Saturday, 18 April 2020

Alisson apona majeraha huku Liverpool ikiendelea kusubiri hatma ya ubingwa.

Alisson apona majeraha huku Liverpool ikiendelea kusubiri hatma ya ubingwa.

Alisson Becker Stock Pictures, Royalty-free Photos & Images ...
Liverpool wamethibitisha kuwa golikipa wao Alisson amepona majeraha ya nyonga yaliyomfanya akose mchezo wa ligi ya mabingwa waliobondwa na Atletico Madrid uwanja wa Anfield.

Alisumbuliwa na tatizo kidogo kwenye mazoezi na baadae akakosa mchezo wa mwezi uliopita uliouiondoa liverpool nje ya michuano kwa kupigwa 3-2 na Atletico Madrid na kupoteza sifa ya kuwa bingwa mtetezi.

Adrian alichukua nafasi ya mbrazili huyo ambaye alisababisha magoli mawili ya Marcos Llorente yaliyoleta jumla ya magoli 4-2 na wahispaniola kutinga hatua ya robo fainali.

Alisson amerusha video inayomuonyesha akirukaruka na kufanya mazoezi mbalimbali ikithibitsha kuwa nyota huyo amepona nyonga yake.

kwa sasa kipa huyo na wachezaji wenzake wanafanya mazoezi kila mmoja nyumbani kwake kwa kuepuka msongamano na kuzuia maambukizi ya virusi vya corona.

Friday, 17 April 2020

Manchester United wahamia kwa Aubameyang

Manchester United wahamia kwa Aubameyang.

Pierre.Emerick.Aubameyang.Arsenal

Imeonekana kuwa rada za Man United zimenasa kwa mshambuliaji wa Arsenal Aubameyang anayewania kiatu cha dhahabu msimu huu akiwa na magoli 17 katika ligi kuu ya uingereza. Man United wana nia ya kupeleka ofa arsenal ya kumsajili Pierre-Emerick Aubameyang.