungwa. Miaka mitatu ilikuwa mingi sana "Mama na baba yangu wanahisi niko wapi? vipi kuhusu mpenzi wangu Reshmail,hapana imetosha nahitaji kutoka hapa,lakini lazima nijiulize nitatoka vipi hapa katika ngome hii" alijisisitiza Adam japo ulinzi madhubuti ulioongezwa kutokana na kutoroka kwa Bite katika mazingira ya kutatanisha pale ngomeni
***
Mwaka wa pili uliisha hivyohivyo kimateso makali yaliyojawa na kumbukumbu mbaya na isingekuwa kuhamishwa kwa darasa la sheria mwaka wa pili kwenda katika maghorofa ya Mwanjonde chuoni hapo basi Reshmail angefeli vibaya masomo yake kutokana na msongo wa mawazo.
Akiwa mwaka wa tatu afya yake ilirejea tele kwani hakuwa akiiona tena picha kubwa ya Adam machoni pake hali hiyo ya afya kurejea ilizusha msemo mpya tena,tofauti na mwanzo walivyosema ana Ukimwi,sasa walisema "Akikonda ana virusi,akinenepa ameanza kutumia dozi" yote hayo alituhumiwa Reshmail lakini kamwe hakuwahi kuthubutu kunyanyua mdomo wake kujibu vijembe hivyo yeye alikuwa mkimya huku akipambana na masomo hadi alipoumaliza mwaka wake wa nne vyema.
Mnamo mwezi wa kumi na moja familia yake yote ilisafiri kuelekea jijini Mwanza kusheherekea kwa pamoja mahafali ya mtoto wao,Eveline ambaye tayari alikuwa kazini baada ya kuwa amemaliza miaka yake mitatu chuoni na kufaulu vizuri pia alijumuika katika kukamilisha furaha hii ya rafiki yake mpenzi huku akiongozana na mchumba wake Benjamin Simon. Reshmail alifurahishwa sana na ujio wa Eve kwani alizidi kudhihirisha kuwa ni kiasi gani yeye ni rafiki wa kweli.
Yalikuwa ni mahafali makubwa na ya kipekee kuliko yote yaliyowahi kutokea ambapo chuo cha Mt.Augustino kilifanya mahafali ya pamoja na matawi yake yote Tanzania,yaani Iringa,Mtwara na Tabora. Kwa ufupi yalikuwa yamefana.
Ni katika pirikapirika na pitapita za huku na huko
za sherehe hiyo ndipo Reshmail akiwa na Eveline ana kwa ana anakutana na familia ya Adam yaani baba na mama yake,aliwatambua kwa uwepo wa Rosemary yule mdogo wake Adam. Rosemary alikuwa ndio kwanza amehitimu shahada ya elimu katika chuo kikuu cha mtakatifu Augustino tawi la mtwara hivyo yeye na familia yake pia walikuwepo katika viwanja vya Raila Odinga kusheherekea mahafali yale."Mchawi...mchawi!" alianza kupiga kelele mama yake Adam wakati Reshmail akisogea taratibu katika eneo walilokuwepo kwa furaha "Uuuwii" alipiga makelele kwa sauti ya juu jambo lililovuruga usikivu katika eneo lile na watu kuanza kumwangalia yeye kama mtu aliyechanganyikiwa,Reshmail na Eve walikuwa wameganda tu na mama Adam akizidi kupiga kelele,jitihada za baba yake Adam kumtuliza mkewe hazikufua dafu,mara ghafla mama Adam akakurupuka akiwa na chupa iliyokuwa na soda ambayo haijafunguliwa bado na kwa kasi akaenda kumkabili Reshmail ambaye akili yake ni kama ilikuwa imesimama na umati uliokuwa umemkazia macho kwa kitendo cha kuitwa mchawi ulimzidishia hofu na fedheha kwake,Eve alimshika mkono Reshmail na kujaribu kumvuta watoke eneo lile lakini tayari mama Adam alishawafikia na kwa nguvu kabisa akaituliza chupa ile juu ya kichwa cha Reshmail palepale akaenda chini huku damu nyingi ikimtoka kichwani. Wanaume watatu akiwemo pia baba yake Adam walifika na kumbeba juu juu,mama Adam ambaye alionekana dhahiri kuwa bado hajaridhika na kipigo alichotoa kwa Reshmail kwani bado alikuwa anaangaza huku na huko kama palikuwa na silaha nyingine. Alikuwa kama mwendawazimu
Wengine walimbeba Rshmail ambaye joho lake la kipekee kabisa lilikuwa limechafuliwa vibaya na vumbi la uwanja wa mpirawa miguu wa Raila Odinga ambapo ndio sherehe zilifanyika. Hali ya sintofahamu ilitawala sherehe zile kwa takribani nusu saa nzima hadi Reshmail alivyoondolewa na familia yake kuelekea hospitali na mama Adam kutiwa katika nguvu ya dola
---------------------------------------------------------------------
Halikuwa jeraha kubwa sana nyuzi mbili zilipita katika kichwa chake kushona jeraha lile
“kwa nini mama mkwe wako akutende hivi” eve alimuuliza Reshmail akiwa pale kitandani
“ni haki yake hata kunipiga risasi mimi ni chanzo cha maumivu haya wanayoyapata” alijibu Resh huku akilazimisha tabasamu
“kwa hio hapa amenionea huruma sana mimi ni sawasawa na muuaji tena wa kukusudia na haki yangu ni kuuawa pia” aliendelea Reshmail huku akitoa tabasamu hafifu tena
“usiseme hivyo mamii sio wewe uliyetaka iwe hivyo ni Mungu pekee” aliongea kwa upole Eve huku akivibinyabinya vidole vya Reshmail
“mama mwambie baba afatilie mama mkwe asije kulazwa selo hata kwa saa moja hana kosa lolote” Reshmail alimwambia mama yake alipoingia katika chumba cha hospitali ya Agha khan aliyokuwaelazwa kwa ajili ya matibabu maneno hayo yalimshangaza sana mama yake aliyetegemea Reshmail atakuwa na hasira ya kutendwa vile mbele ya hadhara
Nafsi ilikuwa inamsuta sana mama reshmail,moyo uliomba msamaha lakini mdomo ulikuwa mzito sana kufanya hivyo. Hali hiyo ilimkondesha sana na kumkosesha raha ndani kwa ndani unene wake wa asili uliyafunika yote hayo na hakuna aliyejua jambo zito alilobeba mama huyu.
Kweli badala ya bwana na bibi Manyama kuegemea upande wa mashtaka ili mama Adam apewe adhabu la wao waliunga mkono kwamba Reshmail alikuwa na makosa mahakama ikatupilia mbali mashtaka hayo na mama Adam akawa huru,jambo hilo badala ya kurudisha undugu liliongeza chuki na uadui
“si nilikwambia ukabisha?? Kama hawajamtoa mwanetu kafara kwanini sasa wamekubali niachiwe huru??” mama Adam alimwambia mumewe jambo ambalo wakati huu hata yeye alikubaliana nalo kuwa motto wao mkubwa wa kiume(Adam) alitendwa vibaya na familia ya reshmail . kuamini kwa mzee Michael baba yake Adam ni sawa na familia nzima kuamini kabisa na sumu ya chuki ikamwingia kila mwanafamilia na kuwa aadui wakubwa wa familia ya mzee Manyama.
-------------------------------------------------------------------------------------------
Siku mbili alizokaa pale hospitali hakuja hata mwanafunzi mmoja kutoka pale chuoni kuja kutoa pole kwa Reshmail wote waliogopa wakiamini alikuwa mshirikina . Eve hakukubaliana hata kwa mbali na shutuma hizo kwani alimwamini sana Reshmail hivyo aliendelea kuwa pale hospitalini pamoja na mchumba wake kumuuguza Reshmail ambaye alitoka siku tatu baadaye.
“baba mimi nitaenda na Eve kwake nitakaa siku tano ndio nitakuja huko” Reshmail alimpa taarifa hiyo baba yake naye hakupinga kwani amani aliyokuwa nayo Resh akiwa na Eve ilikuwa kubwa mno hali iliyowapa faraja hata wazazi wake hivyo walimruhusu bila kusita.
Siku hiyohiyo walipanda ndege kwa gharama za mchumba wa Eveline aitwaye Benjamin Simon,kuelekea Iringa ambapo Eve alikuwa amepata ajira katika benki ya N.B.C tawi la hapo.
Maisha yao yalikuwa mazuri sana kwani Benny alikuwa mwalimu wa shule ya sekondari hivyo katika majukumu waliweza kusaidiana na upendo wa dhati kati yao ulipendezesha zaidi nyumba yao.Reshmail alivutiwa sana na maisha hayo na kumkumbuka sana Adam wake “laiti angekuwepo tungeishi hivi siku moja “ alijiwazia Reshmail wakati akiwaangalia Eve na Benny wakiwa kwenye kochi wamebebana kwa furaha huku wakitaniana
Ilikuwa jioni moja Reshmail na Eve wakiwa katika mizunguko ya hapa na pale mizunguko ambayo kwa namna moja au nyingine iliibua ghafla safari ya kuingia sokoni,waliingia hapo kununua matunda matunda,zilikuwa zimepita siku tano na tofauti na alivyowahaidi wazazi wake hata hakuwa amefikiria kurudi Dar maisha ya Iringa yalikuwa yamempendeza sana .
“Eveline ona eveline jamani angalia kale katoto!!!” Reshmail alimgusagusa begani Eveline huku akimwonyesha kikundi fulani cha watoto pale sokoni
“wewe achana hao machokoraa walionikwapua pochi langu sina hamu nao hata kidogo,kisimu changu cha mchina na shilingi elfu thelathini zikapotelea hewani looh!! Wabaya hao” aliongea kwa hasira Eve huku akisitisha zoezi la kula chungwa aliliokuwa anafanya kwa wakati ule.
“mh!! Eve jamani achaga uongo yaani katoto kama kale jamani hebu kaone kale kadogo “Reshmail alizidi kusisitiza lakini Eve alionyesha bado ana uoga na uchungu moyoni wa kuibiwa vitu vyake na watoto aliowaita machokoraa
“Reshmail shauri zako vitakuliza hivyo we endelea kusema ni vitoto………..mh!! Resh lakini kale kadogo kazuri kweli” aliongea Eve alipokaona kale katoto ambako Reshmail alisisitiza sana.
“toto zuri jamboo!!”
“sijambo shkamoo!!” kalijibu katoto kale kwa uchangamfu sana baada ya Reshmail na Eve kukasogelea na kukasalimia.
“marahaba mtoto mzuri mbona upo hapa! Mwenyewe au hawa ni kaka zako?” Resh alimuuliza
“a a sio kaka zangu mi namsubiri mama ameondoka na watu wameenda huko amesema anarudi nimsubiri” alijibu tena kwa sauti ya kitotototo
“umekula??” aliuliza Eve.
“looh!! Eve hujaacha tu maswali yako ya kichoyo ya uchagani kwenu mh! Unataka aseme amekula ili umnyime au ?” Reshmail alimshushua Eve kiutani
“mh! Limeniganda shoga,una mashushu wewe!!” alijibu Eve kiaibuaibu huku akimpa yule mtoto chungwa lililokwisha menywa tayari.
“mama anarudi saa ngapi??” Reshmail alimuuliza yule mtoto tena
“sijui nimemsubiri hata hajaja amenipa chai tu akaondoka na wale wanaume wawili” alijieleza vizuri motto yule
“mh!! Mjini mjini tu katoto kanajieleza utadhani mtu mzima dah!” Eve alimnon’goneza Reshmail
“haya twende ukale eti motto mzuri!” Reshmail alimwambia yule motto naye akakubali kwa ishara ya kichwa,akiwa pekupeku akafuatana na Reshmail hadi kwenye mgahawa ulioandikwa “MAMA FRED MGAHAWA” uliokuwa pembeni kidogo ya soko kuu la Iringa.
“utamsalimia mama eeh!!” baada ya kumnunulia chakula walilipa na kumuaga
“haya mamdogo!” alijibu yule motto
“unaitwa nani vile”Eve akamuuliza
“naitwa Christian motto wa mama Bite” alijibu na wote kwenye mgahawa wakacheka
Kuifananisha na picha ya Adam,dimplez za yule mtoto zilimfananisha kabisa na Adam,achilia mbali rangi yake ya maji ya kunde na ucheshi wake.
"Eve hapana,mbona kesho naenda kumtafuta Christian ili nimjue baba yake anavyofanana,haiwezekani kufanana kwa kiasi hchi hapana "Aliongea Resh huku akiifunika album ile . Eve alikubaliana naye na siku iliyofuata majira ya saa nne,walikuwa katika hoteli ya yule mama ambapo walimwacha Christian.
"Nyie watoto ni kesi gani hyo mmetaka kuniachia jana" mama mnene kiasi mmiliki wa mgahawa wa Mama Fred aliwapokea kwa maneno hayo makali huku akifunga kanga yake vizuri kiunoni. Resh na Eve hawakuwa na jibu la kutoa walidhani amewafananisha labda "Mama ni nini tena,mbona sisi...." alijaribu kujieleza Eve huku akiishiwa maneno ya kujieleza.
"Mmenitekelezea mtoto hapa anaanza kunililia hapa usiku he! jamani mnataka mniuwe kwa presha mkurya wa watu mie" aliongea kwa ghadhabu na mshangao mkubwa sana yule mama.
"Mama sisi tumempata hapo sokoni,ndio kumleta hapa kwako kwa ajili ya kupata chakula tu mama yangu" Reshmail alinyanyua mdomo wake na kuzungumza kwa sauti iliyojaa mshangao pia.
"He! mauzauza gani haya jamani,mi nimempeleka pale kituo cha polisi usiku uleuule ndugu
----------------------------------------------------------------------
Baridi kali ya Mbeya ilikuwa imemkataa motto wa Bite (Christian) kwa hali hiyo alipotimiza miaka miwili waliondoka na kurudi tena Iringa ambapo Bite alitaka kukaa kidogo halafu aende Mwanza kuweka makazi mapya huko. Jambo la kushangaza licha ya baridi ya Iringa hali ya Christian ilianza kuwa njema kama awali jambo lililosababisha Bite aendelee kukaa katika mkoa huo.hadi anatimiza miaka mine hali yake kiafya ilikuwa njema sana na tayari Bite alikuwa amesahau suala la kwenda Mwanza.akaanzisha genge la kuuza uji na karanga mida ya jioni na mihogo ya kukaanga majira ya asubuhi. Ilikuwa biashara ndogo lakini iliyomuingizia kipato kizuri tofauti na matarajio yake.aliweza kupanga nyumba ya chumba kimoja na sebule aliyoishi na mwanae kwa furaha sana tu bila masumbufu yoyote hadi siku hiyo asubuhi alipokuwa anauza mihogo yake ambapo wanaume wawili ambao sura zao hazikuwa ngeni machoni pake walipofika eneo la biashara yake.Aliwapokea kwa furaha sana na bashasha kama wateja wengine aliozoeana nao.”Bite tukuone pembeni kidogo samahani lakini’ wawili wale walimvuta pembeni Bite
“mh! Mikopo asubuhi asubuhi hamna kwakweli mtadhalilisha hizo suti zenu” aliongea Bite kwa utani huku akiwafata walipo wawili hao
“funga biashara tunaondoka na ukithubutu kupiga kelele au kukimbia nasambaratisha ubongo wako nadhani hujawahi kufikiria kifo cha namna hiyo,hivyo basi fanya kama unavyoagizwa” aliambiwa Bite na wale wanaume huku mmoja akifunua koti lake jeusi la suti na kumwonyesha Bite kitu ambacho hakujiuliza mara mbili mbili kuwa ile ilikuwa ni Bunduki,kwa kuutambua uoga alioupata Bite,yule mwenye bunduki alimbandika kitu mfano wa kishikizo cha nguo na kumwambia “hiyo ni sound recorder nenda ukawaambie wateja wako sisi ni ndugu zako tumekuletea taarifa za msiba nitakuwa nakusikiliza hapa,ole wako nasema ole wako usifuate maelekezo” alipewa masharti hayo ya uongo Bite ambaye laiti isingekuwa pensi yake ya jinsi ambayo huwa anavaa kwa ndani ili kuhifadhia pesa zake za mauzo basi mkojo uliopenya bila yeye kujua ungemwagika palepale hadharani na wala asingepatwa ma aibu yoyote ile.Kama alivyoagizwa aliwaeleza wateja wake wawili waliokuwa wanamalizia kuitafuna mihogo waliyokuwa wameinunua,wakampa pole za dhati . jasho lilikuwa linamtoka alitamani kutumia ishara kuwaambia kwamba yupo katika hatari lakini alipowazia mdomo wa bunduki alikaa kimya kabisa,bila kificho Bite aliiogopa sana bunduki na hakupenda kumwacha Christian katika umri ule.Tayari akili ilisharudi nyuma akatambua hasa,hao watu alikutana nao wapi,walikuwa ni baadhi ya wafanyakazi katika ile ngome aliyekaa miaka miwili na ni hao waliomleta Adam pale ngomeni “nimekwisha mimi Beatrice” alijiwazia Bite huku akitetemeka.
Baada ya kuifunga biashara yake aliwafuata akiwa na mwanae amemshikilia mkono.
“nadhani unajua hatuhitaji mtoto!!! Tunakuhitaji wewe tena sasa hivi” aligombezwa Bite na bila kujijua akajikuta akimwacha mwanae pale “Christian narudi sawa nisubirie pale sokoni sawa mwanangu! “haya mama alijibu Christian kwa furaha kwani alijua amepata fursa kubwa na ya kipekee kwenda kucheza na watoto wenzake pale mtaani
“ulidhani unaweza kutuzidi ujanja sisi,umepotea sisi hatupimiki hata kidogo umeumia tena umeumia sana aliambiwa Bite na wale wanaume wakiwa kwenye gari kuelekea kwenye gari kuelekea kule katika ngome jambo hilo Bite hakulitamani hata kidogo,japo alimpata Christian kwa bahati mbaya lakini alikuwa akimpenda sana kutoka moyoni na hakuwa tayari kutenganishwa naye kwa namna yoyote ile.Alijiuliza maswali mengi sana ni nani atakayempa chakula mwanaye siku hiyo na nyingine zitakazoendelea wakati yeye hayupo,michezo ya kukimbizana aliyoipenda Chriss pia ilimtia hofu Bite na kuhisi huenda mwanae anaweza kupoteza uhai wake kwa kugongwa na gari. Funda la hasira lilimkaba kooni alitamani kufanya lolote lile wakati huo lile jambo liwe ndoto kwake, machozi yaliyotoka ndio yaliyeyusha lile fundo japo kidogo,hasira kali ilikuwa imemkaba Bite aliyekuwa amekaa siti ya nyuma na jamaa mwenye Bunduki katika koti lake lakini maskini hakuwa na la kufanya hadi gari lilipoingia ndani ya ngome ile
------------------------------------------------------------------------------------------
Macho ya Reshmail yalitawaliwa na taswira ya yule mtoto Christian,zilikuwa ni siku nyingi zimepita tangu afungue album yake kumwangalia mpenzi wake (Adam) aliyeaminika kuwa tayari ni marehemu.Ni katika usiku huu alipokuwa akipitia album ya Eveline ndipo tena anakutana na picha ya Adam ambayo yeye (Adam) alimpa Eveline walipoenda Mwanza.”Eveline,Eveline,Eve……….huyu hapa ni nani???”
“we umechanganyikiwa tena eti hebu acha mambo yake ya ajabu huyu Adam” Alijibu Eve kwa uoga.
“ na tuliyemwona leo kule sokoni ni nani??” aliuliza Reshmail
“we Reshmail jamani wanafanana Mungu wangu mbona wamefana hivyo lakini eeh!! Eve alijikuta picha ya mtoto Christian ikiumbika kichwani mwake na
Zangu kwa sababu nimekaa naye hadi saa nne tumemsubiri huyo mama yake aje wapi!! Nikaona isiwe shari ngoja nimpeleke polisi penye usalama kuepuka balaa kumbe na nyie hamjui ni wa nani he!!” alitoa maelezo hayo yule mama na kueleweka vyema kwa Reshmail na Eveline.
“hicho kituo cha polisi umesema kipo wapi?” aliuliza Eve
“kile pale kinaonekana hata kwa hapa,lile jingo la bluu nyuma yake” alielekeza yule mama
Ndani ya dakika tano tayari Reshmail na shoga yake walikuwa mbele ya mapokezi ya kituo cha polisi Iringa mjini
,na walikuwa kwenye foleni wakisubiri zamu yao ya kuhudumiwa ifike.
“nyie ni ndugu zake? Au mmoja wenu ndio mama yake?”
“hapana sisi si ndugu zake ila……”aliishia njiani katika maongezi yake Resh baada ya kukatishwa na yule askari “ila nini? Yaani nyie wanawake wa siku hizi suala la kujali watoto wenu hamtaki kabisa kulisikia mnachojali ni urembo tu wa sura zenu”
“jamani sio kwamba kuna ndugu yake hapa kati yetu ila sisi tumemkuta jana kule sokoni ndio tumemnunulia chakula halafu tukajiondokea zetu,leo hii ndio tunapita pale kwa mama Fred yule mwenye mgahawa yeye ndiye ametupatia taarifa hiyo tukaona sio vibaya nasi tukifika kumwona huyo motto” aliongea Eve aliyeonekana kutokuwa na hofu na kituo cha polisi lakini Reshmail alikuwa ana uoga kwa mbali kama vile anatuhumiwa kwa lolote lile.
“haya yupo tumemuhifadhi na tumepeleka taarifa kwenye vyommbo vya habari wataanza kutangaza kama mama yake bahati mbaya haya atakuja kumchukua na kama amemtelekeza akajiandae kwenda kuishi kwa watoto yatima sisi hatuna uwezo wa kuhifadhi watu hapa zaidi ya mahabusu” alijieleza askari yule huku akijipepea joto kwa kutumia kofia yake iliyochakaa
Majuma mawili yalipita bila mama wala ndugu wa motto kupatikana licha ya kituo cha redio maarufu mjini iringa cha Ebon fm kutangaza kila siku bila kukoma
“eve naenda kumchukua yule motto nafsi yangu inanishauri hivyo na ni lazima nifate ambacho nafsi yangu inaniamuru” Reshmail alimwambia Eve siku moja wakiwa wamekaa sebuleni wakiangalia habari katika luninga.Eve alikuwa amejenga tabia ya kutobishana na rafki yake huyo kwani furaha yake ilikuwa ni kumwona Reshmail akiwa na furaha tele
“lakini Resh,mama yake si atamtafuta ssana??”
“Eve yaani imetangazwa hivyo redioni na hajajitokeza leo hii mie tu kumchukua ndipo ajitokeze? Looh! Acha nae ahangaike kidogo” alijibu Reshmail kwa jeuri
“mh! Haya sikuwezi mwanasheria wangu”
Polisi hapakuwa na usumbufu ni wazi kwamba walikuwa wamechoshwa na matukio ya watoto kutelekezwa na wazazi wao pasipo sababu zilizo wazi,hivyo kitendo cha Resmail kuamua kumchukua Christian ilikuwa ahueni kwao.aliandiokishwa maelezo mafupi tu kabla ya kuruhusiwa kondoka na mtoto ambaye alikuwa dhaifu tayari kutokana na lishe duni na upweke wa kutomuona mama yake kwa siku hizo zote.
Reshmail alikuwa ameyafurahia sana maisha ya Iringa,kampani kubwa kutoka Eveline na mchumba wake ilibeba nusu ya furaha yake huku nusu nyingine ikikamilishwa na uwepo wa Christian mikononi mwake,mara kwa mara alipenda kuwa naye karibu huku akimwita mume wako jambo lililompa faraja kubwa moyoni
”Eve jamani nitakumiss kipenzi changu lakini nitarudi tena asanteni sana kwa ukarimu wenu mlionionyesha tangu mwanzo nimeishi kwa furaha kubwa sana hapa” Reshmail aliyazungumza hayo alipokuwa anawaaga Eve na Benny usiku ambapo kesho yake alitegemea kurejea Dar-es-salaam akiwa ameandamana na Christian mtoto aliyempata katika mazingira ya kutatanisha
Kwa Christian safari ya kutoka Iringa kwenda Dar ilikuwa safari yake ya kwanza ndefu zaidi kuwahi kusafiri
Siku iloyofuata wawili hawa walikuwa ndani ya basi la ‘budget’ litokalo Mbeya kwenda Dar likipitia Iringa.
“Mama alisema baba yupo pale kwenye ile nyumba, tushuke nikamsalimie!” Chriss aliongea hayo huku akielekezea kidole chake kwenye jingo lililoonekana kwa mbali mno kutokea pale barabarani na hapakuwa na dalili ya kuishi mtu pale hivyo Reshmail akachukulia kuwa ni akili ya utoto imemtuma Chriss kuzungumza akaamua kupuuzia
“chriss alikwambia nani we muongo!!”
“alinambia mama siku moja hivi tulipita hapa ,halafu mama alinikataza kusema uongo ni dhambi” alijieleza Christian haraka haraka
“mh! Haya tutakiuja siku nyingine sawa mfalme wangu” Reshmail alimjibu Chriss ili kumlidhisha kwa aliyokuwa anasema
------------------------------------------------------------------------------------
Nyumba tulivu kabisa ya mh.Manyama ililipuka kwa furaha kwa kurejea kwa Reshmail akiwa mwenye furaha tele “umetuletea na mjukuu!!” alitania mama Resh.”mtoto wa Eve huyu anamwita mama mdogo” Resh naye akdanganya “kazuri kweli kama………………” alisita kumalizia baba yake “ni kama Adam baba usiogope kufananisha wamefanana kweli” alimtoa baba yake wasiwasi huku akimkumbatia baba yake kasha mama yake.
“mh!! Tulikuwa wapweke kweli jamani dada” msaidizi wa kazi za ndani aliyeitwa Fatuma alimwambia Reshmail huku akimkumbatia na kumbusu shavuni
“na huyo mtoto kama mwanao vile hebu kaone” aliendelea Fatuma
“sio kama wa kwangu ila ni wa kwangu humwoni alivyonifanana?” alijibu kimzaha na wote wakacheka kwa pamoja
------------------------------------------------------------------------------------
Hali ya sintofahamu iliwakumba wale wafanyakazi wa lile jumba (ngomeni) alipokuwa anatunzwa Adam. Mkuu wa ngome hiyo bwana Lwebe alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila mbua alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila kitu kilikuwa shaghala baghala kila mara aliongea kwenye simu hukuakitoa vitisho vikali sana na hata kutishia kuua. Wafanyakazi hawakumwelewa lolote walizitambua hasira za bosi wao huyo ambaye mara chache anazokuwa katika hali kama hiyo humalizia hasira zake kwa kutoa roho ya mtu
“mlete Adam hapa mara moja !!” aliamrisha huku akijikuna ndevu zake kwa kutumia mdomo wa bunduki aliyokuwa nayo
“maskini Adam sijui amekosa nini” alijiuliza aliyekuwa anaenda kumwita. Bila wasiwasi wowote Adam akamfikia Lwebe D kwa ishara ya mkono akamwamrisha kumfuata,pamoja na mabaunsa wawili waliotinga suti nyeusi . lwebe hakuongea neno lolote hadi walipofika kwa nje,tayari kigiza cha saa mbili kilikuwa kimetawala
“mlete na yule mwingine wa nyumba ya chini” alitoa amri nyingine tena baada ya tano walioagizwa wakarejea na mtu mwingine
“we kinyamkera una bahati sana aliyekuleta hapa amesema haujasambaza taarifa zozote mbaya laiti kama ungethubutu ningeiondoa shingo yako sasa hivi. Nakuacha uende tena lakini tambua mtandao wangu upo popote katika nchi hii sasa ole wako uthubutu kunyanyua mdomo wako kutangaza ujinga” aliambiwa yule binti aliyeletwa pale huku akionyeshwa njia ya kutokea
“we kidume kwa jeuri ya bosi wako kujaribu kunidhurumu pesa yangu wakati wewe unakula na kulala bure hapa;lazima nimwonyeshe mimi ni nani na ni wewe utakayeumia” aliongea Lwebe huku akipuliza moshi wa sigara hewani.
----------------------------------------------------------------------------------
Ilikuwa ni mwezi mmoja tangu Bite arejeshwe kwenye ile ngome lakini katika chumba kingine,hakuwa msaidizi wa kazi tena bali mtuhumiwa na hakupata fursa ya kuonana na Adam hata siku moja . siku alipotolewa nje usiku na kwa mahesabu ya miaka mitano ambayo Adam angekaa pale machale yalimcheza,alivyopewa uhuru wa kuondoka hakwenda mbali sana alifika eneo moja kwenye mtaro na kuanza kusubiria ni nini kitatokea japo hakusikia vizuri maneno lakini alisubiri hata vitendo
Mkataba wa miaka mitano alioandikishana Bi.gaudensia na Lwebe wa Adam kuhifadhiwa pale ulikuwa umeisha tayari na miezi mitatu zaidi ilikuwa imepita,suala hilo la kuchelewesha pesa lilimkera sana Lwebe na pia ahadi za uongo kutoka kwa Gaudencia zilichochea sana hasira za Lwebe kufikia hatua ya kuamua kuzipooza kwa huyo Adam aliyehifadhiwa hapo.ni usiku huo alipoamua kwa mkono wake mwenyewe Adam duniani kama kisasi kwa Bi.Gaudensia
“paa!! Paa!!” mlio mkali wa risasi ulisikika na kumzindua Bite ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi pale kwenye mtalo,kidogo apige kelele lakini viganja vya mkono wake vikawahi kuuziba haraka sana. Hakusikia hata chembe ya kilio na baada ya dakika kama saba akasikia milango imefungwa
Kwa ujasiri na tahadhari kubwa Bite akajisogeza hadi karibu kabisa na eneo ambalo aliamini hakika ndipo mlio wa risasi umetokea huku kichwani kwake akiwa ana jibu la “nimesahau saa yangu” iwapo atakutana au kushtukiwa na mlinzi,kwa hofu alizurura katika lile eneo dakika tatu bila kuona chochoten”au wameingia nae ndani??” alijiuliza bila kupata jibu
“koh!! Koh!! Alishtuliwa na sauti ya kikohozi nyuma yake,mawazo yake alidhania ni mlinzi eneo lile lakini alipogeukz hakuwa mlinzi tena ni mwili wa binadamu ukiwa chini,hakutambua mara moja yule ni nani hadi macho yake yalipolizoea giza la pale “Adam!!!!!”
“we ni nani??” alijibiwa kwa sauti ya chini sana iliyokuwa inaunguruma kama mnyama anayechinjwa
“Bite mimi jamani Adam”
“ondoka watakuua hao Bite ondoka niache mi nife hapa” alijibu Adam
“hapana Adam usife,usife Adam twende tukamtafute mwanetu Chrstian anatamani sana kukuona,usife Adam tafadhali” Bite alibembeleza
Risasi mbili zilizopenya katika paja lake la kulia zilikuwa zimemsababishia Adam kuvuja sana damu na mbele yake alichokitarajia ni kifo hakuna kinginelakini maneno ya Bite nguvu zilirejea upya kabisa tena kwa kasi”Bite ulijifungua,mtoto wangu yuko wapi? Ni wa kiume au wa kike?” alihoji maswali mfululizo Adam huku akijitutumua kusimama kwa nguvu alizokuwa amezipata
“ni stori ndefu na hapa sio mahali pake tuondoke tafadhali jitahidi kuna hatari kubwa kama unampenda mwanao jitahidi tuondoke” aliongea Bite huku akiuweka mkono wa Adam katika bega lake na kuanza kumkongoja kutoka eneo lile huku (Adam) akitumia mguu mmoja na ule uliojeruhiwa ukiwa juu juu.kutoka pale walipokuwa hadi barabarani haukuwa umbali mrefu sana na walifanikiwa kufika,kwa giza nene lililokuwepo hawakuweza kuonekana na mtu yeyote,nguvu zilikuwa zinamwishia Adam kutokana na kuvuja damu lakini alijikaza kijasiri sana na kuendelea mbele
-------------------------------------------------------------------------------
Lwebe na kundi lake baada ya kumpiga risasi mbili Adam waliamini katu asingeweza kunyanyuka kutoka katika eneo lile,na hata angeweza kuinuka hakuwa na pa kwenda hakuujua mkoa huo hata kidogo. Waliingia ndani na kupiga simu kwa Bi.Gaudensia kwamba mtu wake tayari ana risasi mbili mwilini
“msimuue jamani,tafadhali sana kesho naileta pesa yenu mapema kabisa”
“nimechoshwa na ahadi zako mheshimiwa jiandae kuchukua maiti yako siku yoyote utakayotaka utaikuta nimeihifadhi na kama na kuizika nitakusaidia” alijibu kwa ghadhabu kasha akakata simu
Bi Gaudencia akapiga tena
“nakusikiliza”
“basi nielewe kwa leo na hili ni ombi la mwisho tafadhali usimuue kesho asubuhi sana nakuja huko,ninaondoka huku saa nane usiku tafadhali” alibembeleza
“na iwe hivyo atalala nje leo na hata kula hadi utakapokuja
“sawa mkurugenzi” alijibu kwa unyenyekevu Gaudensia
Akini ya Bi.Gaudensia ilifanya kazi haraka haraka akapekua kila kona katika chumba anacholala na mumewe na kwa bahati nzuri kwa akakutana na kadi ya benki ya mume wake ambayo alikuwa akifahamu vizuri kabisa namba zake za siri. Bila kupoteza muda akampigia dereva wake wa siri ambaye huwa anampeleka Iringa naye haraka haraka bila kuhoji akatii amri aliyopewa.bila Reshmail kujua Bi.Gaudensia akaondoka majira saa saba usiku,nafsi ilikuwa ikimuhukumu juu ya baya lolote litakalomkuta Adam “damu ya Adam ipo juu yangu”
“naenda kwa rafiki yangu ameugua ghafla “ mama Reshmail alimuaga mlinzi wa getini
“sawa bosi” alijibu mzee yule wa makamo huku akifunga geti baada ya mama kuwa ametoka nje
Kwa kasi ya ajabu gari iliondoka jijini Dar-es-salaam kwa kuwa ilikuwa usiku sana vizingiti vya watu wa usalama pamoja na foleni havikuwepo sana hivyo dereva alikimbiza gari kwa kadri ya uwezo wake. Breki ya kwanza ilikuwa ni katika benki ya C.R.D.B maeneo ya Ubungo ambapo mama Reshmail alishuka na kuvuta pesa kutoka katika akaunti ya akiba ya mzee Manyama
Badala ya masaa matano kwa gari binafsi kufika Iringa walitumia masaa matatu pekee
“mh!! Huku napo kijijini kweli huyo nae sijui ni mgonjwa sasa usiku huu atapata wapi lifti ya gari” mama Reshmail alimwambia dereva wake alipoona watu wawili wakisimamisha gari
“ah!! Ndo maisha ya Tanzania yalivyo” alijibu dereva huku akiongeza zaidi mwendo wa gari hadi wakaifikia ngome ya vigogo waliyokuwa wakiifua
---------------------------------------------------------------------------
Magari makubwa ya mizigo yatokayo Morogoro kwenda Zambia na Malawi ndiyo yaliyotoa msaada kwa Bite na Adam ambapo Bite alijitambulisha kama mke wa Adam na kwamba wamevamiwa na majambazi na mumewe (Adam) amepigwa risasi. Laiti kama madereva wangekuwa watanzania kwa jinsi walivyo waoga katu wasingewapandisha wawili hawa lakini wakongomani wale ambao vita kwao ni jambo la kawaida waliwachukua Adam na Bite hadi Iringa mjini walipowaacha jirani kabisa na hospitali ya rufaa.
“bila RB hatupokei mgonjwa wa aina hii” alisema muuguzi wa kike wa hospitali ile wakati Bite anajieleza.ni kweli yule muuguzi(nesi) alikuwa na haki zote za kupingana na ujio ule kwani hali aliyokuwa nayo Adam ilihitaji taarifa za polisi kwanza
“haa!!! Mama Christian,ni wewe hata siamini au nakufananisha?” wakati Bite akijiegemeza kwenye ukuta huku akiwa amekata tama alishangaa kutambulika kwake na nesi yule
“Mungu wangu mama wawili jamani!!!” baada ya kumkazia macho naye Bite akamtambua yule nesi kuwa waliwahi kufanya nae biashara katika soko la Uyole Mbeya na pia alikuwa jirani yake pale alipokuwa anaishi,ulikuwa mshangao mkubwa sana
“ehe!! Kulikoni tena ndugu yangu yamekukuta yapi tena mwenzangu?” alihoji nesi huku akiwa amechangamka sana safari hii
“ni makubwa sana,lakini ningeupata msaada wako kwanza kwa mume wangu ndio tungeongea vizuri shoga” alijibu Bite akiwa na matumaini tele
“ondoa shaka shoga huduma mnaipata sasa hivi tena huduma bora,daktari tunaheshimiana naye sana na pia ni shemeji yangu” nesi aliongea hayo huku wakisaidiana kumwingiza Adam ndani ya chumba cha wagonjwa,hapakuwa na maswali mengi,undugu ulitawala pale. Adam akafanyiwa upasuaji mdogo wa kuondoa risasi katika ambao haukuchukua hata hata nusu saa damu na maji pia vikaongezwa katika mwili wake uliokuwa dhaifu sana.kufikia majira ya saa kumi na moja alfajiri Adam alikuwa amepata nafuu kubwa na aliweza kutembea japo kwa kuchechemea
“shoga nikueleze wazi tu kwamba sisi pa kufikia hapa Iringa mimi na mume wangu hatuna! Tangu niondoke ghafla niliacha sijalipa kodi nina uhakika chumba sio changu tena kwa hiyo pa kwenda hatujui” Bite alimweleza hayo mama wawili baada ya kuwa amemsogeza pembeni ili mtu mwingine asiweze kusikia
“ondoa shaka Bite miim kwangu pana nyumba kubwa tu!! Nimejengewa na mnyakyusa mmoja,nimemweka kwenye kiganja kwangu mimi hasikii,haoni wala hasemi,ni kaka yake na huyu daktari we mwenyewe si umeona alivyowashughulikia haraka” kwa sauti ya chini kabisa nesi alijibu
Wote watatu katika teksi wakaongozana hadi nyumbani kwa nesi ni kweli nesi hakuwa na chembe ya utani hata kidogo nyumba ile ilikuwa kubwa sana na haikuwa haki kukaliwa na watu wawili pekee vilikuwa ni vyumba sita pamoja na sebule
“karibuni! Karibuni sana! Nesi aliwakaribisha walipofika nyumbani kwake.
“asante sana ndugu yangu ama kweli ishi na watu uvae viatu” alisema Bite kwa upole sana
“usijali Bite tumeishi vizuri,hatukuwahi kugombana hata siku moja,tumetwishana matenga ya nyanya kwa nini sasa nishindwe kukutendea wema!!!” nesi alimtoa hofu Bite
Chumba walichopewa kilikuwa kikubwa cha kuwatosha kabisa,kitanda cha tano kwa sita kilikuwa saizi yao kabisa. Adam alishangazwa sana na wema huo wa nesi lakini mshango wake uliongezeka maradufu baada ya kukutana na mume wa nesi siku ambayo walikuwa wakitambulishwa kwake kama shemeji zake yaani ndugu zake Bite.mzee huyu wa kinyakyusa aliyeitwa Gwakisa ni kama heshima ilipitiliza na kuwa kama anawanyenyekea wawili hawa. Adam alihudumiwa na yule daktari kana kwamba alikuwa ni mgonjwa wa kisukari au alikuwa ni mtoto wa mfalme,Adam alipata farijiko kubwa sana kuishi pale
Bite kama kawaida alikuwa mwanamke wa kujituma sana,ndani ya wiki moja tayari alikuwa amepata kazi ya ndani katika nyumba nzuri waliyoishi wanafamilia watatu,mwanaume na mke pamoja na mtoto wa kama miaka mitatu wa kike aliyekuwa anasoma shule ya awali
-------------------------------------------------------------------
“bite mama!!”
“bee mama”
“mpeleke mtoto shule halafu baadaye mpeleke pale zahanati akapimwe jana usiku amekohoa sana” ilikuwa sauti ya Eveline akimpa maelekezo Bite ambaye alikuwa mfanyakazi wake mpya na wa kwanza wa ndani ya nyumba yake na mchumba wake. Ratiba ya Bite ilikuwa ni kazi kuanzia asubuhi ya saa mbili ambapo alikuwa akimpeleka Loyce {mtoto wa kaka yake Benny} shuleni na kisha akirejea anaandaa chakula cha mchana kwa siku ambayo Benny hurudi nyumbani mchana na baada ya hapo humfuata Loyce shuleni,kisha maandalizi ya chakula cha jioni na majira ya saa kumi na mbili huaga na kuondoka,ilikuwa kazi ambayo haikumtoa jasho Bite na malipo ya shilingi laki moja kila mwezi yalimtosheleza kabisa kupanga chumba kidogo walicholipia shilingi 15000 kwa mwezi
“tunashukuru sana kwa ukarimu wenu bwana na bibi Gwakisa Mungu awazidishie baraka katika kazi zenu” alitoa shukrani za dhati Adam kwa niaba ya mke wake wa bandia (Bite).uchangamfu wake na wingi wa vituko ulifanya nyumba ya Gwakisa iwe iwe yenye shangwe na tabasamu kila siku,kitendo chake cha kuaga pale kilimsononesha Gwakisa na mkewe lakini hawakuwa na jinsi,kutoka mfukoni mwake aliwakabidhi shilingi laki mbili za kuanzia maisha yao huko waendako
Tayari Adam alianza kumpenda kwa dhati Bite uchapakazi wake na jinsi alivyomwokoa kutoka katika kifo ulichangia sana lakini kiunganishi cha mtoto Christian ndio ilikuwa chachu kubwa ya mapenzi yao.walivyohama katika nyumba yao ya kupanga walianza rasmi kuishi maisha ya mke na mume Adam hakuwa na amani hata kidogo na familia ya Reshmail hasa baada ya kukuta katika nyumba hiyo ndogo waliyohamia magazeti yaliyobandikwa kama mapambo likisema “imani za kishirikina zamwondoa mheshimiwa Manyama bungeni” alitamani sana kuisoma habari hiyo kiundani iliyotoka takribani miaka mitano iliyopita lakini ilikuwa imeandikwa inaendelea ukurasa wa pili anbao haukuwepo pale ukutani
“au walikuwa wanataka kunitoa kafara? Mungu wangu!! Niliwakosea nini mimi” alijiuliza Adam wakati wakiingiza yao ya Rambo ndani ya chumba hicho kimoja kilichotenganishwa na pazia kufanya sebule na chumba
Hisi hizo mbaya zikamfanya Adam aamue kuanzisha rasmi uhusiano na mwanamke ambaye amezaa naye mtoto pia aliyeokoa maisha yake bila kutarajia mwanamke ambaye hajawahi kumkwaza,mwanamke mpiganaji anayempa furaha tele kila siku
“Bite nataka uwe mke wangu”
“Mh!! Niwe mkeo mara ngapi mimi mkeo tayari jamani” alijibu Bite huku akichezea ndevu za Adam ikiwa ni siku ya pili tu tangia wahamie katika makazi hayo mapya
“una utani wewe mbona ulikuwa hujaniambia wala sijawahi kusikia ukiniita mume wako?
“sio lazima nikwambie tayari nina mtoto wako halafu humu ndani kuna kitanda kimoja tena kidogo tu,ulidhani chako mwenyewe!!!” aliuliza Bite kisha wote wakacheka huku wakikumbatiana na kuangukia kitandani
-----------------------------------------------------------------------------------------
Maisha ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamebadilika sana akiwa anasubiri wakati baba yake akimtafutia kazi itakayompendeza alifurahia mara zote na Christian huku akiwa amewabadili watu wote wanaomfahamu kwa ukaribu kutokea kumwita Reshmail na sasa walimwita mama Christian na alikuwa amejivika pete ya ndoa katika kidole chake cha shahada ikwa na jina Adam na nyingine ndogo akiwa amemvisha Christian ikiwa imeandikwa Reshmail.
Hakuwa mtu wa kulialia tena wala msongo wa mawazo haukumsumbua tena aliamini nafasi ya Adam ilikuwa imezibwa vyema na Christian ambaye alikuwa Adam mpya kwake. Walilala wote,walicheza wote na kusimuliana mambo mbalimbali.alipoenda kusalimia rafiki zake walienda wote Christian mkono wa kulia. Harakaharaka Christian alijikuta akimpenda mno Reshmail kuliko hata ilivyokuwa kwa mama yake mzazi,maisha ya kifahari ya kwao Reshmail yalimfanya Christian anawiri sana ungewakuta wakicheza bustanini kama vile wanalingana umri walibembea pamoja na kupigana kiuongouongo,kwa ufupi waliishi maisha ya kusisimua kwa kila aliyewaona. Akiugua Reshmail ni Christian atamuuguza kwa kukaa pembeni yake bila kutoka nje hadi apone hivyo hivyo kwa Reshmail abaye alimwogesha na kumlisha. Wakati huo Reshmail ndio alikuwa mwalimu wa Christian akimfundisha kusoma na kuandika jambo ambalo hata baba yake alilipenda na Christian alikuwa mtu anayeelewa haraka akifundishwa ,reshmail alifurahia sana.
Baada ya kukaa na Christian mwezi sita reshmail kwa mara nyingine Iringa kwa rafiki yake jambo kubwa lililompeleka huko ni harusi ya rafiki yahe huyo ambapo alitarajiwa kuwa matron wa kipenzi chake hicho.
“shoga shughuli kesho kutwa hata haujaonekana jamani au ndio mambo yetu yale haja ya kufanyiwa make up….”aliuliza kiutsni .Eve katika simu alipokuwa anaongea na Reshmail.
“Kesho asubuhi na mapema nakujua ,mume wangu alikuwa na mafua ndio tatizo si unajua tena.”alijibu Reshmail.
Haya mume huyo anavyoringiwa shauriro “alijibu Eve .Christian alikuwa amependekezwa kuwa bwana harusi mdogo pamoja na Loyce (mtoto wa kaka yake Benny).
“He unatoka mume wangu asiuze sura,na jinsi alivyoandaliwa huku Dar es salaam ,utachoka mwenyewe na simtoi mpaka siku ya shughuli,atakayeruhusiwa kumuona ni bibi harusi mdogo(Loyce) peke yake wakati wa kujifunza,sitaki mwingine amuone mpaka siku yenyewe”alijibu Reshmail kwa furaha.
“Haya umeshindwa ambao hatuna waume tunalo,alijibu Eve kisha wakaagana.
Asubuhi ya siku iliyofuata majira ya saa nne asubuhi tayari Reshmail,Christian,mpambaji pamoja na dereva walikuwa ndani ya gari la baba yake (Resh)taratibu safari ya Iringa ikaanza.
“Usitupeleke kwa kasi sawa eeh,alitoa malekezo Reshmail na kukubaliwa na dereva kwa sababu hawakuwa na haraka yeyote ila mbele yao yalikuwa bado masaa mengi sana kabla ya harusi kufanyika.
Kwa mwendo wa kinyonga kabisa gar lilifika mbele ya nyumba ya Eve majira ya saa nne usiku na hakuna aliyekuwa ameschoka sana.Shamrashamra zilikuwa kubwa sana maeneo ya pale kwa Eve kelele zilizidi alipofika Reshmail, na kama alivyoaahidi kweli alishuka yeye peke yake kutoka katika gari akifuatiwa na dereva,urembo wake utadhani alikuwa amepembwa tayari kuingia ukumbini.
“Shoga tabia gain hiyo kupendeza kuliko bibi harusi?”aliuliza eve kiutani baada ya Reshmail kuingia katika chumba ambacho Eve alikuwa amehifadhiwa akiwa na wapambaji wake.
“Hebu acha utani wako,kila mara unadhani tuko shuleni?mwone,”alijibu Reshmail,Eve akajiziba mdomo kwa aibu huku akiwatazama wapambaji wake waliokuwa wamejizuia kucheka lakini uvumulivu ukawashinda wakacheka kwa nguvu.
Chumba kile kikageuka kijiwa cha story kati ya Reshmail na Eve ,stori zingine zilikuwa juu ya mume wa Reshmail (Christian),shoga hadi pete?
“Sina utani mie mbona”?alijibu Resh huku wapambaji wakiwa hawajui hata kinachoongelewa.
“Mama kuna mtu anataka kukuona,ilikuwa ni sauti ya kike ikimueleza Eve.
“Heh!!ushazaa na wewe?”aliuliza kiutani Reshmail.Mh!!niringe huyu ni msaidizi wangu tu wa kazi anaitwa Bite,nampenda naye ananipenda pia.
“Sio kama mimi na Christian “alidakia Reshmail ambaye tangu aingie chumba kilitawaliwa na vicheko.
“Bite humuwezi huyu anaitwa mam Christian ni rafiki yangu tangu utotoni.
“Nafurahi kukufahamu mama Christian hata mimi.alitaka kuondelea kuongea Bite akakatishwa na Eve.”Anayetaka kuniona nani huyo tena?,mwambie nina mgeni Bite akajiondokea bila kumalizia kauli yake.
Sherehe ilifana kuanzi kanisani lakini mambo yote yalikuwa saa mbili usiku maharusi wadogo walipokuwa wametangulia mbele wakifuatiwa na wana ndoa wenyewe(Eveline na Benjamin)huku nyuma yao Reshmail na Fredrick wakifunika kila kitu kwa pale mbele Christian aliteka macho ya watu huku kamera zimemulika yeye. Tabasamu lake pana la wakati wote lililoonyesha vishimo katika mashavu yake yote lilisababisha watu wengine wahisi huenda sio kutoka Tanzania , suti yake iliyoendana kabisa na mwili wake na viatu vyake pia jinsi mkono wake ulivyokuwa umemshika kiustadi Loyce (bi harusi mdogo) ulimfanya MC ashindwe kukaa kimya “nani mwenyewe harusi,wa mbele,nyuma au kati” aliuliza kwa mbwembwe
“mbeleeeeeeeee!!!.......nyumaaaaa!!!!” ndio majibu yaliyosikika kutoka kwa wengi
“hayaa wageni waalikwa wanasema maharusi wa katikati wamefunika sana” alidanganya MC aliyefahamu wazi Christian na Reshmail wameteka macho ya watu wengi pengine kuliko maharusi wenyewe.
Picha zilipigwa kwa wingi lakini Christian hakuonyesha wasiwasi wowote “mh!! Katoto kazuri halafu kajanja hako” wanawake walikuwa wakinon’gonezana huku wakimtazama Christian anavyozidi kusonga mbele
“wamekatoa nje,baba yake ni mreno” alidakia mama aliyesifika kwa umbea pale mtaani aliyejulikana zaidi kwa jina la mama mwingi.hata hawakuhangaika kujibishana nae kwani walishamzoea
Taratibu kabisa kwa mwendo wa kunyata jozi hizi tatu za kuvutia ziligawanyika huku jozi mbili za wakubwa zikienda katika meza kubwa kabisa na watoto wakienda katika meza yao ndogo iliyokuwa akimeremeta soda na vinywaji vingine baridi,”kusema ukweli sherehe imependeza,siongei kama MC bali kama ndugu Kidagaa Peter Kubalunga wengi wananiita MC K.P” alichombeza Msema Chochote (MC) na kushangiliwa sana na umati mkubwa uliohudhuria sherehe hiyo.
-------------------------------------------------------------------------------
“dah!! Umependeza kweli sitaibiwa huko na wajanja,hebu ona ona mgongo wako utadhani huna mamba ulivyopendeza,ona kifua chako mpenzi wangu hapana nitaibiwa mke mie” Adam alikuwa akimtania Bite huku akim funga zipu yake ya mgongoni
“acha wivu mwanaume wewe,kaa ndani usubirie ya kwako aniibe nani wataishia kutamani tu!!” alijibu Bite huku akimun’gunya midomo yake ili lipstick aliyopakaa ikae vizuri zaidi na kioo kikiwa mbele yake
“nakupenda sana mke wangu,tambua hilo niliamua toka moyoni mwangu na wala sijutii hata kidogo najionamwenye bahati sana” Adam kwa sauti ya chini iliyomaanisha anachokisema alimwambia Bite ambaye alitulia tuli akamtazama Adam kisha akamkumbatia na kumbusu.
“nakupenda pia nakupenda sana” Bite akamwambia Adam halafu akatoka nje na kupanda teksi iliyokuwa inamsubiri kwa nje na kuondoka,Adam hakuthubutu kutoa hata pua yake nje kwani bado alikuwa na uoga wa kurejea mikononi mwa watu wabaya
Majira ya saa tatu na nusu Bite tayari alikuwa mlangoni akionyesha kadi yake ya mwaliko kwa watu wa ulinzi kisha mwanadada kutoka kamati ya maandalizi akamwongoza Bite kuelekea katika upande ambao ndugu zake na mwanamke walikuwa wamekaa,eneo la chini ya meza ya bwana na bibi harusi mdogo.Bite alikuwa tayari kama ndugu wa damu kwa Eveline walitokea kuheshimiana sana na hawakuwahi kuingia katika malumbano makubwa sana.
Amani ilitoweka katika meza ya bwana na bibi harusi wadogo,Christian alikuwa amekosa utulivu mara kwa mara alikuwa ananyanyua shingo yake aweze kuona kitu Fulani ambacho hakuna aliyefahamu ni nini kimemsibu
“au kanaumwa tumbo?” alijiuliza matron huku akienda kwenye ile meza kumsikiliza Chriss ana shida gain
“Chriss ni nini baba umekuwaje?” alimuuliza baada ya kumfikia
“nataka kwenda kwa mama” alijibu kwa sauti iliyojaa manun’guniko sana
“subiri kidogo mtoto mzuri nitakupeleka sawa” matron alimdanganya Chriss huku akiamini shida yake ilikuwa kwenda kwa Reshmail,kidogo Chriss alitulia japo bado hakuwa na katika hali ya uchangamfu kama awali
Muda wa kutoa zawadi ulipofika maharusi wote katika jozi tatu walitakiwa kuwa mbele ya umati kwa ajili ya kupokea zawadi zao.Christian na Loyce waliwekewa viti wakakaa wakati Eve,Benny,Reshmail na Fredrick walisimama wima kupokea heshima hizo
“he! We mtoto vipi? Jamani huyu mtoto kulikoni” yule mwanamke aliuliza baada ya kushikwa gauni lake na Christian alipotaka kuondoka baaba ya kutoa zawadi. Bahati mbaya muziki ulikuwa umezimwa hivyo ukumbi mzima ulishuhudia tukio hili la kushangaza
“mamaaaa!! Mamaaaa!!” Chriss alimpigia kelele alipotaka kuondoka
“Chriss…….Christian……Christian wanguuuu!!! Jamani ni mwanangu..ni mwanangu huyu” alipiga kelele mwanamke huyu,alikuwa ni Bite na tayari akili yake imemgundu Christian,watu wote waliamini amechanganyikiwa lakini alikuwa anasisitiza bado kwa maneno hayohayo. Hakika mbele yake alikuwepo mwanaye waliyepotezana zaidi ya nusu mwaka sasa na dalili za kumpata zilikuwa zimeanza kufifia. Mayowe yake yalivyozidi yakapoteza usikivu pale ukumbini na kila mtu kuanza kujiuliza kulikoni eneo lile
“mama mama mama,huyu ni mwanangu…..Christian jamani” Bite kwa sauti ya juu sana akaanza kumwambia Eveline ambaye alikuwa amekodoa macho kuangalia anachofanya Bite pale mbele
“kuna nini jamani” Reshmail alishindwa kujiuliza akamvagaa Eve na kumuuliza
“huyu ni Christian,mtoto wangu jamani mtoto wangu kabisa” alisisitiza Bite. Nguvu zilimwisha Reshmail japokuwa hakuzimia lakini alianguka chini,alishuhudia kila kitu lakini hakuweza kuzungumza,ulikuwa mshtuko wa hali ya juu sana haikuwa sherehe tena bali kasheshe,huku Bite na mayowe yake huku Reshmail akiwa chini. Wapiga picha hawakuwa mbali walilichukua hili tukio kikamilifu tayari kwa kuuza katika vyombo vya habari.
Mwanamama mwenye nguo nyeusi alikuwa anapambana kupenya katika msitu mkubwa wa watu pale ukumbini,mwanzoni hakuwemo kwenye sherehe “vimama vya Kiswahili navyo,hapo umbea tu ndo amefata humu,akipigwa hapo au akikanyagwa atamlalamikia nani” mwanaume mmoja aliyekuwa amevaa suti aliwaambia wenzake huku wakimtazama mama huyo mwenye baibui iliyovaliwa kwa staili ya ninja hasa hasa kwa waumini wa dini ya uislamu anavyopambana kwa juhudi ili apenye. Watu kwa huruma wakampisha,moja kwa moja akiwa anakimbia kwa kasi alifika mbele ya ukumbi akaanza kuzubaa na mara ghafla akakimbilia alipolala Reshmail na kuanza kutikisa
“huyu maza vipi mwehu nini? Yaani mtu ameachiwa hewa impige yeye anaenda kuweka usiku tena na manguo yake” kijana mmoja aliyekuwa amevaa jinsi kwa staili ya mlegezo aliwaambia wenzake
“tulia wewe huenda ni mamake huyo” alijibiwa na wenzake
“reshmail amka amka mpenzi” alimwambia kwa sauti ya chini.
--------------------------------------------------------------------------
Wivu wa utani utani aliouonyesha mbele ya mke wake ulukuwa unatoka moyoni mwake,Adam alihisi huko nje labda kuna mjanja anamchukulia mke wake.”ngoja nikamfumanie mtu leo” alijiwazia Adam huku akipekua pekua nguo gani anaweza kuvaa iweze kumziba sura yake asiweze kufahamika kwa urahisi mbele za watu,’baibui’ ndio jibu alilopata,harakaharaka akajitanda kwa ustadi,alifahamu vyema pesa ya mkewe ilipokuwa inahifadhiwa akajichotea kiasi kilichotosheleza kwa nauli “Mountain view” alijikumbusha jina la hotel ambayo sherehe ilikua inafanyika,ni jina alilolikariri kwenye kadi ya mwaliko.
Akiwa na baibui lake alipanda teksi ikamfikisha moja kwa moja eneo la tukio,kukuru kakara aliyoikuta pale ilimtia hofu kubwa sana aliamini lazima kuna kitu kimeharibika eneo lile hakuwaza kitu kingine bali usalama wa mkewe (Bite) moja kwa moja naye alijichanganya humo ndani n
Tofauti ya malengo yake ya kumjulia hali mkewe,macho yake yanakutana na Reshmail akiwa sakafuni na vazi lake zuri la harusi,sura yake bado ilikuwa haijasahaulika katika kumbukumbu za Adam.
Nguvu zilizokuwa zimemwisha Resh pale chini zilirejea kwa kasi kutokana na kusikia sauti ya kiume kutoka katika nguo za kike “mamaaaaaaaaaaa!!!!” alipiga kelele kwa sauti ya juu huku tayari akiwa amesimama wima akijaribu kukimbia,kamera zikageukia eneo lao tena nyingi zikimmulika mwanamke mwenye baibui (Adam). Kabla hajakimbia Reshmail alidakwa mkono wake.”Adaam……Adaaaam!!!” alipiga kelele kali zaidi wakati huuu Reshmail. Adam alikuwa amejivua baibui kwa upande wa usoni,akiwa hajapewa jibu lolote reshmail palepale alifika Bite,”Adam! Umefikaje hapa mume wangu…si ulisema hauji…” Bite aliuliza
“nini? Nani? Umemwitaje? Na huyu ni…….” Hakuweza kumaliziankauli yake wakati huu,mawazo yakauzidi nguvu ubongo wake akazimia palepale.Wakati huo Chriss alikuwa analia tu hgajui kinachoendelea,Eve na Benny walikuwa wanahaha huku na huko bila kukumbuka kwamba alikuwa na shera safi kabisa tena ya gharama za juu kabisa,Benny ndio alikuwa kama tahira hajui hata pa kuanzia alikuwa ameshtuka sana. Ilikuwa kama vita vile lakini hakuna hata aliyejeruhiwa wala aliyekuwa anapigana vilikuwa si vita vya risasi bali vita vya mapenzi. Wgeni waalikwa waligeuza tukio hilo kuwa kama filamu ya kusisimua lakini waliyokuwa wameianzia katikati bila kujua ilianzia wapi na inaenda wapi.,nani nyota wa filamu na nani adui.
***
Ni katika nyumba ya Eveline.Reshmail akiwa mbele ya Beti amepiga magoti akilia kwa uchungu
“Bite wewe ni mwanamke mwenzangu nionee huruma kwa haya niliyopitia,nimeteseka sana,nimedhalilishwa kwa ajili ya Adam,ni kwa ajili yake hadi leo mimi ni bikra,kwa ajili yake familia yake imetuchukia,kwa ajili ya Adam baba yangu haeshimiki tena mtaani kwetu,Bite sitamani mwanaume yeyote yule,ukininyan’ganya Adam na Christian mimi nitakufa Bite,ni furaha gani utaipata kwa kifo changu kwa ajili ya upendo?,sitajali huyu mtoto uliyezaa nae wala sitaumizwa na ujauzito wake uliombebea,ninakuomba Bite niache na mimi nipate furaha japo kidogo tu katika siku zangu zilizobaki hapa ulimwenguni,nisaidie niweze kurudisha upendo uliogeuka chuki kati ya familia yangu na Adam.Bite uamuzi upo mikononi mwako,ukikataa utaniumiza sana na nina uhakika nitakufa na pendo langu kwa Adam” Kilio kilimzuia kuendelea kuongea,lakini nay eye mgongoni mwake alilowanishwa kwa machozi ya Bite yaliyokuwa yanatililika muda wote wakati Reshmail anaongea,kwa hali halisi alimwonea huruma lakini pia kwa dhati kabisa aliwapenda Adam na Christian.Eve na mumewe Benny walikuwa watazamaji,wenyewe hawakuwa na uwezo wa kutoa maamuzi yoyote yale. Christian alikuwa ametulia kwenye kochi,hali ya utulivu aliyokuwa nayo ilipita siku zote.
“Adam tulipokutana unapajua,yote tuliyofanya unayajua,upendo wangu kwako nadhani unautambua pia……labda sikupangwa kuwa wako milele ndio maana aliyepangwa amejitokeza wakati muafaka,asante kwa zawadi ya penzi lako,asante kwa mtoto na huu ujauzito hii ni heshima kubwa kwako milele,neno gumu ninaloweza kulisema sasa ni kuwa kwa moyo mmoja nakuruhusu uendelee na Reshmail,nayasema haya mbele ya mama yanngu Eveline” alizungumza Bite kisha akashindwa kujizuia kuangua kilio kikuu kilichoamsha hisia za kila mtu pale ndani wote wakadondosha machozi yao. Adam,Reshmail na Bite wote kwa pamoja wakakumbatiana huku machozi yao yakitua juu ya Christian aliyekuwa ktikati yao,ilikuwa ni picha ya kusisimua na kuumiza sana.
****** *****
Kilikuwa kikao kikubwa cha familia yao Reshmail,watu wote muhimu walikuwemo jasoro mama wa familia hiyo aliyesusia kikao,mzee Manyama,Reshmail,Eve,Benny,Bite,na Paskalina walikamilisha kikao hichi,Christian alikuwa bustanini akibembea.Reshmail alikuwa anatoa siri nzito nzito za kushangaza ambazo kwa namna kubwa kabisa zilitoa taswira ya mambo yaliyokuwa yamefichika kwa muda mrefu,uhusiano wa kimapenzi kati yake na mama yake mzazi ulimwacha kila mtu mdomo wazi,Reshmail aliomba msamaha kwa hilo na alieleweka na kusamehewa. Ni katika usimuliaji wa upande wa Bite kuhusu ngome ya vigogo iliyoleta fikra za mazingira ya kupotea kwa kadi yake ya benki katika mazingira ya utata mkubwa,Benny hakuongea neno kwani yeye alikuwa kama mgeni tu katika mkutano huo.Mzee Manyama alikuwa kimya akimtafakari mkewe kwa maovu aliyoifanyia familia yake,kwa mateso aliyompa Adam na kwa uvunjifu wa amani aliouleta baina ya familia hizi mbili,kwa fedheha aliyomletea na kumvunjia heshima yake bungeni na hata mtaani,akiwa mwingi wa hasira alisimama bila kuaga na kuelekea chumbani,kwa hali aliyokuwa nayo Reshmail aliamua kumfata kwa nyuma ili asije kufanya jambo baya huko anapoenda,hasira yake ilipokelewa na na mwili wa mkewe ukiwa sakafuni,tayari alikuwa maiti. “ulistahili hukumu hii” bila kushtuka alisema mzee Manyama huku akimpisha Reshmail aingie humo ndani.
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
Mapema baada ya mazishi ya mama yake mzazi Reshmail akiongozana na Adam katika gari ya baba yake,dereva akiwa Adam walifunga safari ya kwenda Mwanza kwa wazazi wake (Adam).
“utabaki ndani ya gari nitatangulia mimi najua watakuwa wakali hao lakini wakikuona ndipo mzizi wa fitna utakapokuwa umekatwa” Reshmail alimpa maelekezo Adam ambaye alikubali kwa ishara ya kutikisa kichwa.
Gari ilipaki nje kidogo ya nyumba ya kina Adam,kama walivyoelewana akashuka Reshmail akiwa amependeza sana,akaifunga gari kwa kutumia rimoti aliyoshuka nayo na kwa mwendo wa kunyata akaanza kuusogelea mlango akausukuma akaingia ndani,kupitia kwenye kioo Adm lishuhudi Reshmail akitoweka machoni pake.
“umefata nini hapa we mchawi Adam hajakutosha unamtaka na Rosemary ngoja sasa….Rose!!!!” aliita mama Adam,Reshmail akiwa anatabasamu kwani alijua ni muda mfupi wote watakuwa na furaha kubwa. Akiwa bado hajaanza kuongea alishuhudia mama Adam akimfuata na kisu huku Rosemary akifika pale na mwiko mkubwa,wakati huu akili yake ilifanya kazi haraka akaanza kukimbia lakini nguo yake ndefu ilimsaliti baada ya kunasa kwenye geti la kutokea nje.
Kwa macho yake mawili Adam alishuhudia Reshmail akiwa chini huku watu wawili wakimshambulia kwa fujo,alijaribu kufungua mlango lakini ulikuwa umewekwa ‘loki’ sauti yake haikuweza kusikika nje alipigapiga vioo vya gari lakini hakuna aliyemsikia. Alishuhudia damu nyingi sana ikiruka juu. Kwa akili ya haraka haraka akakumbuka kushusha kioo akatokea dirishani
“mamaaaaaaaaaaaaaaa!!!” Adam akaita kwa nguvu palepale mama yake akageuka na kudondosha kisu alichokuwa nacho,”Adam mwanangu ni wewe!!!” alisema mama Reshmail huku aimfuata Adam ambaye hakumjali bali alifika alipokuwa Reshmail “Reshmail,Reshmail” “ mama na dada mmemuua mke wangu jamani mamaaaa!!” alilia Adam baada yakuona hajibiwi kitu.”A.d….am!! ninaku….fa mume wangu….ninakufa kwa furaha…..ni..meku..rudish…sha kwenu…naku…panda..sana” Reshmail aliongea kwa kujiumauma huku akivuja damu,raia wengine walikuwa katika harakati za kutafuta msaada lakini msaada mkubwa uliopatikana ni wa polisi waliowatia nguvuni mama Adam na mwanae Rosemary huku roho ya Reshmail ikimaliza muda wake palepale Igoma jijini Mwanza.kama usingekuwa ujasiri wa Adam basi tukio lile lingegharimu maisha yake,tayari mama mkwe amepotea,na sasa mpenzi wake Reshmail,mama na mdogo wake wakitupwa jela kwa kesi ya mauaji.
--------------------------------------------------------------------------------
“mapenzi yamenipotezea muda wangu nimekuwa mfungwa miaka mitano,mapenzi yameivunja vunja familia yangu,mwanamke niliyempenda ametoweka tayari tena mbele ya macho yangu,ni heri niisome hii sheria vizuri zaidi ili ikiwezekana siku moja niwatetee ndugu zangu walioko gerezani hao pekee ndio furaha yangu,kamwe siwezi kuhangaika tena na watoto wa hapa chuoni hata siku moja sidhani kama wana maana sana kwangu nikithubutu tena huend yatakuwa makubwa zaidi ya awali,usiku mwema Mosenya.” Alimaliza simulizi yake Adam,wote tulikuwa tunatokwa machozi ya uchungu,lakini lengo langu likatimia na swali la muda mrefu likapata jawabu baada ya simulizi hii kuanza kuandikwa katika gazeti la chuo.
Olivia alimalizia hadithi yenyewe niliyoisikiliza kwa makini.
“Mh ilikuwa nzuri simulizi yenyewe.”
Baaedae tulilala maana ilikuwa imefika saa tisa usiku kwa sababu hadithi ilikuwa ndefu sana.
Wakati usingizi unanipitia nilijisemea. Halafu nikalala fofofo.
MWISHO